Yanga yakubali kichapo cha kwanza Ligi Kuu Tanzania Bara

Yanga yakubali kichapo cha kwanza Ligi Kuu Tanzania Bara

Yanga Raha
Screenshot_2021-03-04-23-21-06.jpeg
 
Masikini Yanga...walishaanza kunenepa wenyewe dah! maisha hayana fair kabisa.
 
Huu ndo ubaya wa kuwa unbeaten, yani kila timu inasaka nafasi ya kubunja hiyo rekodi, ndiyo maana tunakutana na ugumu mwingi sanaaa, nadhani wachezaj hawajapewa hii elimu ya ugumu tunaoupata[emoji38]
Hamna wachezaji Talented
 
Baada ya mzunguko wa kwanza Yanga kuifunga Coastal union bao 3-0, leo Coastal Union wamesema wanachezea heshima kwa uwanja wake wa nyumbani na kocha Mgunda amejigamba atakuwa wa kwanza kuifunga Yanga msimu huu.

Yanga inahitaji matokeo kuendelea kujiweka vizuri kileleni lakini uwanja wa Mkwakwani umekuwa haumpi matokeo ya uhakika kwenye misimu ya karibuni.

Kuwa nami kukujuza yatakayojiri uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

=======

Mechi zilizochezwa mapema leo

FT' Polisi Tanzania 1-0 KMC | Sheikh Amri Abeid

FT' Mtibwa Sugar 0-0 Biashara UTD | Jamhuri

FT' Tanzania Prisons 1-1 Mbeya City FC

=======

00' Mwamuzi anapuliza kipenga kuashiria mwanzo wa mcho na Coastal wanaanza kusukuma guzi

06' Yanga inapata penati baada ya Kipemba wa Coastal kumuweka chini mchezaji wa Yanga

08' Tuisila Kisinda anashindwa kufunga penati, mlinda mlango wa Coastal anasimama imara na kuidaka penalt.

10' Coastal wanaweka bao la kwanza baada ya Erick Msagati kupiga shuti mpira uliokuwa unaamba goli la Yanga ulioanzia mpira wa adhabu ndogo

19' Feisal Salum anajaribu shuti la kushtukiza lakini mlinda mlango wa Coastal alikuwa yuko makini na kuuondoa kwenye hatari

32' Yaqub anaingia kuchukua nafasi ya Sarpong kwa upande wa Yanga

37' Tuisila Kisinda anasawazisha, Coastal Union 1-1 Yanga

40' Farid Mussa anashindwa kuongeza bao la pili kwa Yanga baada ya kubaki na mlinda mlango

45' Mpira unaenda mapumziko

46' Mpira umesharejea kutoka mapumziko, Coastal 1-1 Yanga

53' Deus Kaseke anajaribu kupiga shuti lakini mpira unapaa juu ya lango la Coastal Union

64' Mfungaji wa Goli la Coastal, Erick Msagati anakwenda bench na nafasi yake kuchukuliwa na Issa Abusheikh

72' Omari Majimengi najaribu kuitanguliza Coastal kwa mkwaju mkali lakini mlinda mlango wa Yanga anasimama imara

83' Mudathir Abdallah anaweka goli la pili kwa shuti kali lililopita na wavu na kuipa uongozi Coastal Union

90' Dakika tano zinaongezwa kumaliza mtanange

90+5' Coastal Union inatamba uwanja wake wa nyumbani kwa kuichapa Yanga magoli 2-1.

Yanga inashindwa kutamba uwanja wa Mkwakwani dhidi ya Coastal union kwa mwaka wa sita mfululizo na inapoteza mechi yake ya kwanza ligi kuu Bara, majaliwa ya Yanga kubaki kileleni ni kuchacha kwa viporo vya Simba
majaliwa ya Yanga kubaki kileleni ni kuchacha kwa viporo vya Simba...[emoji196][emoji196][emoji196]HAVICHACHI NG'O...!!!![emoji196][emoji196][emoji196]
 
majaliwa ya Yanga kubaki kileleni ni kuchacha kwa viporo vya Simba...[emoji196][emoji196][emoji196]HAVICHACHI NG'O...!!!![emoji196][emoji196][emoji196]
Hawezi tena,utepe umeshakatwa njia nyeupee,watu watakuwa wanajipigia tu iko nje nje kama ya mbuzi vile
 
MVUA IMENYESHA SASA NI MUDA WA KUTAFUTA MATOBO YANAYOVUJA

Anaandika @exaud_msaka_hqbari

Kufungwa Yanga ilikuwa ni swala la kusubiri, yani ni kama kumuona Tembo juu ya mti ni kusubiri maana ataanguka tu

Ilikuwa inashangaza mpira wanaocheza Yanga kwa mechi za karibuni alafu unaambiwa hawajapoteza mchezo.

Mechi Tano za nyuma zilikuwa zinaonesha kabisa kuwa Yanga anafungwa Siku yoyote na wao walikuwa wanajua hilo

Yanga shukuruni Mungu mmefungwa sasa ili mjue shida iko wapi, maana ushindi na sare vilikuwa vinawafanya mdhani kikosi chenu hakina mapungufu

Yanga haina shida ya kocha ina shida ya wachezaji, wachezaji wao ndio wale ile ndio kiwango chao kabisa wala wasilaumiwe

Kama watamtimua Kaze watakuwa wanamuonea tu ila hana uwezo wa kubadilisha aina ile ya wachezaji, hana uwezo wa kumfanya Farid akapata goli kama lile alilokosa pale

Ubingwa wa Tanzania ni Mchakato sana na unahitaji kusubiri na kujipanga, sio kuamka na kuahidi tusipochukua mtuulize

Sasa Yanga wakae chini kistarabu waulizane tuna shida gani na tunaifanyaje, maana sasa Marefa na TFF hawahusikiView attachment 1717307
.
 
Mi nahisi Yanga ndio haina hadhi ya kuwa na supoko

Kwasababu ukianza kuangalia utaweza kujiuliza kipi kilichowafanya ken gold waombe mechi na yanga na sio simba?

Ken gold waliona yanga ndio timu ambayo wana wiana uwezo na ni kweli na ndio maana hata gemu ken gold alicheza vizuri kumzidi yanga japo walibustiwa na kile ki penalty

Na ndio maana hata baada ya ushindi huo 99% mashabiki wa yanga hawakuufurahia huo ushindi
Awakuomba ilikua mechi ya FA ovyo ovyo wangetolwa kwa mpira ule ilikua ni mechi muhimu kabisa
 
Hawa jamaa wanalo, ni mpaka wachomoe huko mwiko nyuma.....😂😂.

Yanga ....Daima mbele.... Nyuma Mwiko😂
 

Attachments

  • IMG-20210228-WA0001.jpg
    IMG-20210228-WA0001.jpg
    28.7 KB · Views: 1
  • Screenshot_20210305-165905_Instagram.jpg
    Screenshot_20210305-165905_Instagram.jpg
    118.3 KB · Views: 1
Back
Top Bottom