Yanga yajaribu kutumia njia za uani kuingia CAF Super League

Yanga yajaribu kutumia njia za uani kuingia CAF Super League

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Wakati timu zitakazoshiriki duru la kwanza la mashindano mapya ya CAF linajulikana, na zimechaguliwa kutokana na ubora wake wa miaka ya hivi karibuni, katika hali ya kushangaza, timu ya Yanga kupitia kwa serikali imewapigia magoti CAF kuomba ipewe nafasi pia ya kushiriki mashindano hayo.

20230406_205349.jpg


Wajuvi wa mambo tukishawahi kuonya kuwa wanasiasa wanaweza kutumika ili kushawishi au kushurutisha Yanga nayo ipewe nafasi katika mashindano hayo.

Ikumbukwe kuwa katika miaka 10 ya mashindano ya CAF CUP ambayo Simba walicheza hadi fainali mwaka 1993, Yanga hawakuwahi kuvuka hatua ya kwanza. Pia ni miaka 25 sasa imepita toka Yanga waingie hatua ya Robo fainali ya mashindano ya klabu bingwa Afrika wakati Simba wamefanya hivyo mara 3 ndani ya miaka hii 5 iliyopita.

Wanasiasa waache kuingilia masuala ya mpira. Hii ni moja ya sababu tunapata mikwamo kila siku katika mpira wetu.
 
Kuna vigezo vingine vinatumika ukiachana na ubora wa hivi karibuni. Na ndio maana Horoya na Tp Mazembe pamoja na kuonekana wameshuka viwango lakini ni miongoni mwa timu zilizopewa nafasi ya kushiriki super league
 
kwani vigezo vya kushiriki iyo super league ni vipi?
nataka vile vigezo ambavyo CAF wenyewe wameorodhesha sio vigezo vyenu sijui robo fainali,sijui nn...mtu mmoja mwenye akili timamu atupe source ambayo sisi tunaweza ingia humo kuangalia CAF wameweka vigezo gani vya kushiriki hili kombe
 
Wakati timu zitakazoshiriki duru la kwanza la mashindano mapya ya CAF linajulikana, na zimechaguliwa kutokana na ubora wake wa miaka ya hivi karibuni, katika hali ya kushangaza, timu ya Yanga kupitia kwa serikali imewapigia magoti CAF kuomba ipewe nafasi pia ya kushiriki mashindano hayo.

View attachment 2578806

Wajuvi wa mambo tukishawahi kuonya kuwa wanasiasa wanaweza kutumika ili kushawishi au kushurutisha Yanga nayo ipewe nafasi katika mashindano hayo.

Ikumbukwe kuwa katika miaka 10 ya mashindano ya CAF CUP ambayo Simba walicheza hadi fainali mwaka 1993, Yanga hawakuwahi kuvuka hatua ya kwanza. Pia ni miaka 25 sasa imepita toka Yanga waingie hatua ya Robo fainali ya mashindano ya klabu bingwa Afrika wakati Simba wamefanya hivyo mara 3 ndani ya miaka hii 5 iliyopita.

Wanasiasa waache kuingilia masuala ya mpira. Hii ni moja ya sababu tunapata mikwamo kila siku katika mpira wetu.
Je kwenye Mpira tunaangalia current performance au past performances?na kipi Bora Kati ya hivyo
 
Yanga atacheza hiyo SL

Jiandae kisaikolojia
Mpaka kamati kuu ya CCM ikae ipange hizo timu.

Itakaa ktk mkutano wake wa robo mwaka mwishoni mwa April 2023.

Itatoa maagizo kwa halmashauri kuu ya chama kuangalia upya mchakato ili timu pendwa na bora kuliko zote Afrika iweze kushiriki CAFSL
 
Back
Top Bottom