Yanga ichukuliwe hatua kwa uharibifu iliyofanya juzi uwanja wa Mkapa

Yanga ichukuliwe hatua kwa uharibifu iliyofanya juzi uwanja wa Mkapa

Video zote mnazopost hakuna hata moja inayoonyesha mashabiki wa Al Ahly wakirusha viti. Wengine mnajitoa ufahamu na kulalamika mashabiki kukanyaga viti utadhani hamjawahi kwenda uwanjani.

Video hii hapa chini inaonyesha nini kilitokea. Angalia nani walianza kurusha viti na vitu vingine. Kama hii haitoshi semeni nitume zingine.
Ndugu kwa akili ya kawaida tu mpaka hao walioko chini kugeukia kuangalia juu sababu ilikua ni nini? Usianze tu kusema nani kaanza kurusha kwakua video yako ndio imeanzia hapo. Inaonyesha ugomvi ulitokea juu na sio rahisi wa chini kuanzisha ugomvi kutokana na hayo mazingira yalivyo.

Ushabiki usiwatie upofu tumieni bongo zenu vizuri
 
Ndugu kwa akili ya kawaida tu mpaka hao walioko chini kugeukia kuangalia juu sababu ilikua ni nini? Usianze tu kusema nani kaanza kurusha kwakua video yako ndio imeanzia hapo. Inaonyesha ugomvi ulitokea juu na sio rahisi wa chini kuanzisha ugomvi kutokana na hayo mazingira yalivyo.

Ushabiki usiwatie upofu tumieni bongo zenu vizuri
Unazungumza mambo ya kufikirika wakati uhalisia unauona. Halafu wakati huo huo unasema "Ushabiki usiwatie upofu"
 
Juzi katika mechi ya Yanga vs Al Ahly uwanja wa Mkapa, mashabiki wa Yanga waling'oa viti na kuwarushia mashabiki waliokuwa wanaishangilia Al Ahly. Inteligensia yangu imeniambia kuwa mashabiki wa Yanga walifanya hivyo baada ya kuudhiwa na kitendo cha mashabiki wa Al Ahly kuwasha moshi uliosambaa upande walilokuwa.

Nakumbuka mwishoni mwa msimu uliopita, Yanga walifanya gwaride na kwa wingi wao walipita mtaa wa Msimbazi ili kuikebehi Simba na wakawasha fataki na moshi. Wengine walidai ule ni utani wa jadi ila tunasahau busara huwa inatumika hata viwanjani kuwatenganisha mashabiki wa pande mbili pamoja kwamba huo utani wa jadi upo.

Nakumbuka baada ya gwaride la Yanga niliwahi kusema, siku mashabiki wa Simba wakisherehekea kwa kupita makao makuu ya Yanga na kufanya kile kile walichofanya Yanga, mashabiki wa Yanga watawafanyia vurugu. Leo maneno yangu yanathibitisha kuwa hilo litakuja kutokea.

Tukio walilofanya mashabiki wa Yanga kupita na kuwasha moshi mtaa wa Msimbazi lingeweza kuleta maafa makubwa sana, tushukuru tu ustaarabu ulioonyeshwa na mashabiki wa Simba. Kama maafa yangetokea, wa kulaumiwa wangekuwa ni vyombo vya ulinzi na usalama vilivyoruhusu jambo lile kufanyika.

Kitendo walichofanya Yanga kimelitia dosari taifa. Tunategemea Mwenyekiti wa chama cha vilabu Afrika ambaye uzuri alikuwepo uwanjani, atoke hadharani aikemee klabu ya Yanga kwa kitendo hicho na pia TFF waipigishe faini klabu ya Yanga na kupewa onyo kali.
UWANJA SI UMEFANYIWA MAREKEBISHO?? SI UNA CAMERA WAKAMATWE WAFUNGWE MIAKA 2 , 2 THN UTAONA KAMA KUNA MLEVI ATASUBUTU KUNG'OA KITI.
 
Juzi katika mechi ya Yanga vs Al Ahly uwanja wa Mkapa, mashabiki wa Yanga waling'oa viti na kuwarushia mashabiki waliokuwa wanaishangilia Al Ahly. Inteligensia yangu imeniambia kuwa mashabiki wa Yanga walifanya hivyo baada ya kuudhiwa na kitendo cha mashabiki wa Al Ahly kuwasha moshi uliosambaa upande walilokuwa.

Nakumbuka mwishoni mwa msimu uliopita, Yanga walifanya gwaride na kwa wingi wao walipita mtaa wa Msimbazi ili kuikebehi Simba na wakawasha fataki na moshi. Wengine walidai ule ni utani wa jadi ila tunasahau busara huwa inatumika hata viwanjani kuwatenganisha mashabiki wa pande mbili pamoja kwamba huo utani wa jadi upo.

Nakumbuka baada ya gwaride la Yanga niliwahi kusema, siku mashabiki wa Simba wakisherehekea kwa kupita makao makuu ya Yanga na kufanya kile kile walichofanya Yanga, mashabiki wa Yanga watawafanyia vurugu. Leo maneno yangu yanathibitisha kuwa hilo litakuja kutokea.

Tukio walilofanya mashabiki wa Yanga kupita na kuwasha moshi mtaa wa Msimbazi lingeweza kuleta maafa makubwa sana, tushukuru tu ustaarabu ulioonyeshwa na mashabiki wa Simba. Kama maafa yangetokea, wa kulaumiwa wangekuwa ni vyombo vya ulinzi na usalama vilivyoruhusu jambo lile kufanyika.

Kitendo walichofanya Yanga kimelitia dosari taifa. Tunategemea Mwenyekiti wa chama cha vilabu Afrika ambaye uzuri alikuwepo uwanjani, atoke hadharani aikemee klabu ya Yanga kwa kitendo hicho na pia TFF waipigishe faini klabu ya Yanga na kupewa onyo kali.
hao sio washabiki wa yanga
 
Kibonde wa mkiani uto
5imba mnajifariji kwa matokeo ya Yanga,mnazani ndio changamoto zenu za kula tano na kudroo mechi tatu mfululizo zitamalizika.

Yaani mpaka mnasusia mechi, mtazani mmelazimishwa kuwa mashabiki wa 5imba.

Maana juzi mmetoka 5000 mpaka 3000,ila hamkujaza hata robo ya uwanja. Mechi ijayo na Wydad ukiwa na MoXtra na kipande cha sabuni unaingia uwanjani,maana hata nyinyi mshaichoka timu yenu.
 
UWANJA SI UMEFANYIWA MAREKEBISHO?? SI UNA CAMERA WAKAMATWE WAFUNGWE MIAKA 2 , 2 THN UTAONA KAMA KUNA MLEVI ATASUBUTU KUNG'OA KITI.
Kibongobongo kufungia mshabiki binafsi si uamuzi unaoweza kutekelezeka. Dawa ni kuilima faini klabu husika. Hata CAF huwa wanatoza faini klabu kwa vitendo vya mashabiki wake na hawadili na mshabiki mmoja mmoja
 
5imba mnajifariji kwa matokeo ya Yanga,mnazani ndio changamoto zenu za kula tano na kudroo mechi tatu mfululizo zitamalizika.

Yaani mpaka mnasusia mechi, mtazani mmelazimishwa kuwa mashabiki wa 5imba.

Maana juzi mmetoka 5000 mpaka 3000,ila hamkujaza hata robo ya uwanja. Mechi ijayo na Wydad ukiwa na MoXtra na kipande cha sabuni unaingia uwanjani,maana hata nyinyi mshaichoka timu yenu.
Umekazania habari za kususia timu, Simba ina mashabiki wanaojitambua na ni kawaida kwa taasisi yoyote iliyo imara watu kutofautiana na wengine kuonyesha misimamo yao waziwazi. Hata mambele huko watu wanagoma kushinikiza mabadiliko. Hakuna jambo la kushangaza hapo.

Halafu haikusumbui kuandika "5imba" kila wakati? Hivi unadhani ukiandika hivyo kuna mtu anaumia?
 
Umekazania habari za kususia timu, Simba ina mashabiki wanaojitambua na ni kawaida kwa taasisi yoyote iliyo imara watu kutofautiana na wengine kuonyesha misimamo yao waziwazi. Hata mambele huko watu wanagoma kushinikiza mabadiliko. Hakuna jambo la kushangaza hapo.

Halafu haikusumbui kuandika "5imba" kila wakati? Hivi unadhani ukiandika hivyo kuna mtu anaumia?
Sasa kwani uwongo hamjasusa, hapo kwenye "5imba" simu yangu ikifikia hilo neno "s" hai-respond.

Taasisi imara huwaga haisusi bali washikadau wote hushikamana na kuwa pamoja, kinyume chake taasisi yenu sio imara.
 
Back
Top Bottom