Yanga hakuchukua ubingwa (1985, 1989,1992,1993 na 1998) Wametuchomekea kwenye orodha yao

1985 Ubingwa Bara - Yanga
Ubingwa Tanzania- Majimaji ya Songea

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
Hapo ndipo kwenye hoja

Ukiangalia miaka hiyo mitano ambayo mleta uzi kazianisha ni kwamba Yanga alikuwa ni bingwa wa Tanzania bara na hakuwa bingwa wa ligi ya Muungano.
Mwaka 1985 na 1998 bingwa wa ligi ya Muungano alikuwa ni Maji Maji lakini Bingwa wa ligi kuu Tanzania bara alikuwa ni Yanga.
 
Kabla 1997 premier league ilikuwa inahusisha timu zipi!?
Kwanza tuwekane sawa, unazungumzia premier league ya upande upi?
Kama unazungumzia Tanzania bara ni kwamba premier league iilihusisha timu za kutoka Tanzania bara. Kama unazungumzia ligi ya Zanzibar basi ilihusisha timu za kutoka Zanzibar.

N.B
Kwenye vitu vya Muungano na visivyo vya Muungano, michezo ni moja ya vitu ambavyo havipo kwenye muungano. Na ndio maana baadae ikaanzishwa ligi ya muungano, kwavile Zanzibar hakuwa mwanachama wa CAF.
 
Sasa ngoja nikufundishe kitu. Ndio maana unahangaika sana. Ninajaribu kukupa ndo ndo bado huelewi.

Premiere League is the top league in the country according to regulations of the association.

League ilikuwa inabadilika badika kipindi kile. Lakini top league ilikuwa ya Muungano ndiyo ilikuwa Premier League.
Kulikuwa na namna tofauti ya kuwapata wawakilishi toka bara na visiwani.

Mfano mwaka 2000 ligi ilianza kwa mashindano ya kikanda. Baada ya kupata washindi wawili wawili kutoka kila kanda team ziliingia kwenye playoff, baada ya play off tukapata washindi. Wakaingia kukipiga. Upande wa bara Mtibwa aliibuka mshindi.

Baada ya hapo wakaingia kwenye ligi kuu. Inayojumuisha Bara na visiwani.
Ndipo yanga akaibuka mshindi.

Reference nakupa hii hapa:-

 
Ndio maana nimekuuliza TFF ilianza lini!? Na ilianza kwa sheria ya bunge au walijiamulia wenyewe!? Fatilia kabla ya TFF mpira Tanzania uliendeshwaje.
 
We kweli 1 2 7 7 aka mtambo.
 
Basi yanga ni mabingwa wa tanganyika mara 22,na hawakuwahi kuwa mabingwa wa Tanzania
 
Naona Venus Star, anahoja na kabla ya kuweka uzi wake hapa alijiridhisha na taarifa juu ya hoja yake.

Na kimsingi, Watu wanashindwa kumjibu hoja yake, kwanini kwenye official website Yanga wameandika wamechukua kombe la ligu kuu mara 27, lakini ukihesabu miaka haifiki idadi ya 27.
 
Basi yanga ni mabingwa wa tanganyika mara 22,na hawakuwahi kuwa mabingwa wa Tanzania
Huwa wanajinasibu kuwa ni mabingwa wa Tanzania bara mara 27. Sasa mleta uzi aje aseme hiyo miaka aliyoiweka hapo ni timu gani zilizochukua ubingwa wa Tanzania bara.
 
Kwanzia mwaka 1982 kulikuwa na ligi ya Tanzania bara, ligi ya Zanzibar na ligi ya Muungano. Top three kutoka ligi ya Tanzania bara wanakutana na top three ya ligi ya Zanzibar katika ligi ya muungano. Hivyo mwaka 1985, 1989, 1992, 1993, 1998 Yanga alikuwa bingwa wa ligi Tanzania bara, ila ubingwa wa ligi ya Muungano ilichukuliwa na timu nyingine mfano maji maji mwaka 1985, 1998
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…