Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Uzuri simba nae huwa anakufa!
Ni kweli kabisa kidunula1 ,Simba hua anakufa lakini sio kwa kelele za Chura bali pale anapopambana na wale wa level yake, miamba na majabali wenzake wa nyikan(TP Mazembe, Al Ahly, Zamalek, Esperance, Enymba, Santos etc) tena hafi kindezi bali hupambana hadi pumzi ya mwisho akijeruhiwa lakini na yeye hujeruhi na wakati mwingine kuua kabisaa kama alivowafanyia Vita FC na Nkana Red Devils.

Huo ndio mfano ukitaka ulinganifu kati ya Wanalunyasi, Wekundu wa Msimbazi Simba SC na Wanachura FC kutokea Bonde la mpunga Jangwani
 
Nimekaona kakikosi kenu ka vijamamaa vya kurukaruka tu
 
Tusubiri tuone huyo Kaimu Meneja mpya atakuja na yepi.

Halafu nashangaa mwanzoni habari za kutafuta kocha mpya zilikuwa moto moto ila ghafla zimekuwa tulii.

Watutafutiage Kocha bwana.
Mmegundua pale hamna kocha eeh Shadeeya?

Ila naona kama mnaanza kutafuta visingizio mapeeeemaaa🤣🤣🤣
 
Ukitutajia vita na al ahly unatonesha vidonda vya wenzako vinaitwa hamsa
 
Kuishabikia Yanga ni 1wapo ya dalili za kutaka kujinyonga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
vita na al ahly kwa simba ni sawa unafanisha ukimwi na malaria

Jamaa wapo level nyingine acha kujipa moyo mlisaidiwa tu na upepo wa kisulisuli acha kujimwambafy
Ndo mana mwaka huu mmechezea za uso raund ya kwanza tu chalii ndo ujue unapozungumzia miamba ya Africa nyie paka wenye manyoya bado sana mna safari ndefu
 
Bahati nzuri ile haikua mara ya kwanza kwa timu za Misri ikiwemo Ahly kufa mbele ya Simba, tangia 1974 alipokaa Mehla El Kubra hapo Shamba la bibi imekua ni kawaida ya Simba kuwafunga Waarabu kila wakanyagapo Tanzania kucheza na Lunyasi

Yanga hawana historia ya kuwafunga Waarabu, si nyumbani wala ugenini, kwahiyo tusiwabeze Wekundu wa Msimbazi hata kama wanapoteza mechi zao za ugenini na hao jamaa
 
Hapa yanga anapigwa si chini ya goli 3

Sent using Jamii Forums mobile app

Hili ni jukwaa la Wana Yanga! Huoni umepotea njia?

Mungu ibariki timu yetu ya Yanga. Kufungwa na hawa mbumbumbu fc, ni jambo lisilokubalika. Bora kupata hata sare. Nilitamani sana na Tarik Seif awepo, ila ndiyo hivyo tena.

Kwa uwingi huu wa viungo walioanza kwenye mechi hii, na hivyo kubakia na mshambuliaji mmoja tu mbele, ni kazi sana kupata ushindi, zaidi tu ya kutuliza mashambulizi ya mpinzani.

Nina imani benchi la ufundi baadae litafanya mabadiliko na hivyo kupunguza kiungo mmoja na hasa Niyonzima ambaye ameonekana hana kabisa mechi fitness.
 
Subirini dawa iwaingie

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…