Nitaongelea kipengele kimoja cha wayahudi na waisrael kwa sasa.
katika historia ya makabila yale kumi na mbili (au kumi na tatu) maana kabila la Yusufu liliwakilishwa na wanae wawili, Manase na Efraim, yaligawanyika na kuunda falme mbili. Ufalme wa kusini uliitwa Yudea (Judah) na uliundwa na makabila mawili: Kabila la Yuda na kabila la Benjamin. Nadhani hawa ndio Jews (I stand to be 'collected', sorry..to be corrected).
Makabila mengine kama Asheri, Dani, Gadi, Naftali, Zebuloni, Simeoni, Rubeni, Isakari, Efraimu na Manase yaliunda Ufalme wa Kaskazini ulioitwa Waisrael (Israelites). Inasemekana kabila la Lewi (Walawi) halikuwa na makao maalum, lilisambaa kote kote miongoni mwa makabile yale mengine hivyo halikuwa na mji wake.
Hayo makabila yaliyounda ufalme wa kaskazini ndiyo yalishambuliwa na mnamo karne kama ya nane BC na kuangushwa na watu wote kuchukuliwa mateka na baadaye kuwa integrated kwenye miji mingine ya ufalme wa Ashuru (Assyria) 2Wafalme 17. Hayo ndiyo makabila ya Israel ambayo inasemekana yamepotea maana hawakurudi tena kwenye nchi yao. Kwa maana hiyo, hata wale ambao walikumbana na panga la Hitler, walikuwa wayuda/Jews/Judah people maana wale wengine hawakupata kusikika tena. Nasikia siku hizi kuna juhudi za kutafuta The Lost Tribes of Israel, sijui kama zitafanikiwa.