Wachezaji 21 Yanga wazifuata Mtibwa Sugar, Lipuli
Kikosi cha wachezaji 21 na viongozi 10 cha Timu ya Wananchi kiliondoka jana jioni kwenda Morogoro na baadaye Iringa kwa ajili ya mechi za kumalizia Ligi Kuu.
Timu ya Wananchi itashuka Kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, kucheza na Mtibwa Sugar Jumatano kabla ya kwenda Iringa kuivaa Lipuli FC Jumapili katika mchezo wa funga Dimba wa Ligi.
Wachezaji walioondoka katika msafara ni pamoja na Farouk Shikhalo, Metacha Mnata, Ramadhan Kabwili na Geoffrey Magaigwa, Juma Abdul, Paul Godfrey, Ally Mtoni, Jafary Mohammed, Adeyum Saleh na Lamine Moro.
Wengine ni Faisal Salum, Abdullaziz Makame, Said Juma Makapu, Deus Kaseke, Mrisho Ngassa, Eric Kabamba Yikpe Gislain, David Molinga, Tariq Seif, Ditram Nchimbi na Adam Kiondo.
Benchi la ufundi linaongozwa na Kocha Mkuu Luc Eymael, Cassim Fareed, Redoh Burden, Abeid Mziba, Said Maulid, Fred Mbuna na Dr. Shecky Mngazija.
Viongozi wengine ni Mike Victor, Edward Martine Fungameza, Laurent Mmassy na Mkuu wa msafara Hassan Bumbuli pamoja na Dereva Sadick Bura.