Zama za Kilimanjaro Express zimeisha

Zama za Kilimanjaro Express zimeisha

Hiyo kampuni hata kama hapo katikati ilikuwa inatoa huduma nzuri, niseme tu kwa sasa hiyo huduma wanayotoa sasa hivi ndio level zao. Kwa sie wahenga tuliosafiri mwanzoni mwa miaka ya 2000 tulikuwa tunaikwepa maana mnaweza kuishiwa mafuta njiani....enzi hizo kampuni ilikuwa inajulikana kama Kilimanjaro trucks au Sawaya

N.B. kama taarifa ya kweli lakini maana kwa gari za Arusha kwa Kilimanjaro Express sio mbaya sana
Hii taarifa wala haihitaji akili nyingi kuitambua kama propaganda kwa mtu mzoefu, jamaa anakwambia kilimanjaro ilijaza mpaka watu wakakosa nafasi 🤣🤣🤣. Wakati mwengine tunapopandaga hayo mabasi kwenye msimu kama huu mnaweza kujikuta kwenye gari hamzidi hata abiria 30
 
Sijapinga mkuu, hayo magari nayafahamu tangu Air Msae na Dar Express wanashika hiyo njia ya Arusha, ilikuwa kampuni ya ovyo, mengine yalikuwa yanatumia Sawaya na mengine yalikuwa yanatumia Kilimanjaro truck. Kuna kipindi alifanya mageuzi ndio akaja na jina la Kilimanjaro Express akawa akajenga jina kutokana na kizazi cha sasa.

Nimetumia neno kama taarifa ni ya kweli (sijamaanisha ni ya uongo) ila kwa kuwa sijapita hiyo njia kwa kutokea Dar kwa muda sana na ndio maana nikasema huduma wanayotoa sasa hivi ndio level yao (means wamerudi enzi zile za longo longo)
Hapana Mkuu, Sija-dispute taarifa yako bali ya mleta mada. KLM of course ina changamoto nyingi, lakini mleta mada kwa kiasi ameongeza na yake pia, Swala la baadhi ya mabasi ya zamani kuwa mabovu ni kweli kabisa, lakini mengine hajawa balanced
 
Hapana Mkuu, Sija-dispute taarifa yako bali ya mleta mada. KLM of course ina changamoto nyingi, lakini mleta mada kwa kiasi ameongeza na yake pia, Swala la baadhi ya mabasi ya zamani kuwa mabovu ni kweli kabisa, lakini mengine hajawa balanced
Okay mkuu
 
Hakuna cha Klm, Bm wala Marangu huduma za ndani hovyo tu.
Wahudumu wazuri ni wachache mno bali wapo mmoja mmoja wanaojielewa wengi wao hamna kitu
Unaijua Extra luxury wewe?[emoji3]
 
Magari Luxury yalivyo mengi namna hiyo...

Kilimanjaro hapana aisee...Na magari yao mengi AC ni tatizo..
 
Wahudumu wa mabasi nilikutana nao huko kusini buana, Njombe- Songea huko Superfeo hadi unatamani safari isifike mwisho!
Na ukizingatia ile ruti katawala yeye tu yaani gari zake zinapishana tt kutwa nzima, angekuwa mwingine angeutumia huo mwanya kuwa na huduma za hovyo.
 
Kumbe bado yapo!! Mara ya mwisho nililipanda mwaka juzi nikaapa kutokulipanda tenaaa. Washafilisika hao, hamna kitu tena!
 
Hii taarifa wala haihitaji akili nyingi kuitambua kama propaganda kwa mtu mzoefu, jamaa anakwambia kilimanjaro ilijaza mpaka watu wakakosa nafasi 🤣🤣🤣. Wakati mwengine tunapopandaga hayo mabasi kwenye msimu kama huu mnaweza kujikuta kwenye gari hamzidi hata abiria 30
Mkuu,kwa nini niwasingizie ilihali sina chochote ninachofaidika nacho?nimesafiri siku ya tatehe 7/07/2022 na gari ya saa 12:30 dereva wa gari alikua jamaa mmoja nilisikia wakiwa wanamuita mkiboshoo.
 
Wapo hovyo sio uongo...
Hayo luxury nilipanda siku moja walisema iko na choo ndani kumbe ni haja ndogo tu...sasa kuna mwanamke mmoja akafanya kubwa badala ya ndogo Aisee gari zima ilinuka safari ilikuwa chungu sana na watu walikuwa wanalalamika mno
Huyo mama alipaswa apewe kazi ya kubeba pupu yake,vyoo vyote ni haja ndogo tu na vimeandikwa
 
Bro uko sahihi kabisa, yaani tangu yule Mama aliyekuwa Mkurugenzi afariki huduma za KLM Express zimedorora hata Bus unaloambiwa ni luxury halina hadhi kabisa, mimi mwenyewe yalinikuta kama wewe nilitoka Dar - Arusha kwa kweli niliona huduma ziko tofauti na KLM Express niliyokuwa nasafiri nayo miaka ya nyuma, na tulikariri hakuna zaidi ya KLM Express, lakini hivi karibuni totally mambo yamebadilika Mabasi yamechoka mno, ilibidi wakati narejea Dar nisafiri na EXTRA luxury coach at list lilikuwa linakidhi. Uongozi wa KLM Express ufanyie kazi malalamiko ya wateja na waboreshe huduma zao kama mwanzo naamini watarudi kwani sasa hivi biashara ni ubunifu na ushindani.
Umechanganya mambo,dar express ndio alifiwa na mke sio KLM
 
Back
Top Bottom