Kim Jong Jr
JF-Expert Member
- Mar 15, 2014
- 11,074
- 20,608
Baba akikutana na kimada hachelewi kuwapiga chini. Mama ni mama tu. Mama hamtupi mwanae. True love iko kwa mama.Mbona baba humsemi?
Hakika mkuuBaba akikutana na kimada hachelewi kuwapiga chini. Mama ni mama tu. Mama hamtupi mwanae. True love iko kwa mama.
Kuna kipindi unapitia magum kila mtu humuoni ila mama Yuko nawe kwa upendo na moyo wote. Japo hata baba wa dizaini hiyo wapo ila mama ni zaidi.
I love all Mama out there...
Lakini ukifa watakuzika tu utake usitake na watoto wako watatunzwa na wao.
Mfu hahisi kitu kamwe, hata wakisusa wakaacha ujiozee barabarani haina impact kwa marehemuNgoja ndugu zako waje kususia maiti yako ukajizike na pesa zako ndipo utajua umuhimu wa ndugu!
Mwaka 2017 nilipata mushkeri kwenye kibarua changu, watu waliokuwa na Mimi ni mama na dada yangu pamoja na girlfriend wangu.Hakika mkuu
Mama ana upendo wa kweli
Kupitia andiko lako hili nimejifunza kituMwaka 2017 nilipata mushkeri kwenye kibarua changu, watu waliokuwa na Mimi ni mama na dada yangu pamoja na girlfriend wangu.
Wengine wote waliishia kuwa wananipigia simu na kusema hivi hela ulikuwa unazifanyia nini Hadi unaishi maisha ya shida. Nilikuwa naumia sana. Unakumbuka si Hawa kila mwisho wa mwezi ulikuwa unatuma hela kwao hupati jibu. Harusi zao na misiba yote ulikuwa unapigiwa simu utoe hela kiasi tofauti na wachangiaji wa kawaida. Ila ukiyumba wanasema eti hela ulikuwa unapeleka wapi na kashifa kibao.
Ila Mama alibaki na true love , She was and still a comforter of all time. Maza unampa Buku ten analia Hadi machozi kwa furaha ila hao ndugu wengine unawapa 20,000 wanasema haitoshi na kukuongelea ushenzi.
Nilichojifunza baki na ndugu zako na wa kwanza awe mama. Hao wengine Piga mstari kabisa toa pale unapoona inafaa kutoa msaada.
Kingine kwa ndugu saidia watoto acha kusaidia majitu mazima. Kama Kuna mtoto anaumwa saidia. Kama mtoto anahitaji ada saidia pale unapoweza.
Mimi mjomba wangu alikuwa na hii principal kasaidia waroto ukoo mzima Hadi tumefika vyuo. Ametengeneza kizazi tunampenda sana maaana tulikuwa tunaona anavyotusaidia hata Kama unahitaji Ada ya milion unapewa. Na alikuwa na muhasibu wake kabisa wa kusimamia hayo mahesabu ya ndugu.
Na ndugu zake wakubwa aliwaambia hamtakuja kula hela yangu maana hamna shukran ila nitawasaidia watoto wenu ambao ni malaika. Huwezi amin mpaka Sasa Nina kumbukumbu za nilivyokuwa darasa la kwanza mjomba anatuma watu walete hela nyumbani mimi niende shule. Mpaka nafika chuo.
Watanzania wengi ndivyo tulivyo, majungu na roho mbayaSafi momy ale..za masiku...nakumiss.hivi sijui kwanini inakua hivi? Ila Kuna rafiki yangu kwao wako 5! Wanasaidiana Sana...Yani hakuna kukopa nje .wanakopana wenyewe na kupigana tafu balaa! Sijui wengine inakuwa ishu
Hatari sana mzee.Kitu kigumu sana kwenye haya maisha ya kijamaa, ni wewe ndo uwe mtu wa kwanza kufanikiwa kwenye familia au ukoo wenu.
Aisee, acha niishie hapa!
Kabisa kabisa mkuu,daahNanukuu..."mpaka sasa kwa umri huo hana hata nyumba, hana maendeleo yoyote yupo yupo tuu anazurura mjini"
Wakasahau kwamba Mwamba kila akikusanya akiba inaishia kusomesha na kuwatibia hao hao ndugu wanaosema hafanyi maenedeleo...
Asipo wasaidia wanamuita moaka kwenye vikao vya ukoo, akiwasaidia wanamcheka kisa hafanyi maendeleo...
Ndugu tuna maudhi mengi sana..
Kabisa mkuu mi mshua alikufa ndo nipo seven then nikamaliza shule nikafail kuingia sekondari nakumbuka kulikuwa na msiba wa bibi yangu mzaa baba sasa kwenye vikundi vyake wakawa wametoa rambi rambi kama milioni tatu huwezi amini nilipoomba kupelekwa shule baba yangu mkubwa alinambia siwezi kusoma mi mi muhuni nililia sana akatokea mdhamini rafiki yake na baba akanipeleka shule nilisoma kwa hasira nyingi na kufika chuo saivi wanabaki wanaona aibu tu na wote waliokuwa na pesa wamefirisika watoto wao hawaishi kunipiga vizinga kuna time mpaka nasema sijui nisiwasaidie ila naona wao hawana makosaHuku kutunziana watoto sina imani nako sana miaka hii
Usitegemee ndugu upande wa baba wakusomeshee, wataishia kugawana mali kama mbweha wanavyogawana swala, nimeshaona hii kwa wengi, sijui wana nini hawa, ila wajomba ni nadra kukutupaaaNdugu miyeyusho sana..mi wazazi wamefariki nipo std 4, hakuna hata ndugu aliyejishughulisha na mimi, nilivyosoma na kukua Mungu mwenyewe anajua..
Leo maisha yana afadhali ndo wanaanza kuibuka, mi huwa nawachora tu..
Uliloandika Ni kweli ndugu wa mume watakupenda kaka yao akiwa hai siku akiondoka duniani ndio wa kwanza kukimbilia Mali, ujombani ndio hulea watoto wa dada zao bila shida Kama mtoto wa familia. Shikamooni wajomba woteUsitegemee ndugu upande wa baba wakusomeshee, wataishia kugawana mali kama mbweha wanavyogawana swala, nimeshaona hii kwa wengi, sijui wana nini hawa, ila wajomba ni nadra kukutupaaa
Tatizo la watu wanaosaidia wanataka gratification. Hapo ndipo mateso yenu yanapoanzia...Muda mwingine kutumia hekima kwenye changamoto hizi za kifamilia ni kujimaliza mwenyewe, unaonesha upendo kwa watu ambao wao hawana upendo na wewe. Wanakuchekea kinafiki ukiwapa msaada, wakitoka wanapanga mipango ya kukudhuru na kukuombea uharibikiwe.
Binadamu wana Roho mbaya sana, hata Yesu hakuwa na kosa lakini walimsulubu msalabani japo aliwapa chakula wakiwa hoi na njaa walivokula na kushiba wakaanza kumtesa. Wanaonesha kukupenda lakini mioyo yao imejawa chuki. Naandika haya nikiwa na Jazba siku kadhaa zilizopita ningekuwa niko karibu na viumbe hawa waliofanya niandike hapa basi leo maiti kadhaa zingekuwa mochwari au zishazikwa na mimi ningekuwa nyuma ya nondo.
Ndugu zangu kwa sasa ni ndugu wa damu tu wadogo zangu na mama zangu. Hawa wanaojiita ndugu za baba huu ushenzi wanaoniletea kwenye familia yangu na mimi binafsi pamoja na kujishusha sana kwao Imefika mahali imetosha, naona ni kama nakumbatia kundi la wachawi huku nikijifanya nawapenda. Huku wao wakiwa na mipango yao binafsi.
Nimesaidia sana kifedha na kila aina ya msaada lakini hawa watu nia yao sio njema Lakini majibu niliyowapa nadhani washanifahamu kwamba mimi sasa ni mtu wa namna gani, siwezi kukumbatia nyoka tena.
Nilipofikia ukinipiga kofi, nakurushia bomu huu upuuzi wa kumuachia Mungu aamue sina tena. Tutajibu dhambi zetu tukiwa kwenye kiti cha enzi.
Maweeeeeee, kuzikwa utazikwa tu kwakua wataogopa utanuka, lakini swala la watoto kusaidiwa kajipange upya...Lakini ukifa watakuzika tu utake usitake na watoto wako watatunzwa na wao.