Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

TSHISHIMBI AANZA KUJIFUA TAYARI KWA LIGI KUU TANZANIA
.

Dar es Salaam. Baada ya kukosa michezo miwili ya Ligi Kuu Tanzania Bara, nahodha wa Yanga, Papy Tshishimbi leo ameanza mazoezi kujiandaa kurudi kikosini.

Tshishimbi amekosa mchezo dhidi ya Polisi Tanzania ambapo timu yake iliambulia pointi moja nyumbani baada ya kukubali sare ya bao 3-3 na mchezo dhidi ya Coastal Union ambapo timu yake ilipata ushindi wa bao 1-0.

Tshishimbi alisema anaendelea vizuri na jana ameanza mazoezi mepesi huku akibainisha kuwa wiki mbili za kupisha timu za taifa kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya Rwanda atakuwa amerudi katika kiwango chake. "Mazoezi mepesi nimeanza Jana na timu inawiki mbili hadi kucheza mchezo wa Ligi natarajia kuwa miongoni mwa nyota watakaocheza mchezo huo kama mwalimu atanipa nafasi," alisema Tshishimbi.

Tshishimbi alitumia nafasi hiyo kuwapongeza wachezaji wenzake kwa kufanikisha timu kupata pointi tatu dhidi ya Coastal Union.

Yanga Fulldozz
 


DROO YA MTOANO KOMBE LA SHIRIKISHO KUFANYIKA KESHO JUMATANO
.

Droo ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika na hatua ya mtoano kombe la Shirikisho itafanyika kesho Jumatano, Cairo Misri

Jioni ya kesho, macho na masikio ya Wanayanga yataelekezwa huko Misri kwani baada ya droo hiyo Yanga itamfahamu mpinzani wake wa hatua hiyo kusaka nafasi ya kucheza makundi kwa mara ya tatu katika kipindi cha miaka minne

Aidha kwa upande wa ligi ya mabingwa, timu 16 tayari zimeshapatikana hivyo kutakuwa na zoezi la kupanga makundi manne ya timu nne nne

Hizi hapa timu 16 zilizofuzu shirikisho ambazo zitaungana na timu nyingine 16 zilizotolewa raundi ya kwanza michuano ya ligi ya mabingwa

Mpinzani wa Yanga atatoka miongoni mwa timu hizi

1.RS Berkane (Morroco)
2.Al Masry(Egypt)
3.Hassania Agadir (Morroco)
4.Zanaco (Zambia)
5.Enugu Rangers (Nigeria)
6.Djoliba (Mali)
7.Esae(Benin)
8.DC Motema PEMBE (DRC)
9.FC San Pedro(Ivory Coast)
10.Bandari (Kenya)
11.Bidvest Witts(South Africa)
12.Ts Galaxy (South Africa)
13.Ploline (Uganda)
14.Triangle (Zimbabwe)
15.Pyramids (Egypt)
16.Paradou (Algeria)

Yanga ina uwezekano mkubwa wa kupangwa na moja ya timu kati ya namba 07 mpaka 16 kulingana na marks zinazotolewa na CAF kwa kuangalia mafanikio ya timu kwenye michuano iliyopita

Yangafulldozz
 
YONDANI APATA MAJERUHI
.
Beki kisiki wa Yanga Kelvin Yondani ameongeza idadi ya majeruhi wa kikosi cha timu hiyo ambacho baadae mwezi huu, kinakabiliwa na mchezo wa mtoano kombe la Shirikisho

Yondani alipata majeraha kwenye mchezo wa ligi kuu juzi dhidi ya Coastal Union

Alishindwa kumaliza mchezo huo ambao nafasi yake ilichukuliwa na Mustafa Suleyman

Afisa Habari wa Yanga Hassan Bumbuli amesema wachezaji tisa wa timu hiyo ni majeruhi

Wachezaji wengine ambao ni majeruhi au wagonjwa ni Lamine Moro, Raphael Daudi, Patrick Sibomana, Papy Tshishimbi, Mohammed Issa 'Banka', Paul Godfrey na Sadney Urikhob

Hata hivyo Yanga imepata ahueni baada ya ligi kusimama kupisha michezo ya kalenda za FIFA na CAF

Hadi kufikia Oktoba 22 siku ambayo Yanga itakuwa Mwanza kupepetana na Alliance Fc, baadhi ya nyota wake watakuwa wamerejea kikosini

Yangafulldozz
 
ZAHERA ABAKIZA MECHI MOJA YANGA

Baada ya kukosa mechi za Ligi Kuu Bara msimu huu akiwa na kikosi cha Yanga, Kocha Mwinyi Zahera sasa amebakiza mechi moja pekee kuanza kukaa kwenye benchi la ufundi.

Hivi karibuni Kocha huyo ambaye ni raia wa Congo, alifungiwa mechi tatu baada ya kuingia uwanjani akiwa na mavazi ambayo si nadhifu kwa mujibu wa Tff huku kanuni za Bodi ya Ligi zikiwa haziruhusu.

Baada ya kifungo hicho, Zahera alikosa mechi mbili ambazo ni dhidi ya Polisi Tanzania na Coastal Union na sasa amebakiza mechi moja tu ili adhabu yake iishe.

Katika mechi mbili za Yanga zilizopita, bila Zahera, Yanga ilifanikiwa kupata alama nne baada ya sare ya 3-3 dhidi ya Polisi na ushindi wa bap 1-0 dhidi ya Coastal.

Yangafulldozz
 
Kwani Zahera ndio muarobaini wa matatizo ya Chura FC? Angalau wakati yeye hayupo mmepata ushindi kwa Coast
 
Ses tunajua amumpendi na hilo liko wazi kabisaaaa. Mi nimekumbusha tu kwamba kabakisha mechi moja Bhaaas. πŸ˜›
Nikwambie kitu mamii? Huyo msemaji wenu wa klabu ambaye wenyewe mnamuita kocha nyie wenyewe, kwahiyari yenu, bila kulazimishwa na mtu yeyote muda si mrefu mtamfungulia mlango wa kutokea maana mtaona anawazingua tu, yetu macho
 
Ngoja nikatafute jezi yangu ya PYRAMID mapema kabisa.
 
Asante MUNGU kwa kujibu maombi yangu
PYRAMID
PYRAMID
Hahahahahahahahahhahahahahahahahah Ni swala la muda tu dawa kuwaingia.
 
Mkichomoka kwa PYRAMIDS sishabikii mpira tena hadi kufa kwangu ......Kwisha jeuri yenu.
 

Wawakilishi pekee wa Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika Yanga SC wamepangwa kukutana na Pyramids ya Misri katika hatua ya mchujo kuwania nafasi ya kuingia hatua ya makundi ya michuano hiyo.
 
PATRICK SIBOMANA AANZA MAZOEZI MEPESI

Habari njema kwa wapenzi na Mashabiki wa Yanga ni kwamba mchezaji wao Patrick Sibomana anaendelea vizuri na tayari ameanza mazoezi mepesi huenda mpaka utakapofika mchezo wao wa Kwanza michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika na wapinzani wao Pyramids Fc mchezo utakaopigwa uwanja wa Taifa terehe 27-10-2019 jijini Dare es salaam yawezekana akawa fiti kuwavaa waarabu hao endapo mwalimu ataamua kumpanga,

Yanga inakabiliwa na majeruhi wengi ambao mpaka Sasa bado hatujapata taarifa kamili juu ya Afya zao na maendeleo yao, Mchezo wa Yanga vs Coastal Union majeruhi wa Yanga waliongezeka baada ya Beki mkongwe Kevin Yondani kuumia na kufanya idadi ya Mejeruhi wa Yanga kufikia nane,wachezaji wa Yanga ambao ni majeruhi hadi Sasa ni Paul Godfrey,Mo Banka,Lamine Moro,Sadney Arikhob,Papy Tshishimbi, Rafael Daud,na Patrick Sibomana ambae tayari ameanza mazoezi mepesi.

Tukumbuke pia Yanga ina michezo miwili ya Ligi kuu bara michezo itakayopigwa jijini mwanza dhidi ya Alliance Fc tarehe 22-10-2019 baada ya hapo itacheza na Mbao Fc tarehe 26-10-2019

Pia Klabu ya Yanga leo imeitisha mkutano wa wana habari utakaofanyika Saa 6:00 mchana makao makuu ya klabu pale Jangwani huenda kutakua na habari njema zaidi kuelekea mchezo wao dhidi ya Pyramids Fc karibuni wana habari wote.

@yangafulldoz
 
Mechi za kwanza itapigwa Oktoba 27 na mechi za marudiano ni November 3.
Wewe dada una roho ngumu sana kuendelea kuifuatilia Yanga waziwazi. Wenzio wanazima redio na TV, wanakuja kusikilizia mwisho wa mechi au kipindi cha michezo EFM
 
Ingekuwa kujiua ningejiuaga zamani sana Mkuu hasa ile mechi ya Simba na Yanga sijui ya mwaka gani ile ambapo mpaka first half yanga tuliongoza kwa bao 3 kisha second half zikakombolewa zote mana nilipataga maumivu ya ajabu.


Na ile ya Yanga kufungwa na Simba 6 - 0 tena kwao pale Jangwani (1976)?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…