Zaka ya 10% unatoa kwenye faida au kwenye utajiri wako?

Zaka ya 10% unatoa kwenye faida au kwenye utajiri wako?

Mimi naijua injili ya kweli ndiyo maana.... siyo hii ya mungu mwenye nafsi 3 wala Yesu wa dhambi ya asili ....siku nikiamua kuleta uzi wa dini waislamu na wakristo watapoteana .. siku za nyuma kuna jqmaa alileta uzi wa 666 ...ule uzi nilitoa fafanuzi hadi mwenye uzi aliukimbia watu wakawa wanangoja awaletee maelezo ya 666 jamaa alishindwa kutokana na fafanuzi niliyo toa nilieleza 666 ni nini ...wapumbavu wa makanisani wanadanganyani mambo mengi
Injili ya kweli ni ipi?
 
Hekalu ni moja tu ...kama ujui kwanini jiulize kwanini daudi alikataliwa kujenga hekalu ...kanisa na sinagogi anajenga mtu yoyote ila hekalu lilikuwa ni moja milele daima kasome upya maandiko utajua kuwa hekalu siyo sawa na sinagogi .....fungu la kumi lilikuwa ni kwa ajili ya hekalu.
Hujajibu swali....

Nimeuliza tofauti ya hekalu na kanisa ni nini ?
 
Kwa maagixo ya nani? Na una uthibitisho wowote unachosema?
Je kuna chochote kinaweza kuonyesha ulichosema m?
1 Wakorintho 9:13-14
[13]Hamjui ya kuwa wale wazifanyao kazi za hekaluni hula katika vitu vya hekalu, na wale waihudumiao madhabahu huwa na fungu lao katika vitu vya madhabahu?
[14]Na Bwana vivyo hivyo ameamuru kwamba wale waihubirio Injili wapate riziki kwa hiyo Injili.
Mungu wa Agano la Kale ni yuleyule wa Agano Jipya.
 
...kanisa na sinagogi anajenga mtu yoyote ila hekalu lilikuwa ni moja milele daima kasome upya
In maana mpaka karne hii hekalu ni moja tu ?
maandiko utajua kuwa hekalu siyo sawa na sinagogi .....fungu la kumi lilikuwa ni kwa ajili ya hekalu.
Kwani ibada za hekaluni na kwenye sinagogi zina tofauti gani ?
 
Hekalu ni Jengo na Kanisa ni mwili wa Kristo
Kanisa ni mwili wa Kristo maana yake ni sawa na kusema Kanisa ndiye Kristo.

Kama Kichwa kinavyokuwa na mwili ili mtu akamilike.

Hivyo Kristo ni Kichwa na kanisa ni mwili ili Kristo akamilike.

Ndio maana mtu anapookoka na kumpokea Kristo, Kristo ndiye anayeishi ndani yake kupitia roho wake.

Hata sehemu/jengo tunalokutanika kufanya ibada kwenye ulimwengu wa mwili ni Kanisa pia, hivyo fungu la kumi ni sahihi kabisa kupeleka kanisani.

Rejea kanisa la mwanzo, wale waliouza mali zao walipeleka fedha zao Kanisani.

Matendo ya mitume 4:34-35
 
Habari. Assume wewe ni mfugaji wa Kiebrania. Umepewa urithi wa ng'ombe 100 na baba yako. Ndani ya mwaka wakazaliwa ngombe 20. Ukawa na ng'ombe 120. Wakati wa kutoa zaka unefika.

Je utatoa ng'ombe wawili kama asilimia kumi ya ng'ombe ishirini walioongezeka au utatoa ng'ombe 12 kama asimilia kumi ya ng'ombe 120 ulionao? Vipi mwaka huo upate majanga na kubakiwa na ng'ombe 80. Utatoa zaka kiasi gani?
Utatia ng'ombe 10
 
1 Wakorintho 9:13-14
[13]Hamjui ya kuwa wale wazifanyao kazi za hekaluni hula katika vitu vya hekalu, na wale waihudumiao madhabahu huwa na fungu lao katika vitu vya madhabahu?
[14]Na Bwana vivyo hivyo ameamuru kwamba wale waihubirio Injili wapate riziki kwa hiyo Injili.
Mungu wa Agano la Kale ni yuleyule wa Agano Jipya.
Unazijua kazi za hekaluni zilizofanywa na watu wa hekalu...
Kazi kubwa ilikuwa ni kufanya ukuhani hivyo walikuwa hawana kazi nyingine zaidi ya hiyo ilikuwa ni 24/7 wanashinda kwenye madhabahu...

Kuhusu hilo fungu la kumi Ni kweli uko sahihi kwa 100% wapate riziki kwa hiyo injili kwa njia ya sadaka na sio zaka...

Na jinsi sahihi ya kupata pesa Kasome jinsi injili ilivyoendeshwa (Matendo ya mitume 4:32-37)
Na haukuwa zaka...

Ndo maana mwanzoni nikasema watu hamjui maana ya zaka na inatolewaje na iliacha kuwepo lini na hasa ilikuwa na msingi upi..

Wewe umethibitisha hicho kuwa hujui maana ya Sadaka,Matoleo,malimbuko na zaka...
 
je mfanya kazi mwenye mshahara ya 1m kwa mwezi atatoa 100k au atasubir kwanza akate gharama zote alizoingia katika kufanya io kazi mfano nauli kwenda ofisini, chakula akiwa ofisin nk atoe asilimia 10 ya bakaa itayobaki? naomba unijibu mkuu
Ile net inayoingia kwenye account baada ya makato Mimi hua nafanya ivo
 
Unazijua kazi za hekaluni zilizofanywa na watu wa hekalu...
Kazi kubwa ilikuwa ni kufanya ukuhani hivyo walikuwa hawana kazi nyingine zaidi ya hiyo ilikuwa ni 24/7 wanashinda kwenye madhabahu...
Kwenye desturi za kale za Kiyahudi kazi za hekaluni zilifanywa zaidi na kuhani mkuu ambaye aliingia patakatifu pa patakatifu mara moja kwa mwaka.

Ila baada kifo cha Kristo kilichozaa agano jipya na kanisa, wale wote waliomkiri Kristo wanaweza kupaingia patakatifu pa patakatifu.
Ndo maana mwanzoni nikasema watu hamjui maana ya zaka na inatolewaje na iliacha kuwepo lini na hasa ilikuwa na msingi upi..
Tupe andiko kwamba Zaka iliacha kuwepo lini?....

Rabbon Mfalme Sulemani
 
Break even ni faida au hasara Mkuu.. hii terminology ya kiuchumi huwa naikoroga
Break even ni Ile point ambayo faida ni zero Yani kama ni biashara umeuza Yale mapato ukatoa matumiz mfano gharama za umeme,maji wafanyakaz...ukajikuta ela yote umeishia kulipa izo gharama ukabaki na nothing...hiyo Ndo break even
 
Kwenye desturi za kale za Kiyahudi kazi za hekaluni zilifanywa zaidi na kuhani mkuu ambaye aliingia patakatifu pa patakatifu mara moja kwa mwaka.

Ila baada kifo cha Kristo kilichozaa agano jipya na kanisa, wale wote waliomkiri Kristo wanaweza kupaingia patakatifu pa patakatifu.
Umeanza vizuri ila umemaliza vibaya..
Kulikuwa na kuhani mkuu na makuhani wengine wa lawi waliokuwa katika malango...
kwa ajili ya sadaka ya utakaso na sadaka zingine...

kuhani aliyeingia patakatifu kwa mujibu wa biblia ni Yesu peke yake ndiyo ana act kama mpatanishi (Ambayo ilikuwa kazi ya kuhani kipindi hicho)

Kasome waebrania tena inamfananisha Yesu na Mfano wa Melkizedek Kuhani wa Milele..

Tupe andiko kwamba Zaka iliacha kuwepo lini?....

Rabbon Mfalme Sulemani
Kasome kitabu cha Waebrania....
Kama kulikomeshwa huduma za kikuhani na Huduma za sadaka ya utakasaji na patakatifu (Ndizo zilizompa Authentification mlawi kupokea zaka)..
Sasa kama kazi zimekoma unategemea mshahara utakuwepoo..

Nikuulize Swali kama hakuna Wagonjwa Kuna haja gani ya kuwa na Madaktari?

Kama hakuna Wanaokufa kuna haja gani ya kuwa na majeneza?

Kama hakuna Wanaosafiri kuna haja gani ya Usafiri?

Angalia hapa chini mafungu kadhaa..
Screenshot_20231130_201238_Biblia Takatifu.jpg

Screenshot_20231130_200921_Biblia Takatifu.jpg


Hakikisha mkuu unasoma sana kabla ya kuchangia hoja
 
Kwa sheria za kiebrania sijui kwa kweli
Nitakuja kuelezea zaka kiislam, nani anapaswa kutoa na nani sheria haimbani. Yupi atoe na kwa kiwango gani.
 
Kwa sheria za kiebrania sijui kwa kweli
Nitakuja kuelezea zaka kiislam, nani anapaswa kutoa na nani sheria haimbani. Yupi atoe na kwa kiwango gani.
Angalau sheria za kiislam zilo fair kiasi fulan..
Huwezi kumdai Zaka Maskini na Mjane...
 
Kwenye desturi za kale za Kiyahudi kazi za hekaluni zilifanywa zaidi na kuhani mkuu ambaye aliingia patakatifu pa patakatifu mara moja kwa mwaka.

Ila baada kifo cha Kristo kilichozaa agano jipya na kanisa, wale wote waliomkiri Kristo wanaweza kupaingia patakatifu pa patakatifu.

Tupe andiko kwamba Zaka iliacha kuwepo lini?....

Rabbon Mfalme Sulemani
Ndugu Proved usibishane na watu wasioamini uwepo wa Roho MTAKATIFU,

Aliye na Roho mtakatifu anajulishwa yote,

Sadaka na ZAKA haijawahi kukatazwa, zaidi sana sadaka na ZAKA imeongezeka Kutoka 10 % Hadi 100% wakati mwingine, itategemea Roho mtakatifu amekusemeshaje Kwa habari ya Kutoa.

Tumeona zakayo aliposamehewa dhambi na YESU, ametoa nusu ya Mali zake zote na alikuwa tajiri, mfano mtu mwenye utajiri wa BL 100 atoe 50%zaka, huoni hiyo ni kubwa sana zaidi ya ZAKA ya kawaida?

Mama mjane akatoa senti chache alizokuanazo ambapo alotoa Kila kitu alochokuwa nacho 100%.

Hanania na Saphira, waliuza shamba na wakaadhimia kwenda Kutoa pesa yote ya kuuza shamba miguuni pa mitume Kwa ajili ya INJILI.

In short, ukiongozwa na Roho mtakatifu, huwezi kuuliza mara mbili kuhusu Kutoa Kwa ajili ya INJILI.

Yeyote anayekwambia Usitoe ZAKA na sadaka kwamba ni AGANO jipya ni Roho ya mpinga kristo inawaongoza hao.

INJILI itahubiriwa vipi watu tusipotoa sadaka na ZAKA? Watumishi watakula nini nk nk!!

Mungu akubariki.
 
Kama ingekuwa kanisa ndio serikali basi ingekuwa halali wao kupokea hilo fungu la 10. Yaani wapokee fungu la 10 burebure tu bila kutoa huduma stahiki . Sadaka zinawatosha
Bora kwa waislam zaka ni kwa ajili ya wasiojiweza tena unaweza mpa ndugu yako asiyejiweza zaka yako
 
Back
Top Bottom