PakiJinja
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 11,689
- 25,848
Yanga kwa maana ya viongozi na wachezaji, Ushindi wenu na dhidi ya Rivers United kule Nigeria ni chachu tu kuelekea safari amnayo bado ni mdefu pamoja na kuonekana kama safari iliyobaki hatua tatu tu.
Waacheni mashabiki wenu wafurahie pia wajigambe, lakini ninyi wakati wenu wa kujipongeza haujafika, bado mna vita kubwa mbele yenu, pia deni kubwa la kulipa, deni litokanalo na imani na matarajio makubwa ya wapenda soka juu yenu.
Mechi ya kesho hampaswi kucheza kama wale mlioshinda mechi ya awali, mechi ijayo mnatakiwa muendelee kutafuta matokeo. Mechi ijayo mnapaswa kuichukulia kama fursa ya pekee ya kujiandaa na mechi itakayofuata, fursa ambayo ni lazima iwapatie matokeo.
Tabia ya kucheza kwa hisia kuwa mmeshashinda mechi ya kwanza hivyo mna kazi nyepesi ya kufanya mnapaswa kuifuta, hiyo ni tabia ambayo ni unprofessional. Kumbukeni, mechi hii ni ni sehemu ya majukumu yenu kwa timu. Wapenzi, wanachama na mashabiki wanahitaji burudani itakayowaletea matokeo, jawaji kuangalia timu iliyoshinda mechi iliyopita bali wanakuja kuangalia timu yenye uwezo inayoelewa maana ya mashindano na kutafuta matokeo kwenye kila mechi.
Haya kwenye ligi, hampaswi kubweteka sababu ya pengo la point kati yenu na timu nyingine, bali muendelee kuheshimu timu nyingine kwa kuendelea kupambana nao hadi mwisho.
Waacheni mashabiki wenu wafurahie pia wajigambe, lakini ninyi wakati wenu wa kujipongeza haujafika, bado mna vita kubwa mbele yenu, pia deni kubwa la kulipa, deni litokanalo na imani na matarajio makubwa ya wapenda soka juu yenu.
Mechi ya kesho hampaswi kucheza kama wale mlioshinda mechi ya awali, mechi ijayo mnatakiwa muendelee kutafuta matokeo. Mechi ijayo mnapaswa kuichukulia kama fursa ya pekee ya kujiandaa na mechi itakayofuata, fursa ambayo ni lazima iwapatie matokeo.
Tabia ya kucheza kwa hisia kuwa mmeshashinda mechi ya kwanza hivyo mna kazi nyepesi ya kufanya mnapaswa kuifuta, hiyo ni tabia ambayo ni unprofessional. Kumbukeni, mechi hii ni ni sehemu ya majukumu yenu kwa timu. Wapenzi, wanachama na mashabiki wanahitaji burudani itakayowaletea matokeo, jawaji kuangalia timu iliyoshinda mechi iliyopita bali wanakuja kuangalia timu yenye uwezo inayoelewa maana ya mashindano na kutafuta matokeo kwenye kila mechi.
Haya kwenye ligi, hampaswi kubweteka sababu ya pengo la point kati yenu na timu nyingine, bali muendelee kuheshimu timu nyingine kwa kuendelea kupambana nao hadi mwisho.