Your Majesty
JF-Expert Member
- Aug 29, 2018
- 3,242
- 5,345
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Peleka kwenye uzi wa simba huko.
ilikuwa ni salamu tu, simba anahisi njaaPeleka kwenye uzi wa simba huko.
Sent from my Infinix-X551 using Tapatalk
Nasikia huyu mnyama ashagoma hata msilitumie jina lake mana yeye huwa habebwi kwenye kutafuta msosi.
Ujumbe wa karne huuKwa mujibu wa vitabu vya dini Biblia, Torah na Quran, mwenyezi Mungu alimuumba Adam na baada ya Adam kuwa na upweke mwingi, mwenyezi Mungu alimshushia usingizi mzito na akazinyofoa mbavu zake za kushoto na kumuumba Hawa, ili amuondolee Adam upweke. Wawili hawa wakazaa watoto na vizazi vyao vikasambaa Dunia nzima.
Nadharia hii inauhusiano mkubwa na mambo mbali mbali duniani ikiwemo hapa kwetu Tanzania. Miaka 17 baada ya kutamatika kwa WW1 nikimaanisha mwaka 1935, enzi hizo ukoloni umeshamiri katika viunga vya Tanganyika na visiwani, iliundwa timu ya wananchi, timu ambayo iliundwa ili kuwaunganisha, kuwakutanisha, kuwaletea furaha na kuwaondolea adha na mateso ya ukoloni watanganyika, timu ya Young Africans.
Muda mfupi baada ya kuundwa timu ya Kwanza kabisa Tanganyika bara na visiwani, watanganyika sambamba na baadhi ya waarabu waligundua Young Africans inapitia kipindi kingi cha UPWEKE Kama kile alichokipita Adam baada ya kuumbwa. Ndio hapo likafanyika Jambo ili kumfurahisha Young Africans kwa kumletea mwenza (Hawa) ili amuondolee upweke mwingi aliokuwa nao. Mwaka 1936, baada ya mwaka mmoja wa shida,upweke na kulala kwa kukumbatia mito kila siku, hatimae muda ulifika na Young Africans akaketewa HAWA wake, kwa kuundwa timu ya Sunderland enzi hizo.
Hakika ilikuwa ni furaha ya ajabu, nderemo na vifijo vilitawala viunga vyote vya tanganyika, manamba mashambani, walimu mashuleni, wafanyakazi wa migodi,viwandani,Askari wa KAR, maakida na Liwali, wahindi na watu wote waliokuwepo enzi hizo hakika walifurahi baada ya Adam kuletewa Hawa wake.
Historia inaonyesha Hawa hana cha kusema mbele ya Adam, kwani Hawa kachapwa mara nyingi zaidi.
timu ya wananchi inakutana na timu iliyoundwa kuiondolea upweke, Adam anakutana na Hawa wake. Najua wakubwa mnaelewa Adam akikutana na Hawa nini kinatokea.
Tukutane Taifa..[emoji16]
Ikawaje?
Toka lini nikajificha miee Mtani. 🤣🤣😅