Zanzibar: Bawa la ndege laokotwa Kisiwani Pemba

Zanzibar: Bawa la ndege laokotwa Kisiwani Pemba

Ila ndege mpaka leo haijapatikana hapa kuna kiini macho flani hivi.
 
Uchunguzi wa awali umebaini kuwa Bawa la ndege lililookotwa na wavuvi wa kisiwa kidogo cha Kojani kisiwani Pemba ni ndege aina ya boieng 777 ikidaiwa kuwa huenda ni ndege ya Malaysia iliopotea wakati iliporuka kuelekea nchini China.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania Hamza S. Johari amesema mara baada ya kuonekana kwa bawa hilo walituma timu ya watalamu kisiwani Pemba na baada ya kulinganisha vielelezo walivyopewa wamethibitisha kuwa ni kweli ni bawa la ndege la aina ya boieng 777 inayodhaniwa kuwa ya Malaysia iliyoruka kwa namba MH 370.

Kufa kufaana wakojani waliookota wanatarajiwa kuzawadiwa zawadi nono na mamlaka hiyo kutokana na kitendo chao cha uzalendo wakuokota kutunza na kuripoti bila ya kufanya uharibifu na kutoa tarifa kunako husika.

Kufatia tukio hili baadhi ya wananchi kisiwani Pemba wamekuwa na maoni tofauti, wapo wanaoona kuwa limetegua kitendawili kilicho gubika dunia juu ya ndege hio ila pia wapo wanaoona imetoa mwelekeo wa kutafuta mabaki zaidi.

Chanzo: ITV
 
Pemba itatangazwa bbc. CCN. AL JAZIRA.. na dunia nzima..Hongera Magufuli mbona
 
Wakichelewa kuja kulichukua watakuta limeshauzwa kama scraper
 
Uchunguzi wa awali umebaini kuwa Bawa la ndege lililookotwa na wavuvi wa kisiwa kidogo cha Kojani kisiwani Pemba ni ndege aina ya boieng 777 ikidaiwa kuwa huenda ni ndege ya Malaysia iliopotea wakati iliporuka kuelekea nchini China.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania Hamza S. Johari amesema mara baada ya kuonekana kwa bawa hilo walituma timu ya watalamu kisiwani Pemba na baada ya kulinganisha vielelezo walivyopewa wamethibitisha kuwa ni kweli ni bawa la ndege la aina ya boieng 777 inayodhaniwa kuwa ya Malaysia iliyoruka kwa namba MH 370.

Kufa kufaana wakojani waliookota wanatarajiwa kuzawadiwa zawadi nono na mamlaka hiyo kutokana na kitendo chao cha uzalendo wakuokota kutunza na kuripoti bila ya kufanya uharibifu na kutoa tarifa kunako husika.

Kufatia tukio hili baadhi ya wananchi kisiwani Pemba wamekuwa na maoni tofauti, wapo wanaoona kuwa limetegua kitendawili kilicho gubika dunia juu ya ndege hio ila pia wapo wanaoona imetoa mwelekeo wa kutafuta mabaki zaidi.

Chanzo: ITV

Naona mzigo wa lawama kupotea kwa hii ndege kaangushiwa Pilot, kwama alikuwa on sucide mission.
 
pia wanaJF mfahamu kuwa ndege nyingi za mashirika makubwa pia huanguka baharini mara kwa mara, sasa ili kulinda brand, atayri wana chain ya kusilence media na walalamikaji waliopoteza jamaa zao. ni sawa na mtu apotee halafu ukienda polisi waseme hawana taarifa. ndege nyingi tu km za qatra, emirate nk, watu wanaanguka katikati ya bahari na wanapotea na dunia haijui, ni ikulu tu za mataifa ndo kuna hizi classfied info
 
pia wanaJF mfahamu kuwa ndege nyingi za mashirika makubwa pia huanguka baharini mara kwa mara, sasa ili kulinda brand, atayri wana chain ya kusilence media na walalamikaji waliopoteza jamaa zao. ni sawa na mtu apotee halafu ukienda polisi waseme hawana taarifa. ndege nyingi tu km za qatra, emirate nk, watu wanaanguka katikati ya bahari na wanapotea na dunia haijui, ni ikulu tu za mataifa ndo kuna hizi classfied info
mmmh!
 
Baseless meaning?

Timu ya wachunguzi ndio imeona kwamba Pilot alishusha ndege chini ili ku kwepa rada za kijeshi na ku de-pressure ndege na kupelekea abiria kufa kabla hajaipotezea baharini.

Kitaalamu iko sawa, ila swali linalobaki ni kuwa co-pilot alikuwa wapi?
 
Kama ni classified info wewe umejuaje haya?
pia wanaJF mfahamu kuwa ndege nyingi za mashirika makubwa pia huanguka baharini mara kwa mara, sasa ili kulinda brand, atayri wana chain ya kusilence media na walalamikaji waliopoteza jamaa zao. ni sawa na mtu apotee halafu ukienda polisi waseme hawana taarifa. ndege nyingi tu km za qatra, emirate nk, watu wanaanguka katikati ya bahari na wanapotea na dunia haijui, ni ikulu tu za mataifa ndo kuna hizi classfied info
 
Kwani wafanyakazi wa Ikulu ni midoli? ni watu kama wewe, hivyo fursa ua kujua hayo na mengineyo ipo.
Tukio limetokea USA na ikulu ikataarifiwa habari ikawa classified, mmatumbi aliepo nchi za mavumbini anaatuambia kuna ndege zinadondoka basi mmatumbi huyu anafanya kazi Ikulu ya Marekani
 
Tukio limetokea USA na ikulu ikataarifiwa habari ikawa classified, mmatumbi aliepo nchi za mavumbini anaatuambia kuna ndege zinadondoka basi mmatumbi huyu anafanya kazi Ikulu ya Marekani
kwahyo wote tulio JF unadhani tuko Bongo land au? pia mtu anaweza akaitumikia Marekani akiwa Tanzania. Acha umbu.mbu.mbu
 
Back
Top Bottom