Yesu Kristo aliuawa kwa sababu za kisiasa zaidi kuliko za kidini

Mkuu umeeleweka sana...Kifo chake kilikuwa cha kisiasa zaidi...aliponena habari za ukombozi watu walielewa ni ukombozi wa kisiasa kutoka kwa dola la kirumi.Ndio maana alipata wafuasi wengi kenye mikutano yake, watu walimchukulia kama vile kina Nyerere na Mandela walivyowaahidi waafrika uhuru kutoka kwa wakoloni.Ndio maana baada ya kukamatwa na kuteswa kwake, watu wengi walimzomea na kumcheka kwa kushindwa kwenye harakati za kupata uhuru kutoka kwa waroma.

Kama kifo chake kingekuwa cha kidini basi Israel ingekuwa na wakristo wengi zaidi.Kwa ule wingi wa watu waliomfuta kwenye mikutano yake, wangeendeleza dini ya ukristo huko Israel na matokeo yake Israel ingekuwa na wakristo wengi sana.Lakini haipo hivyo kwani Israel wanafuata dini ya kiyaudi na kuna wengine hata Yesu hawamjui zaid ya kumsikia tu.

Baada ya Yesu kufa, hakuonekana hadharani baada ya kufufuka lakini wanafunzi wake walidai kwamba amefufuka na wamemuona.Wale waliomfuata kwenye mikutano wakajiuliza, kama alifia hadharani, kwanini asingejionesha hadharani baada ya kufufuka? wakagoma kuamini.Watu wakahoji je uko wapi ukombozi aliotuahidi? wanafunzi wakajibu kwamba ukombozi ulikuwa wa kiroho na sii wa kisiasa.

Wanafunzi wake walipoanza kuhubiri habari za kufufuka kwa Yesu, walikamatwa na kuteswa kwa sababu waliashiria mapinduzi ya kiutawala na kwa hasira za kukosa ukombozi wakati wa Yesu.
 
Safi sana ndugu... inaonekana ni kweli Yesu aliuliwa kwasababu za kisiasa zaidi,kuliko kidini kama tulivyolishwa tango pori... kwasababu hata mie hua najiulizaga iweje israel iwe na wakristo wachache zaidii kuliko Mbeya?
 
Safi sana ndugu... inaonekana ni kweli Yesu aliuliwa kwasababu za kisiasa zaidi,kuliko kidini kama tulivyolishwa tango pori... kwasababu hata mie hua najiulizaga iweje israel iwe na wakristo wachache zaidii kuliko Mbeya?
Jibu ni rahisi sana, Israeli wanahoji kitu kwanza kabla ya kukipokea,...wale ni wasomi/wanasayansi so anything without proof does not appeal to them....Ila wabongo wanafuata sana vitu bila kuuliza na kutafakari, hasa kitu kikiwa cha mzungu mbongo atakiona kama kitu kamili kilichojitosheleza kisicho hitaji kuhoji.

Mfano, madhehebu ya kikrosto kama Anglikana, Katoliki na Lutheran yanaheshimiwa na kufuatwa na wengi sababu yalianzishwa na wazungu.Lakini yale ya wabongo kama makanisa ya Lusekelo na Mama Lwakatare yanadharaulika sana na kufuatwa na wachache.Ni rahisi kusikia kanisa la Lwakatare au Lusekelo ya kiitwa ya freemason kuliko kusikia Lutherani au Anglikana wanaitwa hivyo.Hii ni kwa sababu wazungu waliwaaminisha wabongo kwamba kila kinachotoka Africa(KAMA MILA ZA KIAFRIKA) ni cha Shetani na kwamba Mungu anawatumia wao kueleza jinsi gani ya kutekeleza sheria zake.
 
Target nikufika arusha lakini tutafikaje lazima kuwe na sababu.

Lengo kuu ilikuwa ni Yesu asulubiwe .

Vijisababu vitakuwa vingi. Tamaa, uchu wa madaraka nk lakini lengo limetimia tumepata wokovu.

Hakuna mistake kubwa ambayo shetani amewai kuifanya kama kuruusu yesu asulubiwe.


Hiyoo ni strength inatufanya wakristo kudunda.
 
Umeongea vyema
 
Me swali langu je uyahudi ni dini au kabila?
Na pia yesu aliuliwa na wayahudi,waisrael au warumi?
Nini tofauti ya jews na israel?
 
3. Yesu hakumwaga pesa ya sadaka hekaluni. Alimwaga pesa na bidhaa za wafanyabiashara. kifupi, wajasiriamali walikuwa wamegeuza hekalu kuwa Kariakoo au Tandale. Walikuwa wanafugia hadi mifugo humo kama unavyoona wafuga kuku pale soko la Kisutu (hivi lile soko bado lipo?) na Shekilango.
 
Me swali langu je uyahudi ni dini au kabila?
Na pia yesu aliuliwa na wayahudi,waisrael au warumi?
Nini tofauti ya jews na israel?
Nitaongelea kipengele kimoja cha wayahudi na waisrael kwa sasa.
katika historia ya makabila yale kumi na mbili (au kumi na tatu) maana kabila la Yusufu liliwakilishwa na wanae wawili, Manase na Efraim, yaligawanyika na kuunda falme mbili. Ufalme wa kusini uliitwa Yudea (Judah) na uliundwa na makabila mawili: Kabila la Yuda na kabila la Benjamin. Nadhani hawa ndio Jews (I stand to be 'collected', sorry..to be corrected).

Makabila mengine kama Asheri, Dani, Gadi, Naftali, Zebuloni, Simeoni, Rubeni, Isakari, Efraimu na Manase yaliunda Ufalme wa Kaskazini ulioitwa Waisrael (Israelites). Inasemekana kabila la Lewi (Walawi) halikuwa na makao maalum, lilisambaa kote kote miongoni mwa makabile yale mengine hivyo halikuwa na mji wake.

Hayo makabila yaliyounda ufalme wa kaskazini ndiyo yalishambuliwa na mnamo karne kama ya nane BC na kuangushwa na watu wote kuchukuliwa mateka na baadaye kuwa integrated kwenye miji mingine ya ufalme wa Ashuru (Assyria) 2Wafalme 17. Hayo ndiyo makabila ya Israel ambayo inasemekana yamepotea maana hawakurudi tena kwenye nchi yao. Kwa maana hiyo, hata wale ambao walikumbana na panga la Hitler, walikuwa wayuda/Jews/Judah people maana wale wengine hawakupata kusikika tena. Nasikia siku hizi kuna juhudi za kutafuta The Lost Tribes of Israel, sijui kama zitafanikiwa.
 
Kwa uelewa wako na huyu Herode tunamsikia na kumsoma yeye alikuwa nani katika utawala wa kirumi, na jeeh alihusika vipi katika hukumu ya Yesu Kristo King Octavian
 
It is true. Wala haikuwa kitu cha kusema ilitabiriwa au ilikuwa ni tukio la ajabu. Kusulubishwa ilikuwa kawaida kwa walioonekana wanapinga ukoloni wa kirumi katika Israel.

Pia warumi hawakuamini alikufa. Hata watu waliposema alifufuka na kuonekana katika baadhi ya miji watu ilijulikana kuwa alisaidiwa kupona kile kifo na watu wachache ambao walipanga hiyo plan. Akiwemo Joseph mwenye tomb na mke wa Pilato na baadhi ya mitume na sio wote. Tatizo waliokuja na kusambaza imani waliyoiita imani mpya ndio wakaja na lies ambazo hawakujua facts zake na kusahau siasa iliyokuwa inaendelea na kuchochea sababu za kidini.
 
Si unajua ya kuwa kuna imani sahihi na isiyo sahihi.Katika imani hizi moja ya kweli na nyingine ni kinyume chake.

Sasa ni vyema kama una imani ya kweli umsaidie yule mwenye imani potofu.Huo ndio uninadamu au una wasi wasi na imani yako nini?
Unajua kuna watu wamekua na imani zao hata uwaambie nini hawakulewi, mfano mtu anaabudu ng'ombe na anaamini ni mungu wake
Ni Kazi sana mpaka abadilike
 
Ni kweli kabisa, Wa kristo tutaendelea kudunda sana tena sana tu. Lengo la Yesu ilikua kumkomboa mwanadamu kutoka ktk utumwa Wa shetani.
Hallelujah!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…