Uchaguzi 2020 Yanayotokea Tanzania Leo yalitokea Indonesia 1998

Uchaguzi 2020 Yanayotokea Tanzania Leo yalitokea Indonesia 1998

Hapa naona unjivunia wanakijiji kwasababu ni rahisi kuwadhibiti wasipaze sauti zao kutokana na umasikini wao. Huko vijijini inajengwa taswira kuwa wanaikubali ccm, kwakuwa mifumo na mazingira haiwaruhusu kuweka hisia zao hadharani. Huku mjini kuna watu wengi wenye uelewa wa mambo, ndio maana ccm haijivunii, maana sio rahisi kuuongopea umma kuwa wanakubalika, hiyo ndio inayopelekea matumizi makubwa ya nguvu, ushenzi na uhayawani wa wazi ili ccm watangazwe washindi maeneo ya mijini.

Laiti mazingira yangekuwa rafiki huko vijijini,hisia za wanakijiji zingekuwa wazi, lakini mazingira yaliyopo ni ngumu kwa wanakijiji kuweka hisia zao hadharani, zaidi ya wao kujifanya wanaikubali ccm kwa shingo upande. Na hata hiyo kuwa wanavijiji wanaokubali ccm sio kweli, maana wapinzani wakifika huko na kuwaamsha wote hujikuta hawaitaki ccm. Kisa cha Magufuli kupiga marufuku vyama vya siasa kuzunguka nchi nzima, ni kuhakikisha watu wa vijijini hawatoki kwenye gereza la ccm, ambalo huwa wanawatumia bila ridhaa yao.
Wanakijiji unaowaongelea wewe ni wa dhana ya watu msioishi huko.

Hivi amjajifunza kitu kutoka awamu ya tano ambapo watumishi wametakiwa kutatua kero, amjaona kwenye hizo ziara wanakijiji wanavyojielewa.

Wanakijiji halisi wanajua wanataka nini na wana demand, wanajua haki zao za msingi kama kaonewa basi atakueleza taratibu zote za kisheria alizofuata na kakwama wapi na kwa sababu zipi.

Tena wanakijiji wana uelewa wa haki zao kushinda percentage kubwa ya watu mjini. Tofauti ya watu mjini na vijijini ni priorities tu.

Sasa CCM sio mtaji wa wanavijiji eti kwa sababu wenyewe awaelewi mambo; hapana ni kwa sababu CCM aiwachukulii poa inajua wanachotaka.

Nyie nendeni huko muwaambie mnataka kuwapatia uhuru mkinyimwa kura zao sio kwa sababu awaelewi dunia inazunguka vipi; ni kwa sababu miaka yote amjawaelewa vipaumbele vyao on the basis of actual needs. CCM inawaelea na kutowachukulia poa ndio maana wana aminika zaidi.

We nenda kawaambie unataka kuwapatia uhuru halafu uone majibu yao kwenye sanduku la kura.

Halafu hakuna mkutano wa siasa uliozuiliwa isipokuwa muda wa campaign uliisha mikutano ikapigwa stop. Sasa hivi filimbi ishapigwa ruksa, ila mshaambiwa amani na utulivu kwenye mikutano sasa atutoshangaa CDM siku moja wakiamua kufanya vingine maana kauli za viongozi wao zinalenga huko.
 
Wanakijiji unaowaongelea wewe ni wa dhana ya watu msioishi huko.

Hivi amjajifunza kitu kutoka awamu ya tano ambapo watumishi wametakiwa kutatua kero, amja wanakijiji wanavyojielewa.

Wanakijiji halisi wanajua wanataka nini na wana demand, wanajua haki zao za msingi kama kaonewa basi atakueleza taratibu zote za kisheria alizofuata na kakwama wapi na kwa sababu zipi.

Tena wanakijiji wana uelewa wa haki zao kushinda percentage kubwa ya watu mjini. Tofauti ya watu mjini na vijijini ni priorities.

Sasa CCM sio mtaji wa wanavijiji eti kwa sababu wenyewe awaelewi mambo; hapana ni kwa sababu CCM aiwachukulii poa inajua wanataka.

Nyie nendeni huko muwaambie mnataka kuwapatia uhuru mkinyimwa kura zao sio kwa sababu awaelewi dunia inazunguka vipi; ni kwa sababu miaka yote amjawaelewa vipaumbele vyao based on thei actual needs. CCM inawaelea na kutowachukulia poa ndio maana wana aminika zaidi.

We nenda kawaambie unataka kuwapatia uhuru halafu uone majibu yao kwenye sanduku la kura.

Narudia tena, wanakijiji mnaojivunia wanaccm ni wale wenye uelewa finyu wa mambo. Ni matatizo gani wametatuliwa na ccm ambayo yanawalazimu kuwapa kura ccm? Au unadhani hao wapinzani wanatoka kwenye sayari ya Mars ambapo wakifika hawatawaambia matatizo yao na jinsi ya kuwatatulia? Au unadhani wapinzani wanaogombea huko vijijini hawakai huko, kiasi kwamba hawajui mahita ya hao wanavijiji? Unavyoongea hapa ni kama wapinzani ni watu wasiokaa huko vijijini, bali watapelekwa na town bus kwenda kuwaambia hao wanavijiji watawaletea uhuru. Hii aina yako ya mtazamo ndio inayokupelekea kuona kuwa ccm ina hati miliki ya watu wa vijijini.

Huko vijijini ndiko sehemu ccm inakopora kura kwa vitisho na rushwa, maana hakuna vyombo vingi vya habari, kisha inakuja kuhadaa eti inashinda huko vijijini kisa inakubalika. Mtu anayekunywa maji ya bwawani akichangia na mifugo ana kukubali kwa kipi? Hizi porojo ccm walikuwa wanazitumia zamani, kuwa wanashinda kisa wanawake wengi ndio wabawapigia kura na sio vijana. Sasa hivi vijana wa kike ni kiume wanapiga kura kwa wingi, hiyo porojo imekosa nguvu, ndio mnajifanya watu wa vijijini wanawakubali, kisa mnajua huko njia za upashanaji habari ni duni.
 
Narudia tena, wanakijiji mnaojivunia wanaccm ni wale wenye uelewa finyu wa mambo. Ni matatizo gani wametatuliwa na ccm ambayo yanawalazimu kuwapa kura ccm? Au unadhani hao wapinzani wanatoka kwenye sayari ya Mars ambapo wakifika hawatawaambia matatizo yao na jinsi ya kuwatatulia? Au unadhani wapinzani wanaogombea huko vijijini hawakai huko, kiasi kwamba hawajui mahita ya hao wanavijiji? Unavyoongea hapa ni kama wapinzani ni watu wasiokaa huko vijijini, bali watapelekwa na town bus kwenda kuwaambia hao wanavijiji watawaletea uhuru. Hii aina yako ya mtazamo ndio inayokupelekea kuona kuwa ccm ina hati miliki ya watu wa vijijini.

Huko vijijini ndiko sehemu ccm inakopora kura kwa vitisho na rushwa, maana hakuna vyombo vingi vya habari, kisha inakuja kuhadaa eti inashinda huko vijijini kisa inakubalika. Mtu anayekunywa maji ya bwawani akichangia na mifugo ana kukubali kwa kipi? Hizi porojo ccm walikuwa wanazitumia zamani, kuwa wanashinda kisa wanawake wengi ndio wabawapigia kura na sio vijana. Sasa hivi vijana wa kike ni kiume wanapiga kura kwa wingi, hiyo porojo imekosa nguvu, ndio mnajifanya watu wa vijijini wanawakubali, kisa mnajua huko njia za upashanaji habari ni duni.
Sito kupa pointers zote hila jibu izo chache

CDM wanasera gani katika kutatua mashamba pori maeneo ambayo wanakijiji wanahitaji ardhi au wanamaoni gani ya kutatua migogoro ya wafugaji na wakulima? Ata kama ilani mpya ujaiona wewe, iliyopita ilikuwa na maono gani juu ya hayo mambo.

Vipi kuhusu afya na elimu vijijini?

Lissu ndio kwanza anakwambia miaka yote ilani zimekuwa maandishi tu, hoja ni kupata uhuru. Sasa nenda na agenda hiyo halafu muone kitakachowapata.

Tatizo lenu asilimia kubwa ya wana CDM mna perception ya maisha ya mjini na mnashindwa kuangalia maisha kwa jicho la mkulima ndio maana communication vijijini inawashinda.
 
Kama mifumo ipo tunahitaji serikali itayaoweza kuikarisha Law and Order na kwanini miaka 60 ya itawala wa CCM hilo limeshindikana?
Ndio maana nimemwambia tokea mwanzo tuliitaji kiongozi mwenye utashi sio mfumo, mfn toka mwanzo kulikuwepo na sheria ya kunzuia rushwa ktk uchaguzi, ni mfumo umewekwa akaja kiongozi akabadirisha kidogo anasema itaitwa takrima au ukarimu, hebu tazama hapo mfumo haufahi kama utapata kiongozi mwenye utashi, maana mtu ndiye anayeendesha uo mfumo sio mfumo unaendesha mtu. Ungelikuwa umeisha fanya kazi kwenye mshirika ya umma ungerielewa hili ninalolisema, anaweza akakuta uo mfumo akiona unambana anabadilisha na akuna wa kuoji, ukioji tu unapewa barua ya ovyo. Me Kwangu tunaitaji watu sahii wa kuongoza sio mfumo
 
CCM ni wajanja mno wanacheza na hesabu yan numbers wanajua tuguse wap na wap tuache chadema ngome kuu ilkua n Arusha Kilimanjaro na mwanza sasa chadema wenyewe wakiulizwa ngome zao ni wap watakwambia tuna vijana wasomi na waliokosa ajira na wote waishio mijini WAKATI kimahesabu humo kura zinagawanyika CCM saiz inabase kubwa Kanda ya ziwa yote Kanda ya Kati njoo Arusha manyara Kilimanjaro na Tanga nenda pwani na dar es salaam CCM inauhakika bado mikoa Kama rukwa tabora mbeya mingine iliobakia kura zinagawanyika CCM cuf act na Chadema
 
Hakuna mpinzani atampigia Membe wakati Lisu yupo. Hata 2015 ilisemekana kura za wapinzani zitagawanywa na ACT, lakini kura alizopata mama Anna hata milioni hazikufika.
Binafsi naona Membe akipunguza kura za Magufuli
 
Sito kupa pointers zote hila jibu izo chache

CDM wanasera gani katika kutatua mashamba pori maeneo ambayo wanakijiji wanahitaji ardhi au wanamaoni gani ya kutatua migogoro ya wafugaji na wakulima? Ata kama ilani mpya ujaiona wewe, iliyopita ilikuwa na maono gani juu ya hayo mambo.

Vipi kuhusu afya na elimu vijijini?

Lissu ndio kwanza anakwambia miaka yote ilani zimekuwa maandishi tu, hoja ni kupata uhuru. Sasa nenda na agenda hiyo halafu muone kitakachowapata.

Tatizo lenu asilimia kubwa ya wana CDM mna perception ya maisha ya mjini na mnashindwa kuangalia maisha kwa jicho la mkulima ndio maana communication vijijini inawashinda.

Sera kitu gani bwana, kama issue Ni Sera mbona nchi hii ni masikini mpaka leo, wakati miaka yote ccm ilikuwa inahubiri sera? Hiyo sera ni kama maneno matamu ya kumtongezea mwanamke, unaweza uwe na sera na ukafanya kinyume chake, ili mradi matatizo na mahitaji ya wananchi unayatatua kwa uwezo wako.

Na kwa taarifa yako watu masikini kabisa nchi hii ni hao wakulima, watu wengi wa vijijini wanatamani kuondoka vijijini kuja mjini, kuliko kinyume chake. Ukiona mtu anaondoka mjini kurudi kijijini, ujue maisha ya mjini yamemshinda, hivyo anarudisha mpira kwa kipa. Ccm dio chama kimeongoza nchi hii miaka yote, kama hao wananchi wa vijijini wanaimani na ccm na sio kuwa wanashurutishwa kuichagua ccm, kwanini ni masikini wa kutupwa mpaka leo?

Kwa taarifa yako unaweza kuongoza nchi hii bila ilani, maana sehemu kubwa kwangu naona ilani ni kama list ndefu ya mahitaji ya wananchi, tena ni list isiyo na mtiririko maalum wa kuitekeleza.

Hata mimi nikiwa rais naweza kuiongoza nchi hii bila ilani, nitakachofanya nikikusanya kodi nitapeleka huduma za jamii maeneo mbalimbali ya nchi, na kwakuwa nchi hii ni masikini huduma yoyote nitakayopeleka eneo lolote itakuwa ni sawa, hata kama sio kipaombele chao. Mfano wa nisemacho, ukienda huko vijijini unakotambia kote kuna uhitaji wa shule, maji, barabara, hospitali nk. Lakini unaweza kukuta kipaombele cha kijiji husika ni maji, kisha vingine baadae, lakini kwa utashi wangu naweza kuanza na barabara, kisha shule na vyote nikawa sawa kutokana na umasikini wao, japo kipaombele ni maji. Hivyo ndivyo nchi yetu inavyoendeshwa hivi sasa. Sasa kama unaweza kuongoza nchi kwa utashi wa rais, ilani na sera si ni sehemu ya kifurahishia genge?
 
CCM ni wajanja mno wanacheza na hesabu yan numbers wanajua tuguse wap na wap tuache chadema ngome kuu ilkua n Arusha Kilimanjaro na mwanza sasa chadema wenyewe wakiulizwa ngome zao ni wap watakwambia tuna vijana wasomi na waliokosa ajira na wote waishio mijini WAKATI kimahesabu humo kura zinagawanyika CCM saiz inabase kubwa Kanda ya ziwa yote Kanda ya Kati njoo Arusha manyara Kilimanjaro na Tanga nenda pwani na dar es salaam CCM inauhakika bado mikoa Kama rukwa tabora mbeya mingine iliobakia kura zinagawanyika CCM cuf act na Chadema

Kama ccm ina base kila mahali ndani ya nchi hii, kipi kilifanya uchaguzi wa SM ubakwe?
 
Linatakiwa dodoki la kusafisha akili za watu wanafiki, hapa kwetu inatakiwa tuanze na vyombo vya habari vile ambavyo picha inaonekana lakini sauti haisikiki
Nikufuta vyombo vyote vya habari na marufuku ya wanahabari ndani ya vyombo hivyo kuendelea kufanya hiyo kazi.

Tupate kizazi tofauti kabisa kwenye tasnia hii.
 
Nchi ina miaka zaidi ya 50 haina maendeleo kabsa licha ya kuwa na rasilimali nyingi kuliko mataifa mengi Duniani, kama siyo CCM mda huu Tanzania ingekuwa ni makao makuu ya UN ingekuwa ni level ya Marekani, German, Japan, china, UK, Oman, India , Rusia na mataifa yote Tajiri yaliyosalia Duniani ikiwemo canada, korea kusini nk, Mda huu Rais wa Tanzania angekuwa ndiyo Rais wa ulimwengu akikohia Dunia nzima inatetemeka, CCM imefuja pesa nyingi kwa mambo yasiyo na tija kwa Taifa, Mfano sasa Pesa nyingi inapotelea kwenye kuwanunua wabunge madiwani kurudia chaguzi ndogo kwa gharama kubwa kuwalipa watengeneza propaganda mabilioni , cyprian Musiba ametajirika kwa mgongo wa kuihujumu kuudhofisha kudidimiza demokrasia, na endapo CCM wangezitumia hizo pesa kujenga viwanda kila kata, vyuo vikuu kila wilaya, Hosptal za rufaa kubwa zenye madaktari Bingwa kila mkoa, barabara vijijini kote, daraja toka Dsm mpaka Zanzibar na pemba, wangevuna kura pasipo kutumia nguvu kulazimisha CCM kupendwa, wananchi wanataka maendeleo kulingana na pesa zilizopo siyo kutumia pesa zao kukandamiza demokrasia.
Sasahivi vyote Magufuri ulitaka avifanye Kwa miaka mitano aliyeongoza? Amenunua ndege tu makerere yaliopigwa sio ya nchi hii eti zinamsaidia nini mtanzania anaitaji maji hospatal elimu nk, kujenga ukuta mererani ili kuzuia madini yastoroshwe nayo ikawa nongwa eti anaharibu ela, kahamashisha ujenzi wa viwanda ili tuuze mali zilizo ongezwa samani mnasema ela angewekeza kwenye kilimo, wakati miaka yote tunaona mazao yanaozea shambani, amejenga reli ya kisasa, pamoja na bwawa la kusalisha umeme ili watu wapate unafuu wa maisha bado mnaita wait elephant, eti nimiradi ambayo airudishi Faida Kwa haraka. Mnataka ajira sijui ajira zinashuka kutoka mbinguni. Wanadamu hawana shukurani hata ufanye mazuri kiasi gani
 
hizi ni akili za kuchora, kamwe hatutawahi fika popote ikiwa tutafanya mambo ajili ya kuwaridhisha mabeberu.
Kwani unapombakizia kesi mtu unamridhisha nani.? Hivi mlivyowanyima watu zaidi ya 50000 vitambulisho mnamridhisha nguruwe?
 
Kura za Lissu zitapunguzwa na Membe
Kwa kifupi upinzani unajitafuna wenyewe

ukawa ulishindwa sasa nashangaa kila mmoja yuko kivyake anataka kushinda mpaka membe ana uhakika wa kushinda sasa sjui tutaongozwa na wangap
 
Sasahivi vyote Magufuri ulitaka avifanye Kwa miaka mitano aliyeongoza? Amenunua ndege tu makerere yaliopigwa sio ya nchi hii eti zinamsaidia nini mtanzania anaitaji maji hospatal elimu nk, kujenga ukuta mererani ili kuzuia madini yastoroshwe nayo ikawa nongwa eti anaharibu ela, kahamashisha ujenzi wa viwanda ili tuuze mali zilizo ongezwa samani mnasema ela angewekeza kwenye kilimo, wakati miaka yote tunaona mazao yanaozea shambani, amejenga reli ya kisasa, pamoja na bwawa la kusalisha umeme ili watu wapate unafuu wa maisha bado mnaita wait elephant, eti nimiradi ambayo airudishi Faida Kwa haraka. Mnataka ajira sijui ajira zinashuka kutoka mbinguni. Wanadamu hawana shukurani hata ufanye mazuri kiasi gani

shida sio kwamba binadam hatuna shukrani ni kuna mbulula chache zmekosa cha kuongea
 
Kamsalimie che nkapa huko aliko
Mkapa alitimiza wajibu wake, ameacha arama, sasahivi imepunzika sio kama wewe kila siku ni kulaumu serikali utafikiri serikali ndio iliyokuzaa, baada ya kulaumu baba yako aliyeshindwa kukupereka shule
 
Endelea kujifariji wakati kuna wakulima, Askari, watumishi wa umma, vijana kila mmoja amekata tamaa ya maisha katika serikali hii.
Nani kakuambia. Yaani mnapenda kujipa moyo. Tuulizeni sisi tunao zunguka hii nchi japo kidogo ndio tunajua. Wapinzani wa nyuma ya keyboard mnashida.

Niseme tu ni mtu mjinga wa kiwango cha juu atataka upinzani kwa sasa.
 
Ukiona mtu kachotwa na propaganda za kijinga kama ulivyochotwa wewe basi ujue kuna mambo mawili hapo;
1. Ana elimu ndogo kuweza kuelewa mambo.
2. Amesoma lakini ni mvivu wa kujisomea na kufanya utafiti hata katika mambo madogo madogo. Kifupi ni mbulula.

Naomba uniwie radhi kwa kukueleza ukweli.
maneno ya hovyo ndo faraja yenu bt nikuhakikishie kua uzalendo ni bora zaidi kuliko kutumika na mabeberu.
 
Mkapa alitimiza wajibu wake, ameacha arama, sasahivi imepunzika sio kama wewe kila siku ni kulaumu serikali utafikiri serikali ndio iliyokuzaa, baada ya kulaumu baba yako aliyeshindwa kukupereka shule
Jifunze kwanza kuandika kiswahili sanifu. Kuna makosa tele katika bandiko hilo.
Sio ajabu nyinyi ndio mtaji wa ccm.
 
Nani kakuambia. Yaani mnapenda kujipa moyo. Tuulizeni sisi tunao zunguka hii nchi japo kidogo ndio tunajua. Wapinzani wa nyuma ya keyboard mnashida.

Niseme tu ni mtu mjinga wa kiwango cha juu atataka upinzani kwa sasa.
wapinzani wa tanzania wao wanajua upinzani kupinga ovyo tu, watizame miradi mikubwa aloianzisha rais hadi kenya wanaweweseka maana wanajua ikikamilika itatupa mapato makubwa yatakayotufanya tushike usukani wa uchumi EAC, bt mbuzi hawa wao nikutaka siasa za kuwafurahisha waume zao mabeberu tu.
 
Back
Top Bottom