Nahodha Msaidizi wa Yanga Juma Abdul amesema wachezaji wa timu hiyo wana ari kubwa na wamepania kuwapa furaha mashabiki katika michezo iliyobaki
Yanga imerejea mazoezini wiki iliyopita, nyota hao wakiendelea kujifua chini ya kocha msaidizi Charles Boniface Mkwasa 'Master'
Abdul amesema wamepania kufanya vizuri katika michezo yote iliyobaki akitamba kuwa hawafikirii kama kuna mchezo watapoteza "Wachezaji wako tayari, we mwenyewe si unaona namna tulivyo na ari kubwa katika mazoezi, tunajiandaa kikamilifu na michezo iliyobaki ya ligi na ile ya FA "Hatutegemei kupoteza mchezo wowote tupo tayari kuikabili timu yoyote na tutapata matokeo chanya na sio kupoteza," amesema Abdul
Kipimo cha kwanza kwa mabingwa hao wa kihistoria ni siku ya Jumapili, Juni 07 ambapo wataumana na KMC katika mchezo wa kirafiki ambao utapigwa uwanja wa Uhuru
Baadae timu itaelekea mkoani Shinyanga ambapo Juni 13 itafungua rasmi ligi katika uwanja wa CCM Kambarage, kwa kuikabili Mwadui Fc.