Yanga ina tatizo la kocha, wachezaji au viongozi?

Yanga ina tatizo la kocha, wachezaji au viongozi?

Yanga 70% ya tatizo ni kocha, kocha ana miez 5+ ila timu haijulikan inacheza mfumo gan na ameshindwa ku improve wachezaji, beki mbovu, kipa matatizo ni yale yale, Tuisila tokea anafika alikuwa na tatizo la mipira ya mwisho mpaka leo bado ana udhaifu huo, kiufupi siyon kitu kocha alichokifanya.
Wachezaji wa timu kama Yanga hawapaswi wawe na kocha anaewafundisha namna ya kupora mpira, kupiga kona, kupiga penati, kukaba, au kugeuza nafasi kuwa bao. Kazi ya kocha ni kuifanya timu icheze kwa muunganiko na kutengeneza nafasi za kufunga mabao. Kaze hana lawama maana timu inatengeneza nafasi lakini wachezaji hawatumii nafasi kuwa magoli na hii sio kazi ya kocha. Kocha hafundishi namna ya kudaka mpira au kupiga penati kwa usahihi, kama kuna mchezaji hawezi kuyafanya hayo wa kulaumiwa ni yule aliyewasajili wachezaji wasioweza kupiga kona.

Yanga kila mtu anasajili, na wako waliosajiliwa bila ushauri wa makocha husika. Shida kubwa ya Yanga ni kiongozi kuwa na taaluma ya ukocha pia, hata Zahera alilalamikia hili, mwalimu anafundisha hivi na kiongozi anawafundisha vile.
 
Nimesikia kwenye sports arena M/kiti akitajwa kama mmoja ya watu wanaozinguana na wachezaji kwa kuwaita maduka.
 
Nimesikia kwenye sports arena M/kiti akitajwa kama mmoja ya watu wanaozinguana na wachezaji kwa kuwaita maduka.
Kuna dalili zote kuwa mwenyekiti ndie tatizo Yanga, maana haiwezekani ndani ya muda mfupi Zahera, Mkwasa, Emeyl, Zlaticovic na Kaze sasa wote wawe ndiyo tatizo kwa Yanga. Msola ndiye aliyeruhusu timu isajili wachezaji bila kuweko kwa kocha mkuu wa timu, Msolla ndiye aliyetoa kauli tata ya mashabiki kuchangia pesa za kusajili wachezaji, Msolla ndiye aliyemuondoa Mwambusi baada ya kombe la mapinduzi kitu kinachoonyesha kuwa timu ilikuwa iko vizuri, Msola ndiye aliyeruhusu GSM kusajili wachezaji bila ushauri wa kamati ya ufundi. Msolla ndiye aliyemtuhumu Metacha kuwa ameuza mechi akidai kuwa simu yake imedukuliwa na kutumika kumpigia Metacha, Msolla ni mafanyakazi wa mo (eti).

Msolla bila kuondoka Yanga ubingwa sahauni
 
Kuna dalili zote kuwa mwenyekiti ndie tatizo Yanga, maana haiwezekani ndani ya muda mfupi Zahera, Mkwasa, Emeyl, Zlaticovic na Kaze sasa wote wawe ndiyo tatizo kwa Yanga. Msola ndiye aliyeruhusu timu isajili wachezaji bila kuweko kwa kocha mkuu wa timu, Msolla ndiye aliyetoa kauli tata ya mashabiki kuchangia pesa za kusajili wachezaji, Msolla ndiye aliyemuondoa Mwambusi baada ya kombe la mapinduzi kitu kinachoonyesha kuwa timu ilikuwa iko vizuri, Msola ndiye aliyeruhusu GSM kusajili wachezaji bila ushauri wa kamati ya ufundi.

Msolla bila kuondoka Yanga ubingwa sahauni
Msolla anasema cm yake ilikuwa hacked. Aliyemwambia Mnata kuwa yeye ni duka sio yeye.😂😂😂
 
Msolla anasema cm yake ilikuwa hacked. Aliyemwambia Mnata kuwa yeye ni duka sio yeye.😂😂😂
Simu imedukuliwa kivipi? Lakini hakuna kizuizi cha metacha kuwa duka Yanga, maana kuna fungu kubwa limetengwa na timu fulani ili kufanikisha matokeo kwenye round ya pili wakati timu hiyo ikikabiliwa na mashindano mengi. Na hakuna namna yoyote fungu kama hilo lisifike kwa kwa makipa na mabeki muhimu wa timu lengwa. Habari ya timu fulani kutenga fungu la kazi hiyo ni dhahiri kwa mujibu wa mtoa habari wangu wa ndani kabisa wa timu hiyo. Tatizo ni fungu hilo limeshawafikia nani na nani yanga, wachezaji, viongozi, kocha au watu wa karibu na wachezaji?

Uonjgozi huu sio sahihi kwa Yanga inayotafuta ubingwa msimu huu.
 
Msolla anasema cm yake ilikuwa hacked. Aliyemwambia Mnata kuwa yeye ni duka sio yeye.😂😂😂
Je, Metacha haijui sauti ya Msolla? Ndani ya wiki mbili zimetolewa sababu tatu za Yanga kutofanya vizuri, kuhujumiwa na TFF, KOcha mbovu na Metacha kuwa duka. Lipi ni lipi? Uongozi ujitathimini bhana!!
 
Pale Yanga jini ananenepa wakati kiti anakonda. GSM hela zake zinakwenda moja kwa moja kwa wachezaji na mabadiliko na kuuacha uongozi ukipiga miayo, hii inawezakutoa mwanya kwa viongozi kushindwa kukataa pesa haramu kutoka kwa yeyote.
 
Back
Top Bottom