Yule Jaji aliyetajwa kusapoti wahuni wanaoiba ardhi za watu bado yuko kazini?

Waziri muhuni anajua anavojikoroga na analazimisha kutaja majaji Bungeni ili aonekane yupo sahihi anapokiuka msingi wa sheria. Tusubiri
Majaji wahuni pia wapo sana,na dawa yao ni kwenda nao kihunihuni kama tabia zao zilivyo za kihunihuni!!
 
Huyu Waziri wa Ardhi naona kama ni mnafiki tu, Kama KWELI yuko serious kabisa katika kutatua Migogoro ya Ardhi hapa nchini Tanzania, basi aanze kuifanyia marekebisho Wizara yake anayoiongoza kwa sababu hiyo ndio kinara wa kusababisha Migogoro ya Ardhi.
Awasulubu kwanza Watendaji wabovu wa Ardhi wanaohusika kwenye kusababisha Migogoro ya Ardhi, bila kusahau KUPELEKA MAANGAMIZI MAKUBWA KWA WENYEVITI WA MABARAZA YA ARDHI YA WILAYA (Mahakama za Ardhi) ambazo karibia zote kabisa zilizopo zimetekwa mateka na Matapeli na/au Waporaji wa Ardhi. Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya ni janga kubwa Sana kwa Wamiliki wa Ardhi hapa Tanzania, yamegubikwa kabisa na VITENDO VYA RUSHWA. Watu Wananchi maskini wamekuwa wahanga wakubwa wa kuporwa Ardhi zao na Matapeli wa Ardhi au Watu matajiri, Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya yamekuwa yakibariki Utapeli au uporaji huo. Awashughulikie kwanza hao Mahakimu wa Mabaraza hayo, kwani nao ni Waajiriwa wa Wizara yake ya Ardhi.
 
Mkuu hapa umeongea ukweli mtupu.....Ila kwa huyu Waziri - nina hakika atawfikia na hao wenyeviti wa mabaraza ya ardhi....akisafisha huko, watu watakuwa wameokoa ardhi zao. Maana huko ndio matapeli wamekuwa wakikutumia kufanya uharamia wao. Hata yeye Waziri anajua hilo - alishawahi kusema.
 
Sisi tunataka huku juu kwa Majaji pawe clean sana,maana madudu yote ya huko chini yanakuja kufutwa huku juu kwa Majaji, sasa Majaji nao wakianza kua na tabia kama za Mabaraza ya Aridhi hii ni aibu kubwa sana! Ukisoma kesi ya Mmasi aliyoshinda huko Baraza ni ubatili mtupu na uko wazi kabisa, sasa kukosa Jaji wa Mahakama kuu kua clean asingeifutia mbali ile hukumu ya Baraza! Sasa juu pakiwa pasafi angalau watu watakua na moyo wa kukimbilia kwa Majaji ili wapate haki zao zilizokandamizwa huko chini!!
 
Kwanini mabaraza ya aridhi hayakubadilishwa na kuwa mahakama za aridhi?
 
Tunataka kuona Vitendo, siyo kusema maneno tu bila vitendo.
Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya ni Janga kubwa Sana kwa Wamiliki wa Ardhi ambao ni walalahoi.
 
Sidhani kama upo sahihi kuhusu suala hili.

Kumbuka: Uimara wa Nyumba au Jengo lolote lile huanzia na hatua ya Ujenzi wa Msingi Imara. Kama msingi wa Nyumba siyo imara, basi hata Nyumba au Jengo lote haliwezi kuwa Imara. Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya ni Msingi kwenye suala hili.
 
Tatizo Watumishi wa hayo mabaraza wanalalamika wanapewa malipo kidogo sana,na ndiyo maana wanashawishika na kula rushwa tena bila hata ya aibu!!
 
Tatizo Watumishi wa hayo mabaraza wanalalamika wanapewa malipo kidogo sana,na ndiyo maana wanashawishika na kula rushwa tena bila hata ya aibu!!
You're completely Wrong!

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tz Bw. Edward Lowassa alijiuzuru nafasi yake ya Uwaziri Mkuu kutokana na tuhuma za vitendo vya rushwa kuhusisha Makampuni ya zabuni za ufuaji wa umeme. Je, unataka kusema kwamba Edward Lowassa alijihusisha na vitendo vya rushwa eti kwa sababu alikuwa anapata mshahara na marupurupu madogo kutokana na kazi/ajira au Cheo chake Cha Uwaziri Mkuu????Je, Unataka kusema kwamba Cheo Cha Uwaziri Mkuu hapa Tanzania kina mshahara Mdogo hali iliyomlazimu Edward Lowassa kujihusisha na rushwa ili kujiongezea kipato Cha ziada Cha kuweza kutosheleza au kukidhi mahitaji yake ya kiuchumi??????????????????????? Is it true???????????
 
....“Judges and judicial officers have always been awarded ‘absolute’ immunity for their judicial acts. Absolute immunity covers even conduct which is corrupt, malicious or intended to do injury.” ....


Hii hapa ni kutoka majuu kwa Biden.
 
Hivi kwa nn matapeli wengi wa ardhi na majumba ni akina mangi?
 
Hivi kwa nn matapeli wengi wa ardhi na majumba ni akina mangi?
Kina Mangi wao ndiyo wanajifanya wanajuwa thamani ya Aridhi kuliko kabila lolote lile Tanzania, ndiyo maana wao kupigana mapanga kisa ugomvi wa Aridhi hawaoni shida!!
 
"Mama kaambiwa na mahakama avunje wakati ana hati zote halali" una uhakika gani na uhalali wa hizo hati!!!! Hati huandikwa na binadamu na siyo Mungu, ndiyo maana mahakama ipo kuamua uhalali wa hizo hati za ardhi, zimepatikana vipi, ndiyo utawala wa sheria huo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…