Yanga imekata moto, Ijiandae kwa vipigo

Yanga imekata moto, Ijiandae kwa vipigo

Wazo zuri sana, it is said, to get to the top is easier than to stay at the top. Hivyo Yanga ijitafakari, mwenendo ni wa kusuasua, kikosi ni kipana wengine pia kina Shehani, Baleke, Nondo, Gift, Kibwana, Kibababage na Mkude pia wacheze maana hawajulikani sana uchezaji wao na hawatakamiwa. Kuchezesha wachezaji wale wale kila siku nao ni binadamu wanachoka na pia wanajisahau, kugombea namba husaidia kuboost morale!!

But ni vizuri pia kuona timu zikiikamia sana Yanga maana zinaiimarisha na kuwa timu ngumu zaidi kuifunga. Dawa ni Yanga kuvifunga kibabe hivi vitimu na kuwa imara kama chuma sababu makombe yote mali ya Yanga.

Huu ni wakati Yanga itangaze kwa wachezaji kuwa kila mechi mbele yao ni fainali na kombe liko uwanjani.

Mkakati wa kuchukua points 6 za Simba uanze sasa muda huu now now maana Azam si competitor tena hajiwezi. Points 6 za Simba ndo zimebeba ubingwa wetu wa nne maana Simba kila mechi inabebwa.
mmeanza kulia dawa yenu inakuja na timu yenu hiyo
 
Kwani Aucho hakuwahi kupewa kadi,tokea aanze kucheza mpira?
amewahi kupewa mfano kwenye ngao ya jamii na Simba na ukiangalia moment ya kmc kabla ya Aucho kufanya madhambi ilikuw ni hatari ila yule Mao angewafanya mbaya ,kiujumla ligi imeanza kuchanganya
 
amewahi kupewa mfano kwenye ngao ya jamii na Simba na ukiangalia moment ya kmc kabla ya Aucho kufanya madhambi ilikuw ni hatari ila yule Mao angewafanya mbaya ,kiujumla ligi imeanza kuchanganya
Hatari wewe mpira unaangalia vipi,timu hatari ili attempt mara ngapi, short on target ngapi,wamedominate kwa asilimia ngapi. Tukianza na hao KMC na nyie Kolo FC siku ya ngao maana na nyie mlifurahi kupigwa kkmoja.

Dk zote watu wanachezea half yao halafu uje kusema Aucho kazidiwa,mpaka Yanga ikaamua kucheza mastriker watatu, halafu unasema wamedominate. Mpira unatizama vip ww/ unaangalia vitu gani.

Mda wote Yanga wapo kwenye nusu yao KMC halafu unasema Mao alikiwa mkali.
 
Hatari wewe mpira ukiangalia vipi,timu hatari ili attempt mara ngapi, short on target ngapi,wamedominate kwa asilimia ngapi. Tukianza na hao KMC na nyie Kolo FC siku ya ngao maana na nyie mlifurahi kupigwa kkmoja.

Dk zote watu wanachezea half yao halafu uje kusema Aucho kazidiwa,mpaka Yanga ikaamua kucheza mastriker watatu, halafu unasema wamedominate. Mpira unatizama vip ww/ unaangalia vitu gani.

Mda wote Yanga wapo kwenye nusu yao KMC halafu unasema Mao alikiwa mkali.
kmc ali win kwa kias kikubwa kuwathibiti bahati mbaya ni kufungwa goli la mapema na kuhusu kmc kuzuia zaidi ni kumheshimu mpinzani kwa kuwa wako na ubora wao
 
Lete timu yako ndiyo utaelewa..........


Standard ya Yanga tangu last season ni 2+ goals,........hata tulipowapiga Simba moja kwenye ngao mlijisifu sana na kuona mmejitahidi sana,mkisahau kuwa mmefungwa.......tukampiga Azam 4,hofu yenu ikarudi.......Yanga ikianza kutoa vipigo mtaanza kusema GSM ananunua mechi,Saizi mikia mnashinda hatusikii ya Mangungo out au try again......tukiwapasua mnaanza kelele tena......... mbumbumbu dawa yenu inachemka
 
kmc ali win kwa kias kikubwa kuwathibiti bahati mbaya ni kufungwa goli la mapema na kuhusu kmc kuzuia zaidi ni kumheshimu mpinzani kwa kuwa wako na ubora wao
Waliwin kututhibiti kwa kucheza kwenye half yao, halafu unaema tulizidiwa, wewe timu inacheza na washambuliaji watatu,kiungo tunadominate halafu unasema Yanga walizidiwa. Sio KMC tu hata wewe ukikutana na Yanga,utapaki basi sababu huna uwezo wa kufunguka ukikutana na Yanga.
 
Waliwin kututhibiti, halafu unaema tulizidiwa, wewe timu inacheza na washambuliaji watatu,kiungo tunadominate halafu unasema Yanga walizidiwa. Sio KMC tu hata wewe ukikutana na Yanga,utabaki bus sababu huna uwezo wa kufunguka ukikutana na Yanga.
Yaan tupaki bas kwa ninyi vyura Fc mpira ni mkakati sio kucheza tu mnabahati sanaa ngao ya jamii mngelala na viatu
 
Yaan tupaki bas kwa ninyi vyura Fc mpira ni mkakati sio kucheza tu mnabahati sanaa ngao ya jamii mngelala na viatu
Kwani kwenye ngao mlifanyaje au umesahau na mkashangilia kupigwa moja. Sasa ww njoo halafu funguka ,wewe unazani kocha wenu mjinga kupaki basi siku ile ya ngao ya hisani.
 
Huu ndo ukweli ulio wazi. Ile circle ya mafanikio kwa Wananchi inaenda kutamatika msimu huu.

Timu haina mbinu mbadala, ukizuia zile pass mpenyezo basi hawawezi kupata bao.

Msimu huu tujiandae tu kwa vilio maana hata huko Klabu bingwa sidhani kama tutatoboa huko kwenye makundi...

Nipo tayari kuitwa mbumbumbu/kolo
Ogopa Yanga inayoongelewa imekatq moto

Simba anakuwa

Sadaka Yake
 
Kwani kwenye ngao mlifanyaje au umesahau na mkashangilia kupigwa moja. Sasa ww njoo halafu funguka ,wewe unazani kocha wenu mjinga kupaki basi siku ile ya ngao ya hisani.
game approach umekomaa kupaki bas ....na nyie fungukeni
 
Bongo kila mtu mcha-mbuzi,kwa mtu anayejua mpira hawezi kusema yanga imeshuka ubora bali ndo kawaida kimpira..huwezi ukashinda kila mechi magoli mengi!
 
Utani raha sana
FB_IMG_1727692311388.jpg
 
  • Kicheko
Reactions: Tui
Dada yangu wewe mweupe sana kwenye mpira sina cha kukujibu na sina mpango wa kureply comments zako nilisha kuambiaga.

Nauelewa mpira kuliko kitu chochote kile,miaka zaidi ya ishirini na fuatilia ligi zaidi ya nne, so hauna cha kuniambia kwenye mpira.Mimi sio oya oya.
Jibu hoja acha kujisifia upuuzi, aliyekuambia mimi siujui mpira nani kwani wewe unajua mimi nimeanza kufuatilia mpira lini, huwa mnaonesha mahaba ya wazi wazi kwa timu zenu kwa kisingizio eti mmeanza kufuatilia mpira zamani
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Siyo kwamba unalikwepa swali Jadda kiaina? Mi nakuomba mjibu halafu ndiyo umkaushie toka hapo.

Ova
Mkuu sijaelewa yani kwamba ubora wa timu ni kufunga magoli mengi au, maana kwenye hoja yake kaonesha kwamba ubora wa timu siyo kufunga magoli mengi, tofauti na wanavyosemaga mashabiki wa timu yake akiwemo yeye
 
Back
Top Bottom