Zaa kwa mahesabu, sio uzae watoto waje kufanywa Watumwa huku Duniani

Zaa kwa mahesabu, sio uzae watoto waje kufanywa Watumwa huku Duniani

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
ZAA KWA MAHESABU, SIO UZAE WATOTO WAJE KUFANYWA WATUMWA HUKU DUNIANI!

Anaandika, Robert Heriel
Shahidi!

UTUMWA!
Usukule!
Kutumwa tumwa! Kuvujishwa jasho pasipo malipo, Kulambishwa mavumbi ya viatu pasipo utu. Kuimba pambio katika wimbo wa walao nchi.

Manamba na vibarua wa mashamba, HAO ndio utakaowazaa waje kujambishwa na watoto wa wenzako? Sitaki majibu Yako hapa! Baki nayo.

Zaa Kwa Hesabu zenye jawabu. Sio uzae kama panya, kuzaa watoto wengi Kwa Zama hizi bila Hesabu sio tuu kukosa upendo Bali ni ukatili Kwa watoto wako.

Katika ulimwengu WA teknolojia na Ujuzi na maarifa wingi sio hoja Bali vioja.

Unakuwa na watoto wengi ambao wanatumikishwa kwenye viwanda Kama randa la mbao ndivyo wanavyoranda Randa wakinuka jasho.

Nazaa watoto Saba, najiita kidume kwenye mfumo dume.
Taikon sina shamba wala kiwanja, lakini ninawatoto Saba.

Haipendezi kuzaa watoto waje watumikishwe na kuteswa alafu mzazi bila aibu nawe Kwa ukatili mtoto unamnyonya zaidi mwanao licha yakuwa kipato chake ni duni.
Huo ni ukatili, unyanyasaji na ukosefu wa utu.

Tuzae Kwa Hesabu.
Watoto ambao tunauwezo wa Kuwatunza na kuwaandalia maisha MAZURI na Urithi ili wasiwe Watumwa.

Sio unazaa wapiga Kura wa watoto wa wenzako waluoandaliwa.
Sio anazaa watoto ambao watakuja kuwa vibarua.

Sisemi Kwa ubaya, au kupangia mtu Maisha.
Ila Kwa kweli hakuna kitu kibaya Kwa mzazi mwenye upendo kuona umezaa watoto ambao umewaleta kuja kuteseka na kuteswa na wanadamu wengine.
Mzazi asiye na upendo WA dhati hawezi ona uchungu Kwa mwanaye.

Kwani wengi huzaa Kwa ubinafsi wao tuu. Wakitaka watoto wao waje wawasaidie baadaye lakini hawataki kuwaandaa watoto hao kuishi maisha MAZURI.
Huo ni Ubinafsi na ukatili.

Kama huna uwezo wa kuandaa watoto waishi maisha mazuri, zaa Kwa hesabu. Watoto wachache wanaokutosha.

Jitahidi uangalie Quality zaidi kuliko Quantity.
Sio mtu unajivunia unawatoto wengi lakini watoto uliozaa ni Watumwa, misukule, na watu wanaoteswa na watu wengine.

Zamani watu walizaa watoto wengi Kwa sababu walikuwa wanauwezo wa kuwarithisha mashamba, maboma, na Urithi mwingine.
Lengo jingine na kuleta nguvu kazi katika jamii.
Lakini vipi Zama za leo?

Je tutazaa Kondoo wengi ambao wataongozwa na Simba mmoja?
Au tutazaa Simba mmoja kuongozwa Kondoo wengi?
Au tutazaa Simba wengi kutawala Mbuga?

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Yaan mtu anazaliwa ili aje awe mchepuko kweli?
Awe chawa? Awe msifia watu wengine kama yeye?


Hapana aisee

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app

Kuna watu hawajali,
Wanaona kabisa Hali ngumu, wanaona kabisa hawana vitu vya kuwarithisha watoto wao, hasa Ardhi na mashamba ya uzalishaji,
Wanajiona kabisa wao ni misukule au Watumwa wanalipwa mishahara ya punda, lakini bado mtu anazaa watoto wengi ili wapatikane vibarua wengi zaidi wakutumikishwa.
Hiyo ni laana.

Kuzaa watoto wengi ni Enzi zile Ardhi ipo ya kutosha. Tena yenye rutuba. Unawakatia tuu vipande watoto wako.
Lakini siku hizi tabia ya nchi sio rafiki, hata ukimpa mtoto shamba bado anaweza kuhenyeshwa
 
Kuna watu hawajali,
Wanaona kabisa Hali ngumu, wanaona kabisa hawana vitu vya kuwarithisha watoto wao, hasa Ardhi na mashamba ya uzalishaji,
Wanajiona kabisa wao ni misukule au Watumwa wanalipwa mishahara ya punda, lakini bado mtu anazaa watoto wengi ili wapatikane vibarua wengi zaidi wakutumikishwa.
Hiyo ni laana.

Kuzaa watoto wengi ni Enzi zile Ardhi ipo ya kutosha. Tena yenye rutuba. Unawakatia tuu vipande watoto wako.
Lakini siku hizi tabia ya nchi sio rafiki, hata ukimpa mtoto shamba bado anaweza kuhenyeshwa
Sio tu kuzaa watoto wengi mimi kwangu hata kuzaa kwenyewe tu sitamani.
Dunia na ulimwengu wa sasa sio salama tena kwa binadamu sanasana watoto sanasana watoto wa kike na wa kiume.

Mimi kwa upande wangu ni bora niteseke kwa hali yeyote ile nipambane kwa namna yeyote na ikitokea nikafa basi nife mwenyewe kuliko kufa na kukiacha kizazi changu kiendelee na mambo kama haya ya kwangu.
 
Sio tu kuzaa watoto wengi mimi kwangu hata kuzaa kwenyewe tu sitamani,.
Dunia na ulimwengu wa sasa sio salama tena kwa binadamu sanasana watoto sanasana watoto wa kike na wakiume,.
Mimi kwa upande wangu ni bora ni teseke kwa hali yeyote ile nipambane kwa namna yeyote na ikitokea nikafa basi nife mwenyewe kuliko kufa na kukiacha kizazi changu kiendelee na mambo kama haya ya kwangu,.

Pole Sana Mkuu.
Ila angalau watoto wawili. Sio mbaya.
Kama una kipato cha Kati basi watoto wanne.
 
Mimi hawa wawili wanatosha, kuna jamaa mmoja hivi anao wanne, hana shamba, kapanga nyumba, mke wake ni house wife, unene sio afya lakini jamaa hata kamwili kuja hakuna na yuko kazini tena serikalini zaidi ya miaka kumi, ameajiriwa ndio lakini ajira mbuzi ndio maana ana mahasira muda wote na anahangaika na maushirikina ili apate ubosi wakati Hana connection
 
Mimi hawa wawili wanatosha ,Kuna jamaa mmoja hivi anao wanne, hana shamba , kapanga nyumba, mke wake ni house wife, unene sio afya lakini jamaa hata kamwili kuja hakuna , ameajiriwa ndio lakini ajira mbuzi ndio maana ana mahasira muda wote na anahangaika na maushirikina ili apate ubosi wakati Hana connection

Noma Sana hiyo.

Unazaa cheap labour,
 
Pole Sana Mkuu.
Ila angalau watoto wawili. Sio mbaya.
Kama unakipato cha Kati basi watoto wanne.
Tatizo linakuja kwa hao hao wawili, je akitokea mmoja akawa shoga? Wewe hauoni tatizo lake litakuwa limesababishwa na ujinga wangu?

Ni pia nina imani hata nikizaa mmoja sitakuwa na plan ya kumfanya huyo huyo mmoja kuja kuwa simba atakayeongoza kundi la ng'ombe msituni.

Bado atakuwa maskini na mwenye magonjwa kibao
 
Tatizo linakuja kwa hao hao wawili, je akitokea mmoja akawa shoga? Wewe hauoni tatizo lake litakuwa limesababishwa na ujinga wangu?
Ni pia nina imani hata nikizaa mmoja sitakuwa na plan ya kumfanya huyo huyo mmoja kuja kuwa simba atakayeongoza kundi la ng'ombe msituni.
Bado atakuwa maskini na mwenye magonjwa kibao

Kwangu akiwa shoga nitamuua.
Ingawaje itanisikitisha Sana
 
Sio tu kuzaa watoto wengi mimi kwangu hata kuzaa kwenyewe tu sitamani,.
Dunia na ulimwengu wa sasa sio salama tena kwa binadamu sanasana watoto sanasana watoto wa kike na wakiume,.
Mimi kwa upande wangu ni bora ni teseke kwa hali yeyote ile nipambane kwa namna yeyote na ikitokea nikafa basi nife mwenyewe kuliko kufa na kukiacha kizazi changu kiendelee na mambo kama haya ya kwangu,.

Sanasana watoto wa kike na kiume..... watoto wengine ni wapi Boss ?
 
Back
Top Bottom