Yesu Kristo aliuawa kwa sababu za kisiasa zaidi kuliko za kidini

Yesu Kristo aliuawa kwa sababu za kisiasa zaidi kuliko za kidini

Mkuu umeeleweka sana...Kifo chake kilikuwa cha kisiasa zaidi...aliponena habari za ukombozi watu walielewa ni ukombozi wa kisiasa kutoka kwa dola la kirumi.Ndio maana alipata wafuasi wengi kenye mikutano yake, watu walimchukulia kama vile kina Nyerere na Mandela walivyowaahidi waafrika uhuru kutoka kwa wakoloni.Ndio maana baada ya kukamatwa na kuteswa kwake, watu wengi walimzomea na kumcheka kwa kushindwa kwenye harakati za kupata uhuru kutoka kwa waroma.

Kama kifo chake kingekuwa cha kidini basi Israel ingekuwa na wakristo wengi zaidi.Kwa ule wingi wa watu waliomfuta kwenye mikutano yake, wangeendeleza dini ya ukristo huko Israel na matokeo yake Israel ingekuwa na wakristo wengi sana.Lakini haipo hivyo kwani Israel wanafuata dini ya kiyaudi na kuna wengine hata Yesu hawamjui zaid ya kumsikia tu.

Baada ya Yesu kufa, hakuonekana hadharani baada ya kufufuka lakini wanafunzi wake walidai kwamba amefufuka na wamemuona.Wale waliomfuata kwenye mikutano wakajiuliza, kama alifia hadharani, kwanini asingejionesha hadharani baada ya kufufuka? wakagoma kuamini.Watu wakahoji je uko wapi ukombozi aliotuahidi? wanafunzi wakajibu kwamba ukombozi ulikuwa wa kiroho na sii wa kisiasa.

Wanafunzi wake walipoanza kuhubiri habari za kufufuka kwa Yesu, walikamatwa na kuteswa kwa sababu waliashiria mapinduzi ya kiutawala na kwa hasira za kukosa ukombozi wakati wa Yesu.
Watu mko vizuri bwana kwenye kutetea hoja... asante mkuu.
 
King Octavian

Dini ni siasa ya zamani, siasa ni dini ya mbeleni.

Siasa na dini ni pande mbili za sarafu moja.

Ukiona siasa na dini ni vitu tofauti utapata maswali yasiyo msingi.

ukijua siasa ni dini na dini ni siasa wala huwezi kujiuliza kwamba Yesu aliuawa kwa sababu za dini au siasa.

Siasa ni dini.

Ndiyo maana mkuu wa Wakatoliki ni Mkuu wa nchi ya Vatican.

Ndiyo maana ISIS wanapigania caliphate.
 
King Octavian

Dini ni siasa ya zamani, siasa ni dini ya mbeleni.

Siasa na dini ni pande mbili za sarafu moja.

Ukiona siasa na dini ni vitu tofauti utapata maswali yasiyo msingi.

ukijua siasa ni dini na dini ni siasa wala huwezi kujiuliza kwamba Yesu aliuawa kwa sababu za dini au siasa.

Siasa ni dini.

Ndiyo maana mkuu wa Wakatoliki ni Mkuu wa nchi ya Vatican.

Ndiyo maana ISIS wanapigania caliphate.
Kiranga, nilikua najiuliza upo wapi kiongozi, kumbe tupo pamoja, nashukuru kwa hili, Kwa hiyo kwa tafsir ya haraka haraka ya kiimani Siasa na dhambi ni kitu kimoja?
 
Kilicho muua Yesu ni dhambi zetu sisi wanadamu, hapo zamani mfumo wa kusamehe dhami ilikuwa wa kuchinja mnyama aliyenona ili upate msamaha wa dhambi, ila tatizo ni kwamba damu ya mnyama inazifunika tu, ili Mungu asizione.
Kwa hiyo kwa damu ya Yesu dhambi zetu zinasafishwa kama zilikuwa nyekundu kama damu zitakuwa nyeupe kama barafu (dheruji).

Na kuhusu Israel kuwa na wa kristo wachache sababu ni moja tu, ili u nabii utimie, kwamba "Nabii hakubariki nyumbani kwao"
Maana yake, Ukiwa Mkristo tu hutokuwa na dhambi tena hata ukizini au kulewa au kuuwa??..ila pia, siye Huyu Yesu alisema kila mtu atabeba furushi lake mwenyewe? na pia kutakuwa na hukumu kutokana na matendo yetu?. Npata kizunguzungu kila nikifkiria dhana ya sisi kukombolowa na kifo cha yesu na kauli zake Yesu kuwa tutabeba mafurushi yetu wenyewe
 
Ok!ninavyojua mimi,Yesu aliuawa c kwasababu ya kisiasa wala kidini bali KUTIMIZA KUSUDI LA MUNGU ambalo ni kumwokoa mwanadam na dhambi kwa hyo yote hayo yaliyotendka ni njia ya kutimiza ANIKO TAKATIFU.
huko kuokolewa na dhambi kukoje? Maana si Mwislam, si Mkristo.... wote wanafanya madhambi mpaka sasa...vipi huko kuokolewa? Pia Yesu mwenyewe anasema tutahukumiwa kutokana na matendo yetu....tumeokolewaje sasa kwa kifo chake? Na wale waliofanya madhambi kabla Yesu hajaja kuokoa na tukamfuata tukawa Wakristo, wale wataokolewaje sasa au kifo cha Yesu hakimuhusu? Maana walikuwa hawamjui na hawakuwa wakristo kama sisi leo
 
Hii nilishawahi kusikia zaidi nikasema nitapata wapi vitabu au nakala za mambo haya ya kale.
Kitu kimoja,mambo yanayotokea siku hizi za leo hayatofautiani sana na mambo ya miaka 2000 iliyopita.
Its the same human being we talking about.
Dah! Nakusoma Sana mkuu
 
Kiranga, nilikua najiuliza upo wapi kiongozi, kumbe tupo pamoja, nashukuru kwa hili, Kwa hiyo kwa tafsir ya haraka haraka ya kiimani Siasa na dhambi ni kitu kimoja?
Unaipataje tafsiri hiyo?

Siasa si kitu kibaya (kama tafsiri yako ya "dhambi" ni kitu kibaya). Kinacholeta ubaya katika siasa ni complexity ya maisha ya leo.

Huko zamani jamii ilikuwa haina complexity na watu waliweza kufanya siasa za maana, wadogo waliheshimu wakubwa, wakubwa walijiheshimu.

Kadiri siku zinavyoendelea, kwa kufuata "The Second Law of thermodynamics", mambo yana move kutoka kuwa simple na kuwa complex, uongozi unageuka uongo, siasa inageuka si hasa.

Kuna watu wanaona siasa yote mbaya. Si kweli. Ni mambo ya nyakati zetu hayo.

Kuna siasa nzuri bado. Waziri Mkuu wa Uingereza kashindwa kuongoza, kajiuzulu Uwaziri Mkuu na sasa anajiuzulu ubunge. Hakuna mtu aliyeuawa wala kupinduliwa wala kung'ang'ania madaraka.
 
Mkuu hapo umeandika pumba tupu..is better kama hujui bible ukakaa kimya...unatakiwa usome agano la kale vizur ndo utaelewa agano jipya..hapo utajua kuwa Yesu alikufa kwa sababu za kidini na siasa ilikuwa kama passing code...na hata Leo machafuko yote ya kisiasa yanaongozwa na mapambano ya kidini kat ya Yesu na Shetani ila
siasa ndo battle ground
wafia dini utawajua tu
 
Somo zuri asante kwakuniongezea maharifa Leo kichwani mwangu
Ila majibu ya yesu kwann yalikuwa sio ya Moja kwa Moja?
Yaani ukimuuliza swali anakujibu kwa swali!!!!
Mfano kwenye kutoa ushuru,
Katika hili la kujibu swali kwa swali inaonyesha watawala wa kipind kile walikuwa wavumulivu kias flan. maana alikuwa anakera mno hasa kwa kiongoz wa juu vile. Ndo maana alikufa akiwa kijana labda. Ambacho sielew ni ilikuwaje wafuasi wa Yesu wakaongezeka dunia nzima kirahis ilihali warumi kwa mamlaka yao wangeweza kuidhibiti hali ya uasi? Au masuala ya unaabuduje hayakuwa na uzito kama hayaathiri ukusanyaj kodi na utiifu kwa huyo mkoloni!
 
Mtoa mada asante sana kwa kuwa objective...jambo ambalo ni gumu sana kwa wafia dini...naomba nipendekeze kwa wale wanaopenda kujua habari hizi kihistoria zaidi.....

Ingia you tube...seach...misquoting jesus by Bart Ehrman. Sikiliza lecture yake....na nyingine nyingi...hakika hautotoka bure!

Angalizo: this is historical approach...so be open minded.
 
Si lengo wala dhamira yangu kupinga wala kupindisha Imani ya mtu yeyote, bali ni wajibu wangu kama binadamu mwenye akili na upeo wa kudadisi, kuchanganua na kuyaelewa mambo mbalimbali katika namna tofauti tofauti.

Biblia ni kitabu kama vilivyo vitabu vingine vyenye maarifa, tamaduni na vinavyoelezea hisia za jamii za watu wake, isipokua Biblia ni kitabu maarufu kuliko kitabu chochote kilichowahi kuandikwa katika taaluma ya uandishi hapa Duniani.

Uchambuzi wangu utajikita zaidi katika kuelezea kifo cha Yesu Kristo ambaye historia kupitia vitabu mbalimbali vinavyounda kitabu kikuu cha biblia inatueleza kuwa ndiye chanzo cha Dini ya kikisto au kwa lugha ya kigeni dini hiyo inajulikana kama CHRISTIAN yenye tafsiri ya Wafuasi wa Yesu Kristo.

Historia kutoka katika vitabu vya MATHAYO na LUKA inatuambia kua Yesu Kristo alikua MYAHUDI na alizaliwa sehemu ijulikanayo kama BETHLEHEM katika jimbo la JUDEA. Wakati huo sehem kubwa ya Dunia ilikua inatawaliwa na kumilikiwa na UTAWALA WA FALME YA KIRUMI (ROMAN EMPIRE).

Warumi au Waroma walitawala Kwa muda mrefu sana karibu sehem yote ya dunia chini ya wafalme mbalimbali waliofahamika kama KAISARI (CAESAR).

Katika kila jimbo la utawala wa kirumi, likiwemo jimbo alimozaliwa Yesu la JUDEA aliwekwa mtawala na msimamizi mkuu wa serikali ya kirumi, aliyefahamika kwa cheo cha GAVANA. Kipindi cha Yesu Kristo, Gavana wa JUDEA alijulikana kwa jina la PONTIAS PILATE (PONSIO PILATO)', na alikua chini ya Mfalme wa Roma aliyejulikana kama (TIBERIUS CAESAR).

Kazi kubwa ya kwanza ya Gavana wa Roma katika jimbo ilikua ni kulilinda jimbo na utawala wa kiroma kwa nguvu za kijeshi, na ndio maana kila gavana alipewa wanajeshi wasiopungua 3000 kwa kazi hiyo. Kama mwakilishi wa utawala wa kiroma kazi yake nyingine ilikua ni kuhakikisha anakusanya KODI pamoja na kutoa hukumu(mahakama) katika makosa mbalimbali kwa mujibu wa sheria za kiroma.

utawala wa kiroma pia uliwatumia wenyeji wa maeneo wanayoyashikilia katika utawala, hasa katika utawala wa ngazi za chini au serikali za mitaa, waliyatumia makabila mbalimbali, au viongozi wa Dini inayotawala sehemu hiyo. Mfano katika jimbo la Judea na Jerusalem lilikuwepo baraza la Makuhani au Walimu na Viongozi wa dini, baraza hilo lilijulikana kama SANHEDRIN Kwa lugha ya kiyahudi.

SANHEDRIN ni nini?
Historia inatuambia kuwa Waislael waliamriwa na Mungu kuanzisha mahakama ya majaji na mahakimu ambao walipewa mamlaka ya kuwahukumu waisrael wanapokwenda kinyume na matakwa ya Mungu wao kwa mujibu wa sheria walizopewa na Mungu wao. Majaji hao wote walikua ni wale Viongozi wa Dini pamoja na Walimu wa Dini.

Kiongozi mkuu wa kidini (KUHANI MKUU) au kiongozi wa baraza la SANHEDRIN katika jimbo la Judea aliitwa CAIPHAS (KAYAFA). Viongozi wote hawa wa kiyahudi kama historia inavyotuambia walikua chini ya utawala wa Kiroma na walifanya shughuli zao kwa umakini na uwoga pasipo kuitilafiana na watawala wao WARUMI. Na moja ya jukumu lao ilikua ni kuhakikisha haitokei vurugu ya aina yoyote miongoni mwa WAYAHUDI wala mtu anayepingana na utawala wa kirumi, ama sivyo PILATO aliwatishia kuwa atalifunga hekalu lao la kuabudia.

Utawala wa warumi ulikuwa ni wa kibabe na kimabavu sana kiasi kwamba watu walikua wameuchoka na walikua wakisubir siku moja atokee mtu awaokoe katika utawala huo, kwani walichoka kulipa kodi, kuuliwa hovyo na pia kutumikishwa kwa kazi ngumu na utawala huo warumi, kifupi ni kwamba walichoka kutawaliwa.

Yesu Kristo alipoingia Jerusalem, alifanya matukio ambayo yaliwashtua watawala wa mji huo hasa MAFARISAYO au Makuhani, na kuona kua ujio wake unatishia utawala wao na vilevile waliogopa kwamba Yesu Kristo anaweza kuwa chanzo cha vurugu zilizokatazwa na PONSIO PILATO.

Moja ya tukio alilolifanya Yesu lilikua lile la kuvamia hekalu na kuanza kumwaga mwaga bidhaa pamoja na fedha za wafanyabiashara waliokuwemo humo, kitendo hicho kiliamsha shangwe na vigelegele miongoni mwa wayahudi wakimuona kama mkombozi wao katika utumwa huo wa kiroma. Pia Yesu aliongea maneno yaliyoamsha maswali, maneno yaliyoashiria Mapinduzi ya kiutawala. Yesu alisema; mathayo 24:2.

"Sawa, mnaweza kuyatazama haya yote! Kweli nawaambieni, hakuna hata jiwe moja litakalosalia hapa juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."

Wafarisayo hao waliona kua huo ni mpango wa kuangusha utawala wao na hivyo wakakubaliana kua Yesu lazima adhibitiwe haraka iwezekanavyo. Na ndio maana hata CIAPHAS (KAYAFA) aliamuru kuwa Yesu akamatwe na ahukumiwe haraka usiku kwa usiku, tena usiku wa manane jambo lililovunja sheria za kiyahudi (JEWISH LAWS) zilizoelekeza hukumu zote kutolewa mchana kweupe tena mbele ya umati wa watu.

Yesu alipokamtwa mwanzoni alituhumiwa kwa kosa la Kupotosha imani ya Dini na Mungu wao kwa maana nyingine alikua ANAKUFURU (BLASPHEMY) kitendo cha Yesu kujitangaza kua.yeye ni mwana wa Mungu na Tayari Maandiko yote waliyoyasubir wayahudi hao kayatimiza ilionekana kua KUFURU kwao, hivyo viongozi hao wa dini waliona wamuadabishe yesu.

Lakini kutokana na kwamba wao hawana mamlaka ya kutoa hukumu bali mwenye mamlaka hayo alikua ni PONTIAS PILATE, iliwaradhimu wampeleke Yesu kwa Pilato. Lakini wazee hao wa baraza la SANHEDRIN walipofika kwa Pilato Walizibadirisha tuhuma na wakamtuhumu Yesu kwamba anachochea mapinduzi ya serikali ya kirumi kwa kuwakataza watu wasilipe kodi kwa KAIZARI na vile vile anajiita MFALME, Jambo ambalo kwa mujibu wa sheria za Roma ilikua ni Uhaini (TREASON). Hii ni kwa mujibu wa kitabu cha LUKA.

Yesu alimshawishi ZACCHAEUS (ZAKAYO MTOZA USHURU)wa mji wa YERICHO ambae alikua Mkuu wa Watoza ushuru, aache kazi ya kutoza ushuru na amfuate, Yericho, ni mji uliokua ndani ya eneo la ukusanyaji kodi la Pilato. (Luka 19:2-19)

KWA NINI PONTIAS PILATE (PONSIO PILATO) ALIMUHUKUMU YESU JAPO HAKUMKUTA NA KOSA KWA MUJIBU WA SHERIA ZA KIROMA?

Historia inatuambia kua Pilato alipingana na maelezo ya makuhani na kuyaona kuwa hayana uzito wa adhabu wanayopendekeza Yesu apewe. Alitaka kulithibitisha hilo kwa kumuuliza Yesu maswali ambayo lengo lake ni kuona kama kweli Yesu ni Tishio kwa utawala wa Kirumi. Pilato alimuuliza Yesu,

"Wewe ni mfalme wa Wayahudi?" Yesu akamjibu hayo umetamka wewe.
Pilato aliwarudia makuhani na kuwawmbia

Simuoni mtu huyu kua na tuhuma. Makuhani wakamjibu, lakini amevunja sheria, pilato akawaambia, amevunja sheria zenu sio sheria za kaisari.

Pilato alitoa hukumu ya yesu kuteswa mpaka kufa kwa woga wa kutokea vurugu zitakazompelekea kushindwa kutawala, kwani Aliwaza kua kama hatatoa hukumu hiyo kwa Yesu CAIPHAS atampa lawama zote endapo yatatokea machafuko na vurugu ndani ya jimbo lake la utawala. Vile vile aliogopa kuwajibishwa na KAIZARI endapo vurugu zingetokea, angeonekana ameshindwa kutawala.

Yesu alihukumia Kifo (Death Penalty).
Ukichunguza uchambuzi katika maelezo hayo utaona kuwa kulikua na mvutano wa kisiasa katika uongozi wa nani anakubalika zaidi na nani anataka kumpindua nani. Makuhani pamoja na Wazee wa baraza walitishwa kuwa Yesu kaja kuharibu utawala wao na labda walikua wanapata maslahi zaidi kutoka katika utawala wa kirumi hivyo ujio wa Yesu ulikuja kutiachanga katika kitumbua chao.

Upande wa Pilato japo alidai kua hausiki na mauaji ya Yesu kwa kunawa mikono kwa maji kuashiria kua Umwagaji Damu wa Yesu hausiki nao, alisema

"Sina hatia na damu ya mtu huyu, jambo hili ni juu yenu ""

lakini tamaa ya Madaraka ilimsukuma kutoa hukumu hiyo, uwezekano wa yeye kupinga tuhumu na kuamuru Yesu aachiwe huru ulikua mkubwa na ulikua ndani ya uwezo wake kwa sababu Gavana wa kirume kwa kipindi chao alikua yeye ndiye sheria na yeye ndiye mahakama muamuzi wa mwisho. Lakini alihisi kama angefanya hivyo ingekua mwisho wa utawala wake.

Asanteni kwa Kusoma maandishi haya.
(sept.2016)
Very interesting story, nineipenda.. Hata hivyo Nina maswali mengi ya kuuliza.

He hii dola ya rum ilipindukiwa na nani, mwaka gn

Maswali mengine tayafata.....

Hata hivyo nimrkutana na maneno mawili ya kigeni.


SANHEDRIN السنهدرين majlis kwa maana ya baraza, mahakama

CAIPHAS - linakaribiana na neno CALIPHATE - kwa maana ya kiiongozi wa dini na mtawala.
 
Maandiko watu wanayosema ndio ushahidi wa kuwa Yesu alisulibishwa kama ilivyopangwa hayapo kwenye Torah. Wenye agano la kale wenyewe (Wayahudi) wanapishana na christianity. Waliokuja kupindisha facts ni wale waliotala kufanya ukristu uenee na kuuchanganya na upagani. Wenye agano la kale hawaamini masihi atasulubishwa na kufufuka. Hakuna mstari huo kwenye original Torah.

Pia in addition to that, according to Torah, the Messiah will:

Ezekiel 37:26-28: Build the Third Temple
Isaiah 43:5-6: Gather all Jews back to the Land of Israel
Isaiah 2:4: Usher in an era of world peace, and end all hatred, oppression, suffering and disease. "Nation shall not lift up sword against nation, neither shall man learn war anymore."
Zechariah 14:9: Spread universal knowledge of the G-d of Israel - uniting the entire human race as one: "G-d will be King over all the world—on that day, G-d will be One and His Name will be One"
Jesus fulfilled none of these messianic prophecies. Additionally:

Jesus was not a prophet. Prophecy could only exist in Israel when the land is inhabited by a majority of world Jewry. During the time of Ezra (~300 BCE) the majority of Jews refused to move from Babylon to Israel, thus prophecy ended upon the death of the last prophets (Haggai, Zechariah and Malachi). Jesus appeared on the scene approximately 350 years after prophecy had ended.
Jesus was not descended from King David. Per Genesis 49:10 and Isaiah 11:1, the Messiah must be descended on his father's side from King David. However, according to the Christian claim that Jesus was the product of a virgin birth, he had no father -- and thus could not have possibly fulfilled the messianic requirement of being descended on his father's side from King David! The Christian idea of a virgin birth is derived from a verse in Isaiah describing an "alma" as giving birth. The word "alma" has always meant a young woman, but Christian theologians came centuries later and translated it as "virgin." This accords Jesus' birth with the first century pagan idea of mortals being impregnated by G-ds.
Tradition teaches that the Messiah will lead the Jewish people to full Torah observance. Deut. 13:1-4 states that all mitzvahs remain binding forever, and anyone coming to change the Torah is immediately identified as a false prophet. Throughout the New Testament, Jesus contradicts the Torah and states its commandments are no longer applicable. (John 1:45 and 9:16, Acts 3:22 and 7:37)
U know absolute nothing dude

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio maana Yesu alipanda punda badala ya Farasi alipokuwa anaenda Jerusalem
 
Si lengo wala dhamira yangu kupinga wala kupindisha Imani ya mtu yeyote, bali ni wajibu wangu kama binadamu mwenye akili na upeo wa kudadisi, kuchanganua na kuyaelewa mambo mbalimbali katika namna tofauti tofauti.

Biblia ni kitabu kama vilivyo vitabu vingine vyenye maarifa, tamaduni na vinavyoelezea hisia za jamii za watu wake, isipokua Biblia ni kitabu maarufu kuliko kitabu chochote kilichowahi kuandikwa katika taaluma ya uandishi hapa Duniani.

Uchambuzi wangu utajikita zaidi katika kuelezea kifo cha Yesu Kristo ambaye historia kupitia vitabu mbalimbali vinavyounda kitabu kikuu cha biblia inatueleza kuwa ndiye chanzo cha Dini ya kikisto au kwa lugha ya kigeni dini hiyo inajulikana kama CHRISTIAN yenye tafsiri ya Wafuasi wa Yesu Kristo.

Historia kutoka katika vitabu vya MATHAYO na LUKA inatuambia kua Yesu Kristo alikua MYAHUDI na alizaliwa sehemu ijulikanayo kama BETHLEHEM katika jimbo la JUDEA. Wakati huo sehem kubwa ya Dunia ilikua inatawaliwa na kumilikiwa na UTAWALA WA FALME YA KIRUMI (ROMAN EMPIRE).

Warumi au Waroma walitawala Kwa muda mrefu sana karibu sehem yote ya dunia chini ya wafalme mbalimbali waliofahamika kama KAISARI (CAESAR).

Katika kila jimbo la utawala wa kirumi, likiwemo jimbo alimozaliwa Yesu la JUDEA aliwekwa mtawala na msimamizi mkuu wa serikali ya kirumi, aliyefahamika kwa cheo cha GAVANA. Kipindi cha Yesu Kristo, Gavana wa JUDEA alijulikana kwa jina la PONTIAS PILATE (PONSIO PILATO)', na alikua chini ya Mfalme wa Roma aliyejulikana kama (TIBERIUS CAESAR).

Kazi kubwa ya kwanza ya Gavana wa Roma katika jimbo ilikua ni kulilinda jimbo na utawala wa kiroma kwa nguvu za kijeshi, na ndio maana kila gavana alipewa wanajeshi wasiopungua 3000 kwa kazi hiyo. Kama mwakilishi wa utawala wa kiroma kazi yake nyingine ilikua ni kuhakikisha anakusanya KODI pamoja na kutoa hukumu(mahakama) katika makosa mbalimbali kwa mujibu wa sheria za kiroma.

utawala wa kiroma pia uliwatumia wenyeji wa maeneo wanayoyashikilia katika utawala, hasa katika utawala wa ngazi za chini au serikali za mitaa, waliyatumia makabila mbalimbali, au viongozi wa Dini inayotawala sehemu hiyo. Mfano katika jimbo la Judea na Jerusalem lilikuwepo baraza la Makuhani au Walimu na Viongozi wa dini, baraza hilo lilijulikana kama SANHEDRIN Kwa lugha ya kiyahudi.

SANHEDRIN ni nini?
Historia inatuambia kuwa Waislael waliamriwa na Mungu kuanzisha mahakama ya majaji na mahakimu ambao walipewa mamlaka ya kuwahukumu waisrael wanapokwenda kinyume na matakwa ya Mungu wao kwa mujibu wa sheria walizopewa na Mungu wao. Majaji hao wote walikua ni wale Viongozi wa Dini pamoja na Walimu wa Dini.

Kiongozi mkuu wa kidini (KUHANI MKUU) au kiongozi wa baraza la SANHEDRIN katika jimbo la Judea aliitwa CAIPHAS (KAYAFA). Viongozi wote hawa wa kiyahudi kama historia inavyotuambia walikua chini ya utawala wa Kiroma na walifanya shughuli zao kwa umakini na uwoga pasipo kuitilafiana na watawala wao WARUMI. Na moja ya jukumu lao ilikua ni kuhakikisha haitokei vurugu ya aina yoyote miongoni mwa WAYAHUDI wala mtu anayepingana na utawala wa kirumi, ama sivyo PILATO aliwatishia kuwa atalifunga hekalu lao la kuabudia.

Utawala wa warumi ulikuwa ni wa kibabe na kimabavu sana kiasi kwamba watu walikua wameuchoka na walikua wakisubir siku moja atokee mtu awaokoe katika utawala huo, kwani walichoka kulipa kodi, kuuliwa hovyo na pia kutumikishwa kwa kazi ngumu na utawala huo warumi, kifupi ni kwamba walichoka kutawaliwa.

Yesu Kristo alipoingia Jerusalem, alifanya matukio ambayo yaliwashtua watawala wa mji huo hasa MAFARISAYO au Makuhani, na kuona kua ujio wake unatishia utawala wao na vilevile waliogopa kwamba Yesu Kristo anaweza kuwa chanzo cha vurugu zilizokatazwa na PONSIO PILATO.

Moja ya tukio alilolifanya Yesu lilikua lile la kuvamia hekalu na kuanza kumwaga mwaga bidhaa pamoja na fedha za wafanyabiashara waliokuwemo humo, kitendo hicho kiliamsha shangwe na vigelegele miongoni mwa wayahudi wakimuona kama mkombozi wao katika utumwa huo wa kiroma. Pia Yesu aliongea maneno yaliyoamsha maswali, maneno yaliyoashiria Mapinduzi ya kiutawala. Yesu alisema; mathayo 24:2.

"Sawa, mnaweza kuyatazama haya yote! Kweli nawaambieni, hakuna hata jiwe moja litakalosalia hapa juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."

Wafarisayo hao waliona kua huo ni mpango wa kuangusha utawala wao na hivyo wakakubaliana kua Yesu lazima adhibitiwe haraka iwezekanavyo. Na ndio maana hata CIAPHAS (KAYAFA) aliamuru kuwa Yesu akamatwe na ahukumiwe haraka usiku kwa usiku, tena usiku wa manane jambo lililovunja sheria za kiyahudi (JEWISH LAWS) zilizoelekeza hukumu zote kutolewa mchana kweupe tena mbele ya umati wa watu.

Yesu alipokamtwa mwanzoni alituhumiwa kwa kosa la Kupotosha imani ya Dini na Mungu wao kwa maana nyingine alikua ANAKUFURU (BLASPHEMY) kitendo cha Yesu kujitangaza kua.yeye ni mwana wa Mungu na Tayari Maandiko yote waliyoyasubir wayahudi hao kayatimiza ilionekana kua KUFURU kwao, hivyo viongozi hao wa dini waliona wamuadabishe yesu.

Lakini kutokana na kwamba wao hawana mamlaka ya kutoa hukumu bali mwenye mamlaka hayo alikua ni PONTIAS PILATE, iliwaradhimu wampeleke Yesu kwa Pilato. Lakini wazee hao wa baraza la SANHEDRIN walipofika kwa Pilato Walizibadirisha tuhuma na wakamtuhumu Yesu kwamba anachochea mapinduzi ya serikali ya kirumi kwa kuwakataza watu wasilipe kodi kwa KAIZARI na vile vile anajiita MFALME, Jambo ambalo kwa mujibu wa sheria za Roma ilikua ni Uhaini (TREASON). Hii ni kwa mujibu wa kitabu cha LUKA.

Yesu alimshawishi ZACCHAEUS (ZAKAYO MTOZA USHURU)wa mji wa YERICHO ambae alikua Mkuu wa Watoza ushuru, aache kazi ya kutoza ushuru na amfuate, Yericho, ni mji uliokua ndani ya eneo la ukusanyaji kodi la Pilato. (Luka 19:2-19)

KWA NINI PONTIAS PILATE (PONSIO PILATO) ALIMUHUKUMU YESU JAPO HAKUMKUTA NA KOSA KWA MUJIBU WA SHERIA ZA KIROMA?

Historia inatuambia kua Pilato alipingana na maelezo ya makuhani na kuyaona kuwa hayana uzito wa adhabu wanayopendekeza Yesu apewe. Alitaka kulithibitisha hilo kwa kumuuliza Yesu maswali ambayo lengo lake ni kuona kama kweli Yesu ni Tishio kwa utawala wa Kirumi. Pilato alimuuliza Yesu,

"Wewe ni mfalme wa Wayahudi?" Yesu akamjibu hayo umetamka wewe.
Pilato aliwarudia makuhani na kuwawmbia

Simuoni mtu huyu kua na tuhuma. Makuhani wakamjibu, lakini amevunja sheria, pilato akawaambia, amevunja sheria zenu sio sheria za kaisari.

Pilato alitoa hukumu ya yesu kuteswa mpaka kufa kwa woga wa kutokea vurugu zitakazompelekea kushindwa kutawala, kwani Aliwaza kua kama hatatoa hukumu hiyo kwa Yesu CAIPHAS atampa lawama zote endapo yatatokea machafuko na vurugu ndani ya jimbo lake la utawala. Vile vile aliogopa kuwajibishwa na KAIZARI endapo vurugu zingetokea, angeonekana ameshindwa kutawala.

Yesu alihukumia Kifo (Death Penalty).
Ukichunguza uchambuzi katika maelezo hayo utaona kuwa kulikua na mvutano wa kisiasa katika uongozi wa nani anakubalika zaidi na nani anataka kumpindua nani. Makuhani pamoja na Wazee wa baraza walitishwa kuwa Yesu kaja kuharibu utawala wao na labda walikua wanapata maslahi zaidi kutoka katika utawala wa kirumi hivyo ujio wa Yesu ulikuja kutiachanga katika kitumbua chao.

Upande wa Pilato japo alidai kua hausiki na mauaji ya Yesu kwa kunawa mikono kwa maji kuashiria kua Umwagaji Damu wa Yesu hausiki nao, alisema

"Sina hatia na damu ya mtu huyu, jambo hili ni juu yenu ""

lakini tamaa ya Madaraka ilimsukuma kutoa hukumu hiyo, uwezekano wa yeye kupinga tuhumu na kuamuru Yesu aachiwe huru ulikua mkubwa na ulikua ndani ya uwezo wake kwa sababu Gavana wa kirume kwa kipindi chao alikua yeye ndiye sheria na yeye ndiye mahakama muamuzi wa mwisho. Lakini alihisi kama angefanya hivyo ingekua mwisho wa utawala wake.

Asanteni kwa Kusoma maandishi haya.
(sept.2016)
so?
mkuu Kwani aliyekuambia Yesu aliuawa kwa sababu za kidini ni nani
 
Back
Top Bottom