Zamani ukisikia siku ya Bajeti ilikuwa Talk of the Town, Nchi ilizizima, siku hizi habari utaziona kwa uchache sana

Zamani ukisikia siku ya Bajeti ilikuwa Talk of the Town, Nchi ilizizima, siku hizi habari utaziona kwa uchache sana

Bush Dokta

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2023
Posts
24,831
Reaction score
45,154
Sijajua kama ni shida ya Watanzania au shida iko kwenye bajeti zenyewe.

Ama Watanzania wamesusa baada ya kuona hazina maana sana kwao au ni ujinga tu wanahitaji kuelimishwa.

Zamani tukiwa vijijini ukisikia leo Bajeti ya Nchi itasomwa Nchi nzima masikio na Macho ilikuwa Dodoma.

Siku hizi habari za Bajeti huzisikii sehemu yoyote wala mitaani.

Habari naona heading to Hapa Jukwani na mimi sijalifungua na lina wachangiaji na wasomaji wachache sana.

Hadi Msoma Bajeti anajaribu Kuvuta attention kwa kufananisha Note na jezi ya team ya mpira ili kupata kiki za kuforce.

Enzi za Dkt. Mkulo habari ingekuwa nyingine.

Je tatizo ni Watanzania kushadadia mipira, sanaa na miziki na kuacha mambo ya msingi au Shida ni Bajeti na wasoma bajeti.

Hili nalo mkalitazame wana nzengo

PIA SOMA
- News Alert: - Waziri Mwigulu awasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025
 
Technology!! imekua na inaendelea kukua Kwa kasi###ChillBroo###vyanzo vya upatikanaji wa taarifa ni vingi mnoo,You Choose What You Want for waking up braincells
 
Wananchi wamechoka kusubiria tozo za kuwakamua na kufanya maisha yazidi kuwa km laana kwao kuzaliwa Tanzania
Kwani Bajeti si Wananchi? Kwanini wasuse na wakati inahusu ada, afya na shule za Watoto wao?
 
Hii kitu kuna mtu nilikuwa namwambia jana

Zamani siku ya kusomwa bajeti Nchi yote inakuwa na hali ya ukimya...
Sehemu zenye TV watu walikuwa wanajaa wanafuatilia....Wengine unawakuta wako na headphones masikioni wanasikiliza...Na inakuwa ni mjadala kila mahali..

Siku hizi sasa....Tumewezwa na mambo ya Simba na Yanga...Na wameshatujua na ndiyo huko wanapohakikisha mambo yanakuwa sawa tuendelee kupoteza muda...Tukishtuka hadi ardhi walizonunua wazee wetu vijijini huko zimeshauzwa😄
 
Sijajua kama ni shida ya Watanzania au shida iko kwenye bajeti zenyewe.

Ama Watanzania wamesusa baada ya kuona hazina maana sana kwao au ni ujinga tu wanahitaji kuelimishwa...
Hata Leo ilikua talk of the town

Na kumezizima

Wewe tu na chuki yako

Ndio maana na sredi umekuja kuanzisha

Punguza silesi dogo
 
Hata Leo ilikua talk of the town

Na kumezizima

Wewe tu na chuki yako

Ndio maana na sredi umekuja kuanzisha

Punguza silesi dogo
Hahahaa.......Mkuu leo nimezunguka Mji mzima sijasikia mtu yoyote mahali popote wakiongelea bajeti na sio leo tu hata mwaka jana ilikuwa hivi hivi.
 
Back
Top Bottom