Yesu akirudi leo atasali wapi? Kwa Wayahudi, RC /Wasabato au Kwa Walokole? Au Mashahidi wa Yehova? Naomba majibu

Yesu akirudi leo atasali wapi? Kwa Wayahudi, RC /Wasabato au Kwa Walokole? Au Mashahidi wa Yehova? Naomba majibu

Kuna baadhi ya vitu hutakiwi kupinga kwa kuwa ni mfuasi wa dhehebu fulani,,,,!!!

Ukweli unabaki palepale kwamba Issa (a.s) was not christian and he will not be christian ever as you claim,,,!!!
maana christian ni mfuasi wa kristo, sasa kristo atakuaje mkristo wakati yeye mwenyewe ndio kristo
 
Aje kutokea wapi wakati hakuna kiumbe kinaitwa Yesu wala mahali panaitwa Mbinguni
 
Wewe unaumwa nini? Mungu asali kumuomba nani? Mudi ndio anatakiwa asali
Nyie ndio wakristo mnaoendeshwa. Inaonesha hata biblia yenyewe huijui na wala hutaki kuijua. Yesu ni Mwanadamu na alikuwa ni mtume wa Mungu (aliyetumwa na Mungu) kuja kuwaelekeza wanadamu hasa Wayahudi juu ya mwenendo aupendao Mungu mmoja muumba wa kila kitu.

Kuhusu Yesu kuabudu na Kumuomba Mungu Soma Waebrania 5:7 utaona Jinsi Yesu alipokuwa akisali na kulia akimuomba Mungu Amnusuru. Na ktk hilo, kuna mafundisho makubwa kuwa, kwa jambo lolote, mgeukie Mungu na umuamudu na kumuomba yeye tu. Hicho ni kifungu kimoja kati ya vingi sana ambapo yesu anasali na kumuomba Mungu.

Rejea kipindi anakamatwa kupelekwa kwa Pilato aliomba kwenye jiwe ili adhabu ile Mungu amnusuru. Pia siku 40 alifunga na kusali, unajua alimuomba nani kama yeye ndiye Mungu na anayestahili kuombwa? Pia wakati yuko msalabani ( kwa mujibu wa biblia yako) aliomba kwa kusema " ee baba wasamehe hawa kwa maana hawajui watendalo." Pia aendelea kusema "baba mikononi mwako nakabidhi roho yangu". Je huyo baba aliyekusudiwa hapa unadhani ni Mzee wako Mashishanga? Ndio ndiye Mungu ambaye alimtuma Yesu akupe wewe mafundisho ya kumjua yeye na kumuabudu yeye pekee.

Jamaa na wengine wote wenye mawazo kama yako, nawasihi sn epukaneni na hayo mawazo ya kuwa yesu ni mungu, Yupo Mungu aliyemuumba na kumtuma huyo Yesu duniani. Mkiri Mungu mmoja na umuabudu kabla hujafa. Kumpa uungu Yesu na kumpokonya Mungu halisi Muumba ambaye huyo yesu mwenyewe anamtambua ni kujitoa ufahamu na kujiangamiza mwenyewe.
 
Lakini walimlalamikia hashiki sabato akawaambia Sabato iliumbwa kwa ajili ya mwanadamu na Siyo mwanadamu kwa ajili ya Sabato
Luka 4:16
Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi kama ilivyokuwa desturi yake.

Alikuwa anaingia ndani ya masinagogi kufanya ibada Kwa kufuata maagizo ya Mungu na Wala sio ya binadamu
Kama Kuna watu walikuwa wanampinga hakumfanyi yeye kuacha kuingia ndani ya masinagogi maana hakuingia humo Kwa amri ya binadamu Bali Kwa amri ya Mungu

Yesu alianza kuhuburi Injili akiwa na miaka 30 na alihubiri Kwa muda wa miaka 3 kabla haja paa hivyo basi kuanzia miaka 30 kurudi nyuma Desturi yake ilikuwa kufanya ibada ndani ya masinagogi
 
Nawasalimu wote.

Kumekuwepo na mjadala kuhusu ipi dini ya Kweli, huu ni mjadala wa siku nyingine. Leo nataka tumuongelee YESU KRISTU.

Wakati akiwa hapa duniani, Yesu alionekana hekaluni akihubiri injili, Wayahudi hawakupendezwa sana wakisema anakufuru na kupelekea kumsulubisha msalabani.

Baada ya kifo na ufufuo wake (Kama ilivyoandikwa) ndipo lilianza vuguvugu la kanisa la kwanza!

Ukiwauliza RC watakwambia, Papa wa Kwanza ni Mt Petro na alikuwa mwanafunzi wa Yesu. Ukiwauliza Walokole nao watakwambia wao ndio wapo sahihi, Vivyo Hivyo kwa Wasabato au Mashahidi wa Yehova!

Kama biblia inayotumika ni moja inakuwaje kuna mgongano huu mkubwa?

Je, ni kitu gani hawatuambii?
Kwa bahati mbaya nasikitika kusema swali lako halina mantiki, Wala hali sound..
Hakuna mahali popote kwa Neno la Mungu pameandikwa kuhusu unabii wa Mwana kuja tena Duniani na kuanza kusali sijui wapi... according to the word of God, when comes ndiyo mwisho wa Dunia.
 
Nawasalimu wote.

Kumekuwepo na mjadala kuhusu ipi dini ya Kweli, huu ni mjadala wa siku nyingine. Leo nataka tumuongelee YESU KRISTU.

Wakati akiwa hapa duniani, Yesu alionekana hekaluni akihubiri injili, Wayahudi hawakupendezwa sana wakisema anakufuru na kupelekea kumsulubisha msalabani.

Baada ya kifo na ufufuo wake (Kama ilivyoandikwa) ndipo lilianza vuguvugu la kanisa la kwanza!

Ukiwauliza RC watakwambia, Papa wa Kwanza ni Mt Petro na alikuwa mwanafunzi wa Yesu. Ukiwauliza Walokole nao watakwambia wao ndio wapo sahihi, Vivyo Hivyo kwa Wasabato au Mashahidi wa Yehova!

Kama biblia inayotumika ni moja inakuwaje kuna mgongano huu mkubwa?

Je, ni kitu gani hawatuambii?
Hili swali walisha lijibu Mzee wa upako na Chalamila hata kabla hawajaulizwa na mtu
 
Back
Top Bottom