Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Yupo japo nimeona Polisi Tanzania wameanza mizengwe sa sijajua kama tarehe nne atakuwepo sehemu ya mchezo.
Hivi hawa wapumbavu bado tu hawajakubali yaishe? Mbona nasikia walisainiana mkataba Wa kimangungo na Azam juu ya uhamisho wake Wa mkopo? Mana nasikia walikubaliana tu kwa mdomo kwamba aende polisi kwa mkopo Wa msimu mmoja na baadae azam wamewachenjia gia angani? Wametumwa hawa au!?
 
Mwinyi Zahera alitufanyia kitu mbaya sana! Kumuuza Makambo na kutuletea David Molinga! Mchezaji gani hana kabisa nguvu za miguu! Shuti lake utadhani ni la mtoto wa darasa la sita! Hana kabisa stamina. Aaaaaaaghhhh!!

Nina imani muda utakapowadia, Ditram Nchimbi na huyo Tariq nani sijui! watamchomesha mahindi mpaka aamue mwenyewe kuvunja mkataba na kurejea Congo.

Mkwasa ameanzisha viungo wanaocheza aina moja ya mchezo! Sijui lengo lake ni lipi. Mfano kuwaanzisha Kaseke, Ngasa na Sibomana. Kwa aina hii ya mfumo, kupata matokeo ni bahati nasibu. Aongeze mshambuliaji mwingine na kupunguza kiungo mmoja wa pembeni.

Mpira uko slow, hauvutii kabisa kwa wanajangwani.
 
Mkwasa anatakiwa awe kocha msaidizi na si kocha Mkuu. Uwezo wake Wa kufundisha mpira ni mdogo
 
Huyu Tarik Seif anaonekana kabisa ni mshambuliaji. Ana kitu cha kutusaidia bila shaka siku za usoni. Akija kucheza na Nchimbi, Sibomana upande wa kushoto, upande wa kulia awekwe Balama, Ngasa au Kaseke, Tshishimbi, Fei Toto na Makame katikati, pale nyuma Adeyuni, Yondani, Moro na Juma Abdul/Boxer!

Hakika hiyo tarehe 04 January, ushindi ni lazima. Molinga aanzie benchi ikibidi. Hongereni Yanga kwa ushindi ingawa kipindi cha kwanza mlicheza "Kimasihara sana" Muwe mnajifunza kwa wenzenu Simba, huwa hawalembi wanapopewa nafasi ya kucheza na mwalimi wao.
 
Hakuna Sheria za namna hiyo hii TFF ya Sasa sio fati ya kina ndolanga

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Na yule mtu ivory coast tumemsaini Leo asee sijui uwezo wake hasa ila ana umbo zuri sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…