Baada ya mzunguko wa kwanza Yanga kuifunga Coastal union bao 3-0, leo Coastal Union wamesema wanachezea heshima kwa uwanja wake wa nyumbani na kocha Mgunda amejigamba atakuwa wa kwanza kuifunga Yanga msimu huu.
Yanga inahitaji matokeo kuendelea kujiweka vizuri kileleni lakini uwanja wa Mkwakwani umekuwa haumpi matokeo ya uhakika kwenye misimu ya karibuni.
Kuwa nami kukujuza yatakayojiri uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
=======
Mechi zilizochezwa mapema leo
FT' Polisi Tanzania 1-0 KMC | Sheikh Amri Abeid
FT' Mtibwa Sugar 0-0 Biashara UTD | Jamhuri
FT' Tanzania Prisons 1-1 Mbeya City FC
=======
00' Mwamuzi anapuliza kipenga kuashiria mwanzo wa mcho na Coastal wanaanza kusukuma guzi
06' Yanga inapata penati baada ya Kipemba wa Coastal kumuweka chini mchezaji wa Yanga
08' Tuisila Kisinda anashindwa kufunga penati, mlinda mlango wa Coastal anasimama imara na kuidaka penalt.
10' Coastal wanaweka bao la kwanza baada ya Erick Msagati kupiga shuti mpira uliokuwa unaamba goli la Yanga ulioanzia mpira wa adhabu ndogo
19' Feisal Salum anajaribu shuti la kushtukiza lakini mlinda mlango wa Coastal alikuwa yuko makini na kuuondoa kwenye hatari
32' Yaqub anaingia kuchukua nafasi ya Sarpong kwa upande wa Yanga
37' Tuisila Kisinda anasawazisha, Coastal Union 1-1 Yanga
40' Farid Mussa anashindwa kuongeza bao la pili kwa Yanga baada ya kubaki na mlinda mlango
45' Mpira unaenda mapumziko
46' Mpira umesharejea kutoka mapumziko, Coastal 1-1 Yanga
53' Deus Kaseke anajaribu kupiga shuti lakini mpira unapaa juu ya lango la Coastal Union
64' Mfungaji wa Goli la Coastal, Erick Msagati anakwenda bench na nafasi yake kuchukuliwa na Issa Abusheikh
72' Omari Majimengi najaribu kuitanguliza Coastal kwa mkwaju mkali lakini mlinda mlango wa Yanga anasimama imara
83' Mudathir Abdallah anaweka goli la pili kwa shuti kali lililopita na wavu na kuipa uongozi Coastal Union
90' Dakika tano zinaongezwa kumaliza mtanange
90+5' Coastal Union inatamba uwanja wake wa nyumbani kwa kuichapa Yanga magoli 2-1.
Yanga inashindwa kutamba uwanja wa Mkwakwani dhidi ya Coastal union kwa mwaka wa sita mfululizo na inapoteza mechi yake ya kwanza ligi kuu Bara, majaliwa ya Yanga kubaki kileleni ni kuchacha kwa viporo vya Simba