Yanayojiri Bungeni Dodoma: Jumatano, Trh 16 Aprili 2014 - Majadiliano ya bunge zima sura ya 1 & 6

....

....Heko UKAWA Karibuni uraiani tuendeleze mapambano kuyang'oa MASHETANI !!!!
 
unapaswa kuombewa wewe ni pepo linakufata.
kwani kuna binadamu hawakuumbwa na Mungu?
muulize babu yako alikuwa anatibiwa wapi kabla ya hosptali kuletwa?
hoja yako haina mashiko

Ninapata shida na uelewa wako.
1.unafahamu tofauti ya tiba ya mganga wa jadi na tiba asilia(mimea)? mimi baba yangu alitumia tiba asilia(mimea) na si waganga wa kienyeji.
2. mimi sijaleta hoja khs tiba za mababu wa zamani,hoja nliyoleta niya mchakato wa bunge la katiba...sasa wewe sijui uliyoyaandika umeyajenga kwenye hoja gani.
3. Jifunze ustaharabu ktk majadiliano hasa unapoona mtu/watu hawajadili unachotaka wewe
 
Prof Ibrahim Lipumba leo kachafua hali ya hewa bungeni. anasema kumbe ccm ilikuwa imeshapanga serikali 2? sasa imekuwaje mmetuhita tena mkatumia mabilioni yote haya na tayari mlikuwa mmesha panga serikali 2. kweli bunge limewaka moto leoooo
 
CCM na washirika wao wanaendelea kutoa vijembe na hoja dhaifu. Kwanza wanalalama wapinzani kuungana. Wapinzani kuungana si ajabu hata Zanzibar CCM na CUF wameungana licha ya kuwa mahasimu kwa miaka mingi sana. Vyama vina sera tofauti. Tofauti hizi zinakuwepo pale vinapotafuta kuungwa mkono na wananchi katika sera zao. Lakini kwa suala lenye masrahi ya kitaifa lazima watanzania waungane bila kujali itikadi za vyama vyao.

CCM ndo wanawagawa watanzania katika misingi ya vyama vyao ili wapitishe mambo yasiyo na masrahi kwa taifa ili waendelee kupora fedha na rasrimali za wananchi. Ndo maana wanalalama sana na kuona nongwa kuona CUF, NCCR-Mageuzi na CHADEMA wameungana lakini cha kusikitisha CCM hao hao hawakulalama wakati CUF na CCM walipoungana ili kuunda serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar.

Kuhusu gharama za muungano, wizara za muungano zipo hakuna itakayoongezwa. Na kwa muundo wa serikali mbili kuna wabunge zaidi ya 70 wanaotoka zanzibar. Na kwa maana hiyo ili kuweka usawa kati ya bara na visiwaani, inamaana kuna wabunge zaidi ya 70 toka Tanzania bara kufanya idadi ya wabunge zaidi ya 140 wanaoshughulika na mambo ya muungano. Gharama hizi CCM hawazioni kama ni mzigo kwa watanzania. Lakini muundo unaopendekezwa katika rasimu, bunge la muungano litakuwa na wabunge 75 tu wa muungano. Zaidi ya wabunge 65 watapungua katika bunge la muungano. Sasa swali la kujiuliza ni hili: Je, nafasi mbili (2) au Tatu (3) za rais, makamu au na waziri mkuu wa Tanganyika ndo zitachukua gharama za wabunge zaidi ya 65 waliopungua toka kwenye bunge la muungano? CCM acheni vijembe, uongo na upotoshaji!
 


HATI IMECHAKAAA KIASI HIKI ETI ILIKUWA SEHEMU SALAMA. WHAT A SHAME!
Hii hati ndiyo iliyowatoa ukumbini ukawa imewaumiza sana wanatamani waibe tena wapate hoja tena.
 
Wahuni wote lazima wadhibitiwe ipasavyo. Hatutaki vurugu kwenye nchi yetu
 
Mimi sahizi natazama east africa tv angalau wanachambua yanayojiri huko mjengoni

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Ningekuwa Mbunge nisingeshiriki mchakato huu. Ningekaa jimboni tuu.
 
hii hati ndiyo iliyowatoa ukumbini ukawa imewaumiza sana wanatamani waibe tena wapate hoja tena.

kisheria kama hati hii ni ya kweli basi ilitakiwa iwepo kama kiambatanisho umoja wa mataifa wakati tanzania inasajilia. Lakini cha kushangaza umoja wa mataifa wanasema hawana hati yoyote ile inayotambua muungano kati ya tanganyika na zanzibar zaidi ya barua tu kuonyesha wao wameungana
 
Mzungumzaji aliyemaliza anamuomba Rais jk hawa waliotoka wakienda kumpigia magoti asikubali hata kidogo kwakuwa wamemtukana sana kwenye huu ukumbi.
 
Wamesubiri posho itoke ndiyo wakatoka hakiamungu lazima tuwakabe warudishe posho zetu hatukubali wachezee pesa zetu.
Mimi niko apa kwenye geti la ukumbi wa msekwa wanakogawana hizi posho zetu, wakianza kutoka nawabana watupe chetu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…