LIVE Yanayojiri vita ya Israel dhidi ya Palestina na HAMAS

Live coverage on JamiiForums
Uamuzi ulipitishwa na Baraza Kuu la UN (Nov 1947), ikiwemo Marekani na USSR.

Ardhi ya Palestina zaidi ya nusu (56%) ilikabidhiwa kwa Wayahudi, huku Yerusalemu ikiwekwa chini ya usimamizi wa kimataifa.

Wayahudi walikubali mpango huo, lakini Waarabu wakakataa kuuafiki.

Mapigano ya Wayahudi na Waarabu Palestina yakazuka mara tu baada ya uamuzi wa UN.

Kufuatia vita hivyo, Israeli ilifanikiwa kuchukua maeneo mengi ya Waarabu wa Palestina, ikiungwa mkono na Mfalme Abdullah wa Transjordan (Jordan kwa sasa), ambaye hakupenda Palestina iwe nchi huru kwa sababu ya maslahi binafsi ya kutaka kuimiliki yeye.

Hadi kufikia mwaka 1950 (miaka 3 tu baadaye) Israeli ilikuwa ikimiliki 77% ya ardhi ya Palestina. Mfalme Abdullah alikuwa amejitwalia Mji wa zamani wa Yerusalemu na eneo la kati la Palestina (sasa yajulikana kama West Bank).

Wakati huu ni Waarabu wapatao 160,000 pekee ndio walikuwa wamesalia katika maeneo yaliyokuwa yakitawaliwa na Israeli.
 
Vita sio lele mama.
 
Achana nae huyo
Hana analojua ndo maana full kutukana baada ya kuona walichokitegemea Kwa isarel hakijatimia
 
Achana nae huyo
Hana analojua ndo maana full kutukana baada ya kuona walichokitegemea Kwa isarel hakijatimia
kwa miaka mingi wamekuwa wakipotosha watu humu kwa historia zao za kuchonga tulikua tunawaangalia kama hatujui.
Binafsi sikuwahi kufikiria nitakuja kuandika kuhusiana na mgogoro ule pamoja na kuujua kiundani.
This time nimelazimika sababu yanayotokea pale ni serious kwa pande zote halafu wansibuka watu kujadili kwa misingi ileile ya chuki na kupotosha.
Haiwezekani kutafuta achievements kupitia chuki na upotoshaji.
Watu wanakufa, binaadam anadharirika heshima ya mtu inaondolewa halafu watu wanadhani chuki na upotoshaji ndiyo vitatuliza hali ya mambo. Hawajui sumu wanayoitengeneza.
Waarabu ndiyo wamewaharibu kabisa Wapalestina, Wamewafanyia Wapalestina Arabanization mpaka sasa huwezi kupitia utamaduni ukamtafuta Mpalestina umtofautishe na Mwarabu.
Ni rahisi sana kwa Mpalestina kuoa au kuolewa ma Myahudi kuliko Mpalestina kuoa Mwarabu. Hayo hawayaoni kabisa,
 
Hofu na mkanganyiko umeibuka huko Gaza, baada ya Jeshi la Israel kuwaambia zaidi ya Wapalestina milioni 1 waliokwama Kaskazini mwa eneo lililozingirwa kuhamia Kusini, ndani ya saa 24 kabla ya mashambulizi ya ardhini yanayotarajiwa.
 
Isiwe taabu, tunaondoka....HAMAS pambaneni na wanaume wenzenu.

Katika picha mtoto anaonyesha aama ya Piece na Love na sisi tunamwambia "mwaaa.."

 
Technically, hakuna tofauti kati ya Mpalestina na Mwarabu. Wote ni Waarabu.

Kuna Waarabu wa Saudi, Syria, Yemen, Palestina etc.

Palestina ni geographical location ambapo wakazi wake wanaitwa Wapalestina.
 
Technically, hakuna tofauti kati ya Mpalestina na Mwarabu. Wote ni Waarabu.

Kuna Waarabu wa Saudi, Syria, Yemen, Palestina etc.

Palestina ni geographical location ambapo wakazi wake ni Wapalestina.
Technically, yeah nakubaliana na wewe.
Wapalestina sasa hivi hawana culture tofauti na ile ya Mwarabu.
Ila, wakisimama Mpalestina na Mwarabu, just kwa kuwaangalia unaweza kuwatofautisha bila kupepesa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…