Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Ukiona hivyo ujue sina mishe za kuniweka busy leo Mtani. [emoji23]
Leo nimekupa nishani ya heshima kituo cha Pili[emoji23][emoji23][emoji23]

Si nilikwambia wewe ndio app yangu naona nafasi unaimudu vyema
 
Daaa natumai muda si mrefu mambo yatakuwa sawa
 
Wacha weee.

Hapo mlishajiokotea points za kununua halafu eti leo ndio unasema hutaki makando kando na malalamiko. Lol
Simba inapiga mpira mkubwa haiitaji kununua wala kuhonga ili kupata ushindi, level za Simba ni za Duniani huko siyo huku porini walipo Yanga🐸.
Jambo moja unatakiwa kujua unapoiongelea Simba jua unaiongelea Dunia kwa ujumla.
#Next level #Back2Back10 (kwa sauti ya haji manara)
Simba nguvu moja
Simba bingwa
 
Kuna lile goli la pili la Banka hadi mtangazaji akamwambia "aishi manula roho yako muhimu aishi" 😂😂😂

Alijua kabisa magoli ya Timu ya Wananchi yanaeza kuua mtu.
Shadeeya kumbe ulishaanza kunenepeana hovyo😜 kwa kujifariji na vigoli uchwara, subiri Mnyama Simba aje kufanya yake kwa kutwaa Ligi kuu na FA hakika mwili wako utarudi kwenye hali yake ya kawaida.😜
Simba nguvu moja
Simba bingwa
 
Yah!! Na kama mechi zile mbili za watani wa jadi alikuwa mwiba kwani beki za simba zilipata sana tabu.

Na kama sio janja janja ile mechi ya raundi ya kwanza yule mama alimnyima penalti ya wazi kabisa.
Aisee wewe Shadeeya acha mambo yako bwana, hivi wale waganga waliokaa golini kwenye dabi ya marudiano mlishawalipa pesa zao? Maana pale yangetokea maafa ila hayo mambo myaache yanamiaibisha sana.🐸
 
Ama kweli biashara asubuhi jioni mahesabu. Wamewahi mapema wakaandaa kitita cha kutosha wamekusanya maponti harakaharaka eti sahzi wanashusha pumzi kwa kutuambia sasa hivi tujiandae vema mana hakutakuwa na malalamiko ha ha ha ha!
Back2Back10

Simba nguvu moja
Simba bingwa
 
Sijui kama watakuelewa hawa haswa huyu Shadeeya.
 
Hata mimi nina shaka kama kweli watanielewa, haswa huyo Shadeeya ndio kabisaaa!!!🤣🤣🤣
Ni kweli Mkuu hawa watu kwa sasa hawako sawa tuwavumilie tu, unajua hakuna kipindi kigumu kama hiki kwa mashabiki wa Yanga ligi haijakwisha lakini tayari Bingwa wanamjua.
Hapa Shadeeya atapinga japo ndio ukweli anaoufahamu.
 
Mlikuwa mnapiga kelele eti ligi ifutwe halafu ili iweje sasa.
Walidhani watapewa wao ubingwa, tena ubingwa wa mezani kwq sababu kuna waandishi wa habari wali manazi wa Chura FC wanawavimbisha kichwa eti wanawaita "mabingwa wa kihistoria" ukiuliza maana yake nini wanasema Yanga ilichukuaga ubingwa mwaka 47!!!🤣🤣🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…