Ule mchezo wa kukaa barabarani then kila gari linalopita mnashindana kwa kusema hili langu nyie hamjaupitia? Mimi nilikuwa naibuka kidedea kila siku! Amakweli utoto mzigo!
hahaha kweli ujinga huu! Mie nilijua yale maroli scania 113 huwa yanaendeshwa na watu wenye nguvu sana zaidi ya baunsa. Kumbe hata katoto tu kanaweza kuendesha Donn ngoja niite my waifu wangu aje anione nilivyokuwa mjinga. Diaa! Diaa Evelyn Salt njoo huku once.
Mimi nilikuwa nafikili mtu akifia hospitali hutakiwi kulipia gharama za matibabu kwani nilidhani wanalipia waliopona tu.
mimi niliwahi kulamba sukari na majani nikanywa na maji ya baridi kisha nikakaa juani...................
Hivi umesema ulivokuwa mtoto au hadi sahivi una ujinga mpenzi?
ujinga hauishi mpendwa Evelyn Salt au nadanganya Slave ?
Me nilikuwa najua eti Posta kuna bomba kuubwaa ukienda kupost barua inasafirishwa ndani ya bomba hadi inafika ulikotuma!! Thijui kungekuwa na mabomba mangapi!
mimi nilikua naamini kuna watu wamekaaa sehemu wananiangalia. na ni baada tu ya kuanza kuangalia sinema eti unamuona mtu anaiba au amejificha alafu wenzie hawamuoni nikajua na sisi ni hivyo hivyo kuna watu wanatuona na sisi hatuwaoni.
Niliwahi kumuuliza mdingi baada ya kuona magari mengi Posta ".....yote haya huna hata moja?
unamaanisha baby wangu Slave ni mjinga!!!!!!
unanitafuta maneno......
Miaka hiyo ya 1978 kuendelea hadi 1985 nilikuwa najua wanaovaa miwani wote ni wasomi sana tena sana, na pia mwalimu yoyote nikikutana nae amebeba mzigo lazima nimkimbilie nimsaidie na hata kwenye yale mabasi yetu ya mjini (town bus) "Shimawino" tulikuwa haturuhusiwi kukaa kwenye siti hata kama zipo wazi tunajua ni za wakubwa tuu, kweli tulikuwa gizani.
Mi nilikuwa nikimuona mtu alievaa miwani alafu anakipara basi najua ni daktari pia tajiri wakutupa
Ujinga una mwisho, kwanza sio ujinga alikuwa na utoto tu!!!!!!!!!teh teh teh..... Sasa kama ingekuwa ujinga unaisha si elimu pia ingekuwa na mwisho mpendwa...!!!