Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

20201203_101137.jpg

Hafla ya ukabidhiwaji wa rasimu ya awali ya mabadiliko ya uwendeshwaji wa klabu ya Yanga umefanyika jana na kukabidhiwa na mwenyekiti wa kamati ya mabadiliko WAKILI ALEX MGONGOLWA akiambatana na meneja mradi huo ambaye pia ni MKURUGENZI wa Uwekezaji kutoka kampuni GSM Eng Hersi Said ambao ni WADHAMINI wa gharama za mradi huo.

Rasimu hiyo imepokelewa na Mwenyekiti Dkt. Mshindo Msolla akiambatana na wajumbe wa kamati ya utendaji, mjumbe wa baraza la wadhamini na wazee wa klabu yetu. Hakika leo ni siku ya KIHISTORIA katika maendeleo endelevu ya klabu yetu!

#daimambelenyumamwiko
#timuyawananchi
 
20201203_101211.jpg

Mwenyekiti wa klabu ya Yanga Dkt. Mshindo Msolla baada ya kupokea rasimu ya awali ya mabadiliko ya uwendeshwaji alimkabidhi Senzo Mbatha ambaye watashirikiana nae kusimamia mchakato huo kuelekea Mkutano Mkuu wa Wanachama.

#daimambelenyumamwiko
#timuyawananchi
 
20201203_101241.jpg
Picha ya pamoja, Uongozi wa klabu ya Timu ya Wananchi umepokea rasimu ya Mabadiliko kutoka kwa washauri wetu Kampuni ya laliga ambao wamekamilisha jukumu la kupendekeza mfumo bora wa uendeshaji.

#daimambelenyumamwiko #timuyawananchi
 
Baada ya ya Timu ya Wananchi kutangaza rasmi Zabuni ya Ujenzi wa Hostel na Uwanja wa Mazoezi wa Klahu huko Kigamboni


20201203_102147.jpg

Wakandarasi walioomba Zabuni hiyo kutoka makampuni zaidi ya 10 wakiwa kwenye uwanja wa klabu yetu ya Yanga Kigamboni, walivyotembelea na kujionea hali halisi kimazingira tayari kwa utekelezaji wa ujenzi wa uwanja wa mazoezi pamoja na hostel za wachezaji mara tu mshindi wa tenda atakapotangazwa.

#TimuYaWananchi #DaimaMbeleNyumaMwiko
 
naomba mtuwie radhi kwa kupata ushindi mwemba kama mpatavyo nyie watani ushindi wa kimoko kimoko
Duuh!!

Jumamosi inakaribia rafiki. Nasikia mnasema tusiende Uwanjani eti? ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Saa viingilio vya kwetu mnatuzuwiaje eti? ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ Hebu tuwacheni tukawashingile Plateau.
 
Duuh!!

Jumamosi inakaribia rafiki. Nasikia mnasema tusiende Uwanjani eti? ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Saa viingilio vya kwetu mnatuzuwiaje eti? ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ Hebu tuwacheni tukawashingile Plateau.
sherehe hujaalikwa, kwanini ujipendekeze kuja?
 
Back
Top Bottom