Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐒🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸🐸
 
Ni wale wale mlikua mnawapokea Airport au ni wengine?
 
Ukiitazama Yanga Afrika kwenye karatasi wala sio timu mbaya, kila Mchezaji ana kitu cha upekee ambacho kinaweza kukupa kitu kwenye VPL, ni timu nzuri tu kwenye karatasi wala sio timu mbaya kama watu wanavyodhani

LAKINI KWANINI WANAYUMBA? Kujenga timu yoyote ni process unaweza kukaa hata miaka mitatu ukiwa bado unajenga timu yako, kilichopo Yanga Afrka ni huo Mchakato wa ujenzi wa timu yao mpya, ni kawaida kupitia milima na mabonde mpaka kupata Mwanga

JE HUO MCHAKATO WATAFANIKIWA? Mpaka sasa naona wana asilimia chache ya kufanikiwa, kwakuwa kwanza Viongozi wamewaaminisha Mashabiki kuwa hawapo kwenye mchakato, wamewaaminisha Mashabiki kuwa timu ipo kamili na inaweza kupambana, matokeo yake ni PRESHA

UNADHANI KWANINI HAWATOFANIKIWA? Nimeitazama Yanga kwa misimu mitatu iliyopita na huu ndio wanne, kikosi chao kinabadilika sana, huwezi kuwa na Mchakato kama kila msimu unatoa watu 15 na kuleta watu 16, ni ngumu na hii inafanyika kila msimu, kuanzia wachezaji mpaka benchi la Ufundi

IPI NAFASI YA VIONGOZI MPAKA HAPA WALIPO? Binafsi sioni nafasi ya Viongozi kwenye mustakabari wa Yanga imara, ni hatari sana kama Mjumbe ana nguvu kuliko Mwenyekiti, ni hatari kama Viongozi wanaishi kwa matamko, ni hatari kama Viongozi hawawezi kukiri wazi walianguka na waanze upya, njia pekee waje mbele wakiri na waanze upya

KIPI SASA VIONGOZI WAFANYE? Kwanza ni kushusha presha maana Ligi ni Marathon, Simba hajacheza mechi zake hivyo wasijipe presha kuwa wamekosa ubingwa, pili wakae chini kugawa malengo yao, wana karata mbili, karata nyepesi zaidi ni kukaza FA, waondoke na kitu na nafasi ya Kimataifa waipate, kombe pia litasusha presha

NAFASI YA WACHEZAJI IKOJE? Nadhani wachezaji watambue kuwa wao ni sehemu ya project ya Yanga Imara, kila dakika 90 ziwe vita, wanaokaa bench wakiitwa waitike kwa moyo mmoja, kila Mtu acheze kwa niaba ya timu, hii ndio namna pekee ya kuendelea kusalia kwenye project

CHA KUMALIZIA NDUGU MCHAMBUZI? Nadhani Mwenyekiti afanye press ya maana kutoa mwelekeo wa Yanga Afrika uliojaa ukweli, ukweli mchungu ni bora kuliko maneno yasiyotekelezeka, kisha washushe presha na kutumia kikosi hiki kuanza Project mpya
 
Piga haoo
 
Ujenzi wa timu bila benchi bora ni ujinga, chukulia mfano Chelsea ya Lampard ilivyokuwa ina struggle, Tuchel kaingia within a week timu imebadilika.
 
Nimesikitika sana ila nimehisi uongozi Wa klabu unajificha kwenye kivuli cha Kaze na benchi lake! Wamenivunja moyo sana!
 
UKWELI HUJITENGA NA UWONGO VIONGOZI WAMETUONGOPEA SANA MWISHOWE MATOKEO NDIO HAYO VIJANA TULIOWALEA NDIO WALIOTUFUNGA KWA KILA MECHI DOGO WA COAST BUSWITA MUHILU WAMETUPROVE WRONG
Kaze amezingua sana! Hivi anafanya nini? Yaani leo ilikuwa inaonekana kabisa Fiston alichemsha mapema lakini bado yumo tu mpaka dakika 90! Nchimbi amekaaje muda wote huo?
 
Unabahati mbaya. Liverpool na Yanga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…