Zamaradi Mketema: Watanzania tulirogwa na nani?

Zamaradi Mketema: Watanzania tulirogwa na nani?

IMG_8147.jpg
 
Hilo swali la watu kutokuwa na uzalendo angewauliza viongozi wa Serikali wanaokwapua na kufanya ufisadi Kila siku, yeye akiwa mzalendo inatosha asiwapangie Cha kufanya wasiotaka kuwa wazalendo
 
Mtangazaji Zamaradi Mketema amechukizwa na tabia ya Watanzania kutokuwa wazalendo kwenye masuala ya kitaifa hususani kwenye mashindano yanayohusisha nchi na nchi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram zamaradi amesema,

"Msanii wa NIGERIA akikosa tuzo ama hata kushindwa kwenye shindano lolote unayaona kabisa maumivu ya WANIGERIA, wananchi wao huumia kutoka moyoni, Njoo huku kwetu sasa, MSANII akikosa Tuzo ama shindano lolote ndio unapoishuhudia wazi kabisa FURAHA ya Watanzania, kiufupi kushindwa kwa wasanii wetu ni furaha na Vigelegele kwetu huku vicheko na maneno ya Dhihaka yakisindikiza kushindwa kwao, hivi somo la UZALENDO limekuwa Gumu kiasi hiki Tanzania!!!? WENZETU WAMEWEZAJE!!? Na sisi Tulirogwa na nani!!!??" - Mketema

Nini maoni yako?

Written by Mjanja M1 ✍️
Nyinyi mnapokuwa na mafanikio na ushindi mnadai Nchi ni yenu kwa misemo ya Nchi inawenyewe.

Tena mnakwenda mitandaoni kujidai nyie ni wajanja na tusiwapangie cha kufanya.

Ila mkifeli mnataka tufeli sote?

Ujinga mtupu.
 
Hilo swali la watu kutokua na uzalendo angewauliza viongozi wa serikali wanao kwapua na kufanya ufisadi Kila siku, yeye akiwa mzalendo inatosha asiwapangie Cha kufanya wasiotaka kua wazalendo
Zamaradi ameonesha kiwango kidogo sana cha kuchambua maswala
 
Umaskini chuki na roho ,hao wanaijeria hata kutunga nyimbo hovyo kama bongo tu ,ukitafsiri mashairi ya hovyo unakuta mtu eti anashabikia Asake yulee hata kuimba hajui.

Hapa bongo kama wote wapo against ya Diamond kama wanamchukia ila akikosa tunzo bado wanamlaumu yeye.... Tanzania ujinga ni mwingi sana wanafurahi mtu kukosa ndio hawa waliandaa petition ili mtu ashindwa eti kwa mlengo wa siasa.

Pambaneni na ujinga wenu ,kila kitu mnaleta siasa msanii nje ya kipaji chake ana haki ya kupiga kura na kuchagua chama chochote.
Hasira za nini Mkuuu?

Mnataka uzalendo kwenye Kukata mauno?
Kila mtu apambane na hali yake.

Kwenye Ufisadi na wizi wa mali za umaa kimya.....kwenye Mipira na Kukata mauno Mnataka Uzalendo

Wafrika mmerogwa.
 
Apambane na hali yake. Yeye aliyokua anawafanyia wenzie pale clouds wakati ruge anamlala hakuuona uchawi ule?
Watz ni wabinafsi sana. Yeye Mambo yakimwendea hana habari na wenzake.

Mambo yamemwendea kombo sasa analalamika eti watanzania wana Roho mbaya anasahau ya kwake.
 
Hasira za nini Mkuuu?

Mnataka uzalendo kwenye Kukata mauno?
Kila mtu apambane na hali yake.

Kwenye Ufisadi na wizi wa mali za umaa kimya.....kwenye Mipira na Kukata mauno Mnataka Uzalendo

Wafrika mmerogwa.
Toa ujinga wako wa siasa .!!
 
Mtangazaji Zamaradi Mketema amechukizwa na tabia ya Watanzania kutokuwa wazalendo kwenye masuala ya kitaifa hususani kwenye mashindano yanayohusisha nchi na nchi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram zamaradi amesema,

"Msanii wa NIGERIA akikosa tuzo ama hata kushindwa kwenye shindano lolote unayaona kabisa maumivu ya WANIGERIA, wananchi wao huumia kutoka moyoni, Njoo huku kwetu sasa, MSANII akikosa Tuzo ama shindano lolote ndio unapoishuhudia wazi kabisa FURAHA ya Watanzania, kiufupi kushindwa kwa wasanii wetu ni furaha na Vigelegele kwetu huku vicheko na maneno ya Dhihaka yakisindikiza kushindwa kwao, hivi somo la UZALENDO limekuwa Gumu kiasi hiki Tanzania!!!? WENZETU WAMEWEZAJE!!? Na sisi Tulirogwa na nani!!!??" - Mketema

Nini maoni yako?

Written by Mjanja M1 [emoji3578]
Mwambie Nigeria sio Tanzania lakini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Angehoji wale vijana wa CCM chipukizi walioshinda wote watoto wa vigogo kabla ya kuhoji uzalendo
 
Mtangazaji Zamaradi Mketema amechukizwa na tabia ya Watanzania kutokuwa wazalendo kwenye masuala ya kitaifa hususani kwenye mashindano yanayohusisha nchi na nchi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram zamaradi amesema,

"Msanii wa NIGERIA akikosa tuzo ama hata kushindwa kwenye shindano lolote unayaona kabisa maumivu ya WANIGERIA, wananchi wao huumia kutoka moyoni, Njoo huku kwetu sasa, MSANII akikosa Tuzo ama shindano lolote ndio unapoishuhudia wazi kabisa FURAHA ya Watanzania, kiufupi kushindwa kwa wasanii wetu ni furaha na Vigelegele kwetu huku vicheko na maneno ya Dhihaka yakisindikiza kushindwa kwao, hivi somo la UZALENDO limekuwa Gumu kiasi hiki Tanzania!!!? WENZETU WAMEWEZAJE!!? Na sisi Tulirogwa na nani!!!??" - Mketema

Nini maoni yako?

Written by Mjanja M1 ✍️
CCM imetufundisha na kulea kuchukiana hususan kama siyo mwanaCCM basi hata usalama watakuchukia.

Sasa huyo Mketema aache ushubwada, apeleke malalamiko yaje pale kwetu Lumumba waone matokeo ya athari za siasa za kiinterahamwe walizoziasisi
 
Ruge alipompoteza Zamaradi alifanya jitihada ya kumtafuta na kumpigia simu ambapo kwenye simu hiyo, Ruge alisikika akilia akimuomba Zamaradi asimuache, lakini Zamaradi akavujisha mazungumzo yao na kilio cha Ruge kwa rafiki zake au mitandaoni...Je, Zamaradi alirogwa na nani?
Hahahaaa.......hayo aliyoyafanya yatamkuta tu siku moja in the same way
 
Fanya kazi uchawa wa siasa mwanaume haupendezi ... Umaskini utakumaliza punguza chuki.
Endeleeni kukata mauno mkisubiri kupewa sifa.

Ukishinda tuzo ni yako wewe binafsi ukifeli pia ni wewe umefeli.

Usitake shida zako tukubebee sisi.
 
Huwa ninakereka sana pale malaya wa enzi za TANU anapojifanya ana busara sana... huyo Zama akae kimya
 
Jibu ni


Wasanii wa Nigeria kwenye shida zote hata huandamana pamoja kudai haki


Tanzania wasanii wamechagua upande


Wakishindwa wananchi wanafurahi
 
Wasanii wete wenyewe si wazalendo, hawajawai kusimama na wananchi pale kunapokua na tatizo linalohitaji sapot yako, wasanii wapo sambamba na serikali kusapoti agenda za serikali na chama ili kuwakandamiza wananchi
 
Back
Top Bottom