Zamani ukisikia siku ya Bajeti ilikuwa Talk of the Town, Nchi ilizizima, siku hizi habari utaziona kwa uchache sana

Unazungumzia zamani ipi? Maana mimi nina mwaka wa 27 leo nafuatilia bajeti.
 
Vina muda basi kuja kudanganywa nani anataka wa tutulize wese uku kitaani
 
Hazina jipya, bajeti za kumkamua mtanzania kila mwaka unakimbilia Tv kutazama maumivu?

Mimi ndio nimeona habari za bajeti usiku huu hapa JF, nilikua sifahamu chochote, wengi hasana habari nszo.
 
Ccm ni chama kilichopoteza mvuto kwa kizazi hiki, kitendo Cha kugeuza bunge kuwa la chama kimoja limepotezea mvuto bunge zima. Na hiyo ni kidogo, subiri uone uchaguzi utakavyokuwa na wapiga kura wachache, maana hakuna atakayepoteza muda kupiga kura kisha ccm watangazwe washindi.
 
Uko sahihi kabisa, lakini hali hii inaweza kuwa imepelekewa na mambo ya viongozi wetu wanaokuwepo madarakani. Mfano mzuri tuu hivi unakumbuka awamu ya hayatti magufuli namna watu walijawa na hamu ya kufuatlia vyombo vya Habari kaka kutafuta Habari za nini setikali imefanya siku husika, serikali inajambo gani, na rais sna hotuba gani. Ukweli ni kuwa watu wamekata Tamaa na nchi Yao hawaoni haja ya kufuatlia mambo ya siasa tena kutokana na ujinga wa baadhi ya viongozi wenye Nia ovu na nchi yetu.
 
Noma sana aisee wamechoka kweli
 
Hili naliona....kwenye issue za siasa watu wamejikataa kabisa.
 
Hazina jipya, bajeti za kumkamua mtanzania kila mwaka unakimbilia Tv kutazama maumivu?

Mimi ndio nimeona habari za bajeti usiku huu hapa JF, nilikua sifahamu chochote, wengi hasana habari nszo.
Hii Tabia Ya Wananchi kususia mambo ya Kitaifa sio nzuri na ina impact kubwa kwenye Social and National cohesion.

Watz sio wamoja tena
 
Kiukweli bajeti ilikosa muelekeo baada ya nchi tatu kuanza kutofautiana East African Community. Nyerere akajikita kwenye Ukoministi asioujua ,Kenya na Uganda waka maintain sera za Mwingereza.
Tulikuwa na East African Currency Board hata Yemen ilikuwemo.Mara mpasuko kila mmoja akachapisha pesa yake.
Hawa mawaziri wa fedha kwetu tulikuwa n Habib Jamal,Kenya nadhani walikuwa na Mwai Kibaki,Uganda sikumbuki.Na kweli bajeti zao zilikuwa zenye mashiko.
Pammoja na kuwa na finance Minister nakumbuka tulikuwa na wizara ya mipango ikiongozwa na Abudulhaman Babu.
Bajeti kweli ilikuwa bajeti, kuna mwaka Jamal aliiongeza bei ya kibuku senti kidogo,kumbe wanywaji kibuku walikuwa wanafamiana hasa pale Tanzania Region club ya askari wastaafu vita ya kwanza na pili.Wakasusa kuinunua na kuinywa baada ya siku kama nne hivi Jamal alibadirisha gia angani na kuirudisha bei ya awali tena serikali ikiomba samahani.
Nowadays ni man eat man society,wabunge wengi,mawaziri wengi,wachumi wengi,washauri wengi hadi AI lakini hakuna unafuu.
 
Huyu Abdulrahman Babu uliyemtaje ndio yule wa Umma Party?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…