Yanayojiri Mapokezi ya Makamu Mwenyekiti CHADEMA Tundu Lissu, na Mkutano wa Hadhara Temeke Leo Jumatano 25/1/2023

Yanayojiri Mapokezi ya Makamu Mwenyekiti CHADEMA Tundu Lissu, na Mkutano wa Hadhara Temeke Leo Jumatano 25/1/2023

Ni Asubuhi tulivu siku ya Jumatano,

Katika Jiji hili kuu la Kibiashara la Dar es Salaam leo majira ya saa 7:35 mchana anatarajiwa kutua mwanamapinduzi wa kweli Tundu Antipas Lissu ambaye anarejea nchini mwake baada ya kulazimika kuwa uhamishoni kwa takriban miaka 6 kutokana na Jaribio la kutaka kumuua.

Tundu Lissu mpinzani mkuu wa aliyewahi kuwa Rais wa Tanzania John Magufuli anarudi nchini baada ya mazungumzo ya Maridhiano ya kisiasa yanayoendelea kati ya CCM na Chadema yaliyoasisiwa na Rais Samia Suluhu Hassan na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alitangaza mwanzoni mwa mwezi huu kuondolewa kwa zuio haramu la mikutano ya hadhara lililowekwa kinyume na Katiba na mtangulizi wake John Magufuli.

Mapokezi ya Mwanasiasa huyo mashuhuri yataongozwa na Jabali la Siasa za Tanzania na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe, Viongozi mbalimbali wa chama hicho na wafuasi wa Chadema waliojiandaa kufanya maandamano makubwa ya kumpokea.

Maandamano hayo ya Mapokezi yatakwenda moja kwa moja Mpaka Uwanja wa Bulyaga Temeke Mwisho ambapo umeandaliwa Mkutano mkubwa wa Hadhara utakaohutubiwa na Lissu kuanzia saa 8 mchana.

Kama kawaida yetu sisi wa Molemo Media tunatarajia kuwaletea kila kitakachojiri katika Mapokezi hayo tangu anabusu ardhi ya Tanzania na Kisha Mkutano mkubwa wa Hadhara katika viwanja vya Temeke Mwisho.

Akizungumza na waandishi wa Habari hapo Jana Mwenyekiti wa Kamati ya Mapokezi ya Lissu Home Coming Mchungaji Peter Msigwa aliyekuwa ameambatana na Katibu wa Kamati Catherine Ruge alisema maandalizi yote yamekamilika na Watanzania watarajie mapokezi makubwa kuwahi kutokea hapa nchini.

Msigwa alisema chama kimeandaa mapokezi hayo kutokana na mazingira yaliyomlazimisha Lissu kukimbia nchi yake na Sasa anarudi nyumbani baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuanza kurejesha nchi katika ustaarabu wa kisiasa unaotakiwa.

Kamati hiyo pia inaundwa na Baraka Mwago ambaye ni Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani.

Karibuni Sana!
Mimi nimemiss kale kalafudhi kake jamaniiii. Kananikumbusha nyumbaniii
 
Ni Asubuhi tulivu siku ya Jumatano,

Katika Jiji hili kuu la Kibiashara la Dar es Salaam leo majira ya saa 7:35 mchana anatarajiwa kutua mwanamapinduzi wa kweli Tundu Antipas Lissu ambaye anarejea nchini mwake baada ya kulazimika kuwa uhamishoni kwa takriban miaka 6 kutokana na Jaribio la kutaka kumuua.

Tundu Lissu mpinzani mkuu wa aliyewahi kuwa Rais wa Tanzania John Magufuli anarudi nchini baada ya mazungumzo ya Maridhiano ya kisiasa yanayoendelea kati ya CCM na Chadema yaliyoasisiwa na Rais Samia Suluhu Hassan na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alitangaza mwanzoni mwa mwezi huu kuondolewa kwa zuio haramu la mikutano ya hadhara lililowekwa kinyume na Katiba na mtangulizi wake John Magufuli.

Mapokezi ya Mwanasiasa huyo mashuhuri yataongozwa na Jabali la Siasa za Tanzania na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe, Viongozi mbalimbali wa chama hicho na wafuasi wa Chadema waliojiandaa kufanya maandamano makubwa ya kumpokea.

Maandamano hayo ya Mapokezi yatakwenda moja kwa moja Mpaka Uwanja wa Bulyaga Temeke Mwisho ambapo umeandaliwa Mkutano mkubwa wa Hadhara utakaohutubiwa na Lissu kuanzia saa 8 mchana.

Kama kawaida yetu sisi wa Molemo Media tunatarajia kuwaletea kila kitakachojiri katika Mapokezi hayo tangu anabusu ardhi ya Tanzania na Kisha Mkutano mkubwa wa Hadhara katika viwanja vya Temeke Mwisho.

Akizungumza na waandishi wa Habari hapo Jana Mwenyekiti wa Kamati ya Mapokezi ya Lissu Home Coming Mchungaji Peter Msigwa aliyekuwa ameambatana na Katibu wa Kamati Catherine Ruge alisema maandalizi yote yamekamilika na Watanzania watarajie mapokezi makubwa kuwahi kutokea hapa nchini.

Msigwa alisema chama kimeandaa mapokezi hayo kutokana na mazingira yaliyomlazimisha Lissu kukimbia nchi yake na Sasa anarudi nyumbani baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuanza kurejesha nchi katika ustaarabu wa kisiasa unaotakiwa.

Kamati hiyo pia inaundwa na Baraka Mwago ambaye ni Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani.

Karibuni Sana!
Asante sana Journ Molemo
 
Keshahakikishiwa ulinzi?

Kwani hukuona Mbowe alivyolindwa kule Mwanza tokea airport mpaka Furahisha? Angalia pale Gold Crest hotel, walipofikia viongozi wa CHADEMA, ulinzi wa polisi ulivyokuwa umeimarika.

Hata leo ulinzi utakuwa thabiti toka kutua kwake. Unafikiri utawala wa Samia utakuwa tayari kupata aibu ya Lisu kudhuriwa?
 
Kwsni hukuona Mbowe alivyolindwa kule Mwanza tokea airport mpaka Furahisha? Angalia pale Gold Crest hotel, walipofikia viongozi wa CHADEMA, ulinzi wa polisi ulivyokuwa umeimarika.

Hata leo ulinzi utakuwa thabiti toka kutua kwake. Unafikiri utawala wa Samia utakywa tayari kupata aibu ya Lusu kudhuriwa?
Amen
 
Kwsni hukuona Mbowe alivyolindwa kule Mwanza tokea airport mpaka Furahisha? Angalia pale Gold Crest hotel, walipofikia viongozi wa CHADEMA, ulinzi wa polisi ulivyokuwa umeimarika.

Hata leo ulinzi utakuwa thabiti toka kutua kwake. Unafikiri utawala wa Samia utakywa tayari kupata aibu ya Lusu kudhuriwa?
Kwa hiyo analindwa hadi nyumbani kwake na polisi wa selikali? Ndio alivyohakikishiwa?
 
Back
Top Bottom