LIVE Yanayojiri vita ya Israel dhidi ya Palestina na HAMAS

Live coverage on JamiiForums
kuna siku utaelewa.
 
Kwamba wamekufa shahidi wanaenda kupata mabikra ila wavaa kobasi bhana
 
Hakuna mahali niliposema kuwa "Palestine" haikuwepo!

Ulileta barua ya Napoleon kama ushahidi kwamba "Palestine" ilikuwepo ingawa sijawahi kupinga popote. Je, umeisoma vizuri hiyo barua? Unakubaliana na Napoleon kwamba "Palestine" ni "Land of Israel" na kutokana na tawala za kimabavu za madola yaliyokuwa yakiitawala "Palestine" zilipelekea Wayahudi kuishi uhamishoni kwa maelfu ya miaka?

Unaionaje hiyo perspective?

Palestine ambayo ilikuwepo maelfu ya miaka ni tofauti na "Palestina" hii inayozungumziwa hivi leo kama "taifa la Waarabu wa Kipalestina". Nimeshafafanua hii hoja kwenye post zilizopita. Na bahati nzuri, umekuwa ukileta ushahidi wewe mwenyewe unaounga mkono baadhi ya hoja zangu.

Kila ambacho umekuwa ukikileta hapa kama "ushahidi" kuhusu "Palestine" iliyokuwepo kabla ya 1947 hakithibitishi utaifa wa kile kinachoitwa "Palestina" hivi sasa kama "taifa la Waarabu wa Kipalestina".
 
OK! Ni kwa sababu gani Waarabu waliona mpango wa UN unawaminya wao? Mbadala wa kile walichokikataa ulikuwa upi?
 
Wana wa Israel (Yakoub) ni tofauti na nchi inayoitwa "Israel" iliyoanzishwa na Muingereza.
Pamoja na kwamba sikubaliani na wewe, I can say the same thing kuhusu "Waarabu wa Kipalestina".

Wapalestina wanaotajwa hivi sasa ni tofauti na Wapalestina waliokuwa wakiishi katika maeneo ya "Palestine" ya kihistoria. Uthibitisho upo kuhusu hili.
 
Hii inamaanisha whether Palestine wangekubali hizo partitions or not bado wangeondolewa tu. Maana licha ya Israel kutwaa maeneo 1948 or 1967 ila kila mwaka inajitanua tu.
I have a different perspective!

Israel kutwaa maeneo ni matokeo ya vita dhidi yake na mataifa ya Kiarabu baada ya mkwamo wa UN partition plan. Ni matokeo ya defensive war, ambapo kwa mtazamo mwingine, ni tofauti na kile kilichofanywa na Urusi nchini Ukraine (war of aggression).

Je, Tanzania ilifanya makosa kuivamia Uganda ili kumfurusha Idi Amin?

Tukumbuke maeneo ambayo ni Gaza na West Bank kwa sasa yalikuwa chini ya utawala wa "wavamizi" Misri na Jordan kabla ya vita ya mwaka 1967. Hayakuwa independent states.
 
Hoja ya Netanyahu ni kwamba wapalestina ni waarabu walivamia, na ndio hoja za hao mashetani wa west aka Zionism, ni hoja dhaifu ambayo inapingika kirahisi kwa
1. Sayansi
2. Historia
3. Dini.

1. Kisayansi wapalestina si waarabu per Se, ukipima gene zao asilimia hadi 60 zinafanana na wayahudi na watu wa kale wa kaanani, Kifupi wapalestina wana gene kali za kiyahudi kuliko hao wanaojiita wayahudi, ila Netanyahu na washenzi wenzake kila siku wanapingana na hawa wana sayansi.

2. Kidini ukisoma Conquest za kiisilamu maeneo yote Egpty, Nenda mpaka Spain Andalusia, nenda North America, Iran mpaka Mongolia huko waarabu walipeleka tu viongozi hawakujichanganya na raia husika za Hizo nchi ndio maana Egpty mpaka Leo Imepakana na Ghuba ila ukipima Dna Zao ni chini ya Asilimia 20 wana Dna Ya kiarabu.

So waarabu hawapo popote si Egpty, si Palestina, si Algeria si Morocco, Hata ukienda Iran ambayo imepakana karibu na waarabu ni Kama asilimia 2 tu dna yao ni ya Kiarabu.

Hivyo si kweli kwamba wale ni wavamizi toka Nchi za kiarabu

3. Angalia Culture Wapalestina na levant kwa Ujumla hawavai Kanzu, nguo zao tofauti na waarabu wengine, Aina zao za kucheza, vyakula vyao, na mambo mengine tofauti kabisa na waarabu wenyewe.

So wapalestina ni wapalestina, mpalestina wa Leo na aliekuwepo hapo Miaka 3000 aliopita ni yule yule, hatuna Haja ya kuzunguka, DNA pekee Inatosha kuthibitisha hili. Ashkenaz Jews Leo wana DNA dhaifu ya kiyahudi kushinda hao Wapalestina wanao waua.


Ukitaka kuelewa Mchezo wa Zionist/British wana force kila mtu awe mwarabu, Mcopt wa Egpty hataki kuitwa mwarabu ila wanalazimisha, Berbers wa Libya ama Algeria hataki kuitwa mwarabu ila anaitwa hivyo hivyo, Druze, amazhingh, Chechens, kushite, Assyrian, Samaritan na makundi kibao hapo Middle East yoyote yanajumushwa yanaitwa tu waarabu hali ya kuwa waarabu ni wale tu wanaoishi kwenye ile Ghuba.
 
Russia na Israel ni ndugu wa damu, mwaka 1948 Marekani na Russia ziliunga mkono kuanzishwa kwa Israel kwa kishindo
Basi huu udugu wa kinafiki.
Maana huko Ukraine Kuna idadi kubwa ya wayahudi na wanachapika vibaya na Russia.
Na Putin nae anashadadia harakati za Palestina .
Nahisi kiongozi wa Russia alikua na interest zake kipindi hiko kuiunga mkono Israel.
Ila Putin imekuwa tofauti.
 
Mbona unatudanganya kaka?!
Maeneo aliyoteka Israel yote ni ya kupanua Jewish state na yeye ndiye aliyeanza kuvamia hakuanza kuvaniwa.
Pia Palestine ilitakiwa kupaya uhuru Toka kwa Uingereza sip Jordan na Egypt kama unavyotudanganya hapa.
 
Hapo unatudanganya.
KABLA RAIA WA JORDAN KUANDAMANA KING ABDULLAH ALISHAMFUKUZA BALOZI WA ISRAEL NA KUIFUNGA BALOZI PALE AMMAN.
NA KUNA MIKUTANO ALIYOIKATAA YA US OFFICIALS MPAKA ALIPOSHAWISHIWA NA ELSISI NA THAMIM AL THANI.
Taifa la ghuba lililokua lategemea ulinzi was US ni Saudi Arabia na wenyewe washapatana na Iran na wameweka mkataba wa kushirikiana kiulinzi.
Labda utaje na Egypt.
 
Nimeshataja Jordan...

Mapatano ya saudia na Iran hayahusiana na huu mzozo.
 
Una hoja fikirishi mkuu...

Hata Wayahudi wa hapo Ethiopia waliohamishiwa Israel miaka ya 1980 ni wa kabila la Dani pia.

Hata Iran wapo wayahudi (japo inasemekana ni wachache kwa sasa), hawa walihamishiwa huko na mfalme wa Babeli na wameishi huko Uajemi (Iran ya sasa) chini ya tawala kadhaa za kiajemi.

Hawa Ashkenazi Jews ni wa kabila gani hasa ?

zitto junior Mathanzua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…