Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Duu hadi Google wanatambua uhalisia Wa timu zetu ngoja nitafute maana ya Astronauts.
 
Mkuu ungewawekea kabisa na msimamo wa Ligi ulivyo sasa hivi maana Shadeeya and company hawakawii kubisha kua Lunyasi ndio Machampioni wa TPL kwa mwaka wa tatu mfululizo, tena wakiwa na mechi TANO mkononi๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€
Huyo ulie mtaja ni Binamu yangu wa damu lkn mkaidi kama kazaliwa nchi jirani๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†
 
Mkuu ungewawekea kabisa na msimamo wa Ligi ulivyo sasa hivi maana Shadeeya and company hawakawii kubisha kua Lunyasi ndio Machampioni wa TPL kwa mwaka wa tatu mfululizo, tena wakiwa na mechi TANO mkononi๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€
๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€
 
Daktari wa klabu ya Yanga Dk Shecky Mngazija amesema hali ya kiungo fundi Haruna Niyonzima ambaye alipata maumivu kwenye mchezo dhidi ya Biashara United, anaendelea vizuri.

Niyonzima alicheza mchezo huo kwa dakika saba tu baada kupata majeraha kwenye dakika ya tatu na kulazimika kutoka kwenye dakika ya saba baada ya kushindwa kuendelea na mchezo.

Dk Mngazija amesema Niyonzima anaendelea na matibabu na upo uwezekano atakuwa sawa kabla ya mchezo dhidi ya Kagera Sugar ambao utapigwa Julai 09.

Aidha ameeleza kusikitishwa na mchezo wa kibabe ulioonyeshwa na vijana wa Biashara United ambao umesababisha nyota wake kupata majeraha.

"Siyo Niyonzima tu, nahodha wetu msaidizi Juma Abdul na Abdulaziz Makame nao wamepata majeraha lakini tunashukuru wote wanaendelea vizuri," alisema.

Baada ya mchezo dhidi ya Kagera Sugar, Yanga itarejea jijini Dar es salaam ambapo Julai 12 inakabiliwa na mchezo wa nusu fainali kombe la FA dhidi ya Simba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ