TANZIA Yusuf Manji, Mfanyabiashara maarufu aliyewahi kuwa mdhamini wa Yanga SC afariki dunia nchini Marekani

TANZIA Yusuf Manji, Mfanyabiashara maarufu aliyewahi kuwa mdhamini wa Yanga SC afariki dunia nchini Marekani

View attachment 3029953
Yusuf Manji enzi za uhai wake
Mfanyabiashara maarufu na aliyekuwa mdhamini wa Klabu ya Yanga, Yusuf Manji amefariki dunia jana Jumamosi Juni 29, 2024 saa 6 usiku katika Jimbo la Florida nchini Marekani alipokuwa anapatiwa matibabu.

Taarifa za kifo hicho zimethibitishwa na mtoto wake, Mehbub Manji akizungumza na Mwananchi Digital muda mfupi uliopita.

Yusuf Manji alikuwa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Quality Group Limited (QGL), kampuni inayojihusisha na sekta mbalimbali kama vile magari, ujenzi, vifaa vya kilimo, utalii, huduma za afya, na mali isiyohamishika.

Manji pia alifahamika kwa kujihusisha na shughuli za kijamii na misaada mbalimbali nchini Tanzania. Pia amewahi kuwa mwenyekiti wa klabu ya soka ya Yanga.

Pia Manji alijihusisha na siasa kupitia Chama cha Mapinduzi na kufanikiwa kuwa Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu Manispaa ya Temeke. Septemba 6, 2017 alipoteza sifa ya Udiwani kutokana na kutohudhuria vikao zaidi ya sita na vikao vya kamati vya maendeleo ya halmashauri ya Temeke zaidi ya vitatu.

Atakumbukwa kwa mafanikio makubwa na mchango wake katika uchumi wa Tanzania.

Pia soma
- Yusuf Manji apoteza sifa ya kuwa Diwani wa Mbagala Kuu kwa kushindwa kuhudhuria vikao
Ninamkumbuka alivyowahonga pilau wanaccm wa Mbagala kwani walikula na kubeba yekiawei mpaka likawashinda, wakamchagua kuwa diwani wao, hata hivyo hakuwahi kuhudhuria vikao vya madiwani.
UMASIKINI AGHARI.
 
Hapa ndio Mungu alituletea usawa.

Uwe Tajiri sana, Uwe fukara sana.

Kukata moto kupo palepale.


Kumbe tukifa Mali zote tunaziacha, na kwamba wakati wa Kufa, Pesa haziwezi kuzuia huo mchakato.




Maana yake ni kwamba, Hata utoe Makafara uwe Tajiri, hata Udhulumu mtu, KUFA UTAKUFA TU.


SWALI NI JE..... UMEJENGA KWENU??? AU NDO UTAACHA WOSIA WA ,NIKIFA, MNIZIKE MAKABURI YA KINONDONI😂😂🥱
Lakini mkuu kuna tofauti gani ya kuzikwa kwenye makaburi ya umma na kuzikwa nyumbani kwako?

Mimi nijuavyo ukifa umekufa na haijalishi ni wapi utazikwa. Ardhi ni ile ile. Udongo wa Kinondoni na udongo wa nyumbani kwako, vyote ni udongo.
 
View attachment 3029953
Yusuf Manji enzi za uhai wake
Mfanyabiashara maarufu na aliyekuwa mdhamini wa Klabu ya Yanga, Yusuf Manji amefariki dunia jana Jumamosi Juni 29, 2024 saa 6 usiku katika Jimbo la Florida nchini Marekani alipokuwa anapatiwa matibabu.

Taarifa za kifo hicho zimethibitishwa na mtoto wake, Mehbub Manji akizungumza na Mwananchi Digital muda mfupi uliopita.

Yusuf Manji alikuwa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Quality Group Limited (QGL), kampuni inayojihusisha na sekta mbalimbali kama vile magari, ujenzi, vifaa vya kilimo, utalii, huduma za afya, na mali isiyohamishika.

Manji pia alifahamika kwa kujihusisha na shughuli za kijamii na misaada mbalimbali nchini Tanzania. Pia amewahi kuwa mwenyekiti wa klabu ya soka ya Yanga.

Pia Manji alijihusisha na siasa kupitia Chama cha Mapinduzi na kufanikiwa kuwa Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu Manispaa ya Temeke. Septemba 6, 2017 alipoteza sifa ya Udiwani kutokana na kutohudhuria vikao zaidi ya sita na vikao vya kamati vya maendeleo ya halmashauri ya Temeke zaidi ya vitatu.

Atakumbukwa kwa mafanikio makubwa na mchango wake katika uchumi wa Tanzania.

Pia soma
- Yusuf Manji apoteza sifa ya kuwa Diwani wa Mbagala Kuu kwa kushindwa kuhudhuria vikao
To Allah we belong and to him we will return
 
Ililuwaje wakawekwa kwenye payroll
Kipind Wana jitafuta walikuaga Wana mkatabaa na EATV Sasa wakawa wamesitisha mkatabaa na EATV Wakawa na mgogoro..

Kipindi icho icho Wakawa wanafukuzia kuanza kuonyesha ze comedy kwenye television ya TAIFA

Manji alitoa pesa yake mfukoni kulipia gharama zoteee na mishahara na marupurupu yoote kwa kina masanja na wenzake WOTE..

Unaweza ku search interview ya masanja akisimulia historia ya Maisha yake kwenye kipindi Cha ""THE CLASSIC WITH MASANJA" PRESENTER NI JABIR SALEH WA EFM RADIO
 
Back
Top Bottom