Zaidi ya KM 2000 za barabara kuanza kujengwa kwa mtindo wa EPC +F. Serikali yasema hazitalipiwa Tozo

Zaidi ya KM 2000 za barabara kuanza kujengwa kwa mtindo wa EPC +F. Serikali yasema hazitalipiwa Tozo

Mimi ninajua nataka wewe hapo unieleze Ufisadi uko wapi Ili tufanye wote analysis,si umejenga hoja wewe au?

3.8 trilion/ 2035kms = * Tsh per Km
Ujaona ufisadi hapo bado?

Wakati one km almost 1 bilion hapo huoni kiwango ni kikubwa mno kuliko 1 bilion ukigawanya mkuu?
 
3.8 trilion/ 2035kms = * Tsh per Km
Ujaona ufisadi hspo bado?

Waksti one km almost 1 bilion hapo huoni kiwangi ni kikubwa kuliko 1 bilion ukigawanya mkuu?
Kwanza unajua bei ya kutengeneza km 1 ya lami ya asphalt au double surface dressing? Pili unajua factos zinazoamua bei?

Hapa chini ni km 25 Kwa bil.45 ,haya nambie hii ni EPC?
 
Kwanza unajua bei ya kutengeneza km 1 ya lami ya asphalt au double surface dressing? Pili unajua factos zinazoamua bei?

Hapa chini ni km 25 Kwa bil.45 ,haya nambie hii ni EPC?
Beijing ni hao hao, unataka kuniambia kuwa umetoa mfano unaofanana au unaoweza kujibu swali langu?
Kms 179 kwa 45 bilioni ni single project,

je kwa Trilion 3.8 kwa kms 2035 huoni ni mradi mkubwa ambao 10% ya mradi huo ingerudi kwenye jamii umaskin ungepungua?

Kwa haraka haraka km moja inakaribia 2 bilions 😳
 
Beijing ni hao hao, unataka kuniambia kuwa umetoa mfano unaofanana au unaoweza kujibu swali langu?
Kms 179 kwa 45 bilioni ni single project,

je kwa Trilion 3.8 kwa kms 2035 huoni ni mradi mkubwa ambao 10% ya mradi huo ingerudi kwenye jamii umaskin ungepungua?

Kwa haraka haraka km moja inakaribia 2 bilions 😳
Nikupe Chico wanaojenga Km 60.za Mbeya? Gharama Kwa km 1 ni bil.2.3 ,una hoja nyingine?

Kama hujui kaa kimya,Nyie ndio kina Mpina waganga wa kienyeji
 
Nikupe Chico wanaojenga Km 60.za Mbeya? Gharama Kwa km 1 ni bil.2.3 ,una hoja nyingine?

Kama hujui kaa kimya,Nyie ndio kina Mpina waganga wa kienyeji
 
Umeishiwa 😁😁😁😁
Nimecheka 🤣🤣🤣🤣
 
Kwa mara ya Kwanza baada ya Uhuru Tanzania imepata Rais Samia apewe maua yake.

Serikali ya Rais Samia imeandika Historia nyingine ya ubunifu kwa kusaini kuanza ujenzi wa barabara za kuu za lami kwenye mikoa 13 kwa pamoja zenye jumla ya urefu wa KM 2035 kwa mtindo wa EPC+ F (Engineering, Procurement, Construction and Finance) kwa gharama ya Tsh.Tilioni 3.8 ambapo miradi inatarajiwa Kukamilika ndani ya miaka 4 (2023-2027).


Akizungumza wakati wa kushuhudia kutiwa saini kwa mikataba hiyo Jijini Dodoma, Waziri wa Ujenzi Prof. Mbarawa amesema kwamba, barabara hizo hazitokuwa za kulipia tozo kama wapotoshaji wanavyosema. Ikumbukwe hii haijawahi tokea toka Uhuru, walinda legacy mnafundishwa kazi.

My Take
Samia anawaonesha kwamba Private Sector inalipa kuliko Ujamaa mbuzi ambao baadhi ya watu wasiojielewa wanakumbatia.

Ndio maana hata kwenye Bandari anataka awafundishe namna ya kutumia rasilimali kwa manufaa ya watu badala ya kuhubiri propaganda za Uzalendo mbuzi na umaskini over years.

Hongera sana Mh. Rais, na Waziri wa Mbarawa Kwa Ubunifu,Historia itaandika jina lako kwa wino Mwekundu.

=====

MIRADI YA BARABARA ILIYOSAINIWA KWA UTARATIBU WA EPC + F

i) Barabara ya Kidatu – Ifakara – Lupiro – Malinyi – Kilosa Kwa Mpepo – Londo – Lumecha/Songea (km 435.8) inapita katika mikoa ya Morogoro na Ruvuma na inapita pia katika Majimbo ya Kilombelo, Ulanga, Malinyi na Namtumbo;

ii) Barabara ya Arusha – Kibaya – Kongwa (km 453.42) inapita katika Mikoa ya Arusha, Manyara na Dodoma na inapita katika Majimbo ya Arusha Mjini, Arumeru Magharibi, Simanjiro, Kiteto na Kongwa;

iii) Barabara ya Handeni – Kiberashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboroti – Mrijo Chini – Dalai – Bicha – Chambolo – Chemba – Kwa Mtoro – Singida (km 384.33) inapita katika Mikoa ya Tanga, Manyara, Dodoma na Singida na inapita katika Majimbo ya Kilindi, Chemba, Kiteto, Singida Mashariki na Iramba Mashariki;

iv) Barabara ya Igawa – Songwe – Tunduma (njia nne) (km 237.9) inapita katika Mikoa ya Mbeya na Songwe na inapita katika Majimbo ya Mbarali, Mbeya Vijijini, Mbeya Mjini, Mbozi, Vwawa na Tunduma;

v) Barabara ya Masasi – Nachingwea – Liwale (km 175) inapita katika Mikoa ya Lindi na Mtwara na inapita katika Majimbo ya Masasi, Nachingwea na Liwale;

vi) Barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago – Maswa (km 339) inapita katika Mikoa ya Manyara, Simiyu, Singida na Arusha na inapita katika Majimbo ya Mbulu Mjini, Mbulu Vijijini, Karatu, Iramba Mashariki, Meatu, Maswa Mashariki na Kisesa; na

vii) Barabara ya Mafinga – Mtwango – Mgololo (km 81) inapita katika Mkoa wa Iringa na inapita katika Majimbo ya Mufindi Kusini na Mafinga.

Unajua sijafahamu unachosifia hapo kwamba wachina wanajenga bure hawatalipwa au kitu gani kinatofautiana na Marais waliopita, Ni ujinga TU unakusumbua ujamaa mbaya Hao wanaokujengea Ni wajamaa na iyo kampuni Ni ya serikali, Kuna baadhi ya vitu upaswi kuichia sekta binafsi full labda Shea.
 
Unajua sijafahamu unachosifia hapo kwamba wachina wanajenga bure hawatalipwa au kitu gani kinatofautiana na Marais waliopita, Ni ujinga TU unakusumbua ujamaa mbaya Hao wanaokujengea Ni wajamaa na iyo kampuni Ni ya serikali, Kuna baadhi ya vitu upaswi kuichia sekta binafsi full labda Shea.
Rudia kusoma.utaelewa
 
Tatizo la wanaojiita wasomi ndio wametufikisha hapa tulipo.
Hakuna kigezo cha kujenga barabara ya lami kwa kila km moja 2 bilion.
Ndio yale yale ya SGR
We Jamaa bwana unasikitisha sana,kwanza gharama zilibadilika Toka 2019 COVID ilivyoanza ,kabla ya hapo kujenga Barabara ya lami ilikuwa kati ya 1.2-1.8bln kutegemeana na aina ya lami ,Sasa hivi inacheza kati ya 1.8-2.5 kutegemeana na aina ya lami na nature of terrains,harafu Teknolojia imekuwa saizi tunajenga super pave na asphalt zaidi kuliko surface dressing
 
Kiongozi usipojua hesabu kila kitu utapigwa tu.
Na kwa mwendo uliopo kila kitu tunapigwa
Aliyekuwa anajua hesabu ni nani nikuletee hesabu zake Ili uniambie kama tumepigwa au hatukuoigwa tena nitakuletea Barabara ya Mpemba Isongole.
 
We Jamaa bwana unasikitisha sana,kwanza gharama zilibadilika Toka 2019 COVID ilivyoanza ,kabla ya hapo kujenga Barabara ya lami ilikuwa kati ya 1.2-1.8bln kutegemeana na aina ya lami ,Sasa hivi inacheza kati ya 1.8-2.5 kutegemeana na aina ya lami na nature of terrains,harafu Teknolojia imekuwa saizi tunajenga super pave na asphalt zaidi kuliko surface dressing
Haya unayasema wewe, ila leo siku ya kusainiwa mikataba Professor Mbarawa , alikuwa anasimulia mambo ya Mh Mpina.
Sijawahi kusikia JPM akitaja figure ulizo xisema bali nimezisikia kwako kipindi cha awamu ya 6.
 
Napongeza hii initiative ya Serikali
Japo yatupasa kuwa makini na gharama Za wakandarasi kutokuwa kubwa kuliko bei ya soko.

Pili lazima reinforcements ya quality monitoring iwe na uwezo pia mamlaka ya kuhakikisha barabara zetu zinakuwa na ubora stahili (Value for Money).

Tatu,Nchi yetu tayari Ina undertake turnkey mega infrastructure projects (SGR,Stigler,BRT,Etc)..Kimsingi uchumi wetu umeelemewa sana..Hatukupaswa kuharakisha kusign mikataba ya kandarasi zote Kwa wakati mmoja..EPC+F ni mkopo (Mkandarasi anajenga mradi Kwa kukopa Kwa niaba ya serikali in which sense tukilipa tunalipa na riba zote involved na zaidi sana tukichelewa kulipa kuna penalties..

Nchi yetu bado ni Changa,Hatupaswi kuwa na haraka sana ktk ujenzi wa miradi ambayo ROI si ya muda mfupi..Modalities Za EPC+F makampuni yanakopa kwenye commercial banks (Local or International)..Kuna riba..

Nadhani tuendako kwenye infrastructure projects tuangalie uwezekano wa ku implement EPC+F yenye BOT Modalities (Build,Operate and Transfer) hivyo contractor anakuwa na perspective ya kibiashara pia hivyo Hawezi ku overcharge au kujenga mradi chini ya kiwango.

Nne,Miradi yote tajwa inajengwa kwenye ukanda wa madini ya thamani kubwa (Vito na Rare Earth Metals)..Wachina wanajua nini Tuko nacho chini ya ardhi kupitia espionage satellite zao hivyo haya makampuni mengi makubwa ni State Owned or affiliated (SOE) hivyo yana mission zaidi ya ujenzi wa barabara (Ktk Hili nashauri vyombo vyetu vya usalama kufuatilia hili na kuwezeshwa ili kuziba mianya mikubwa ya utoroshaji na uvunaji wa rasilimali Za nchi..

Mwisho,Utekelezaji wa mipango ya maendeleo iende sambamba na ujenzi wa mifumo ya uzalishaji mkubwa (Kilimo,Ufugaji,Viwanda) ili kunenepesha uchumi na kuwezesha serikali kulipa madeni makubwa yatokanayo na mikopo toka Bank Ya Dunia,Benki ya maendeleo ya Afrika n.k.
 
Back
Top Bottom