Zanzibar ina watu wenye akili sana. Serikali yao inatambua hili ndio maana huduma zote muhimu za afya hupewa bure

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Anayebisha aende hapo Zanzibar nauli ni ndogo tu kwenda na kurudi. Unakwenda asubuhi mchana unafanya tafiti zako jioni unarudi
Huduma zote za afya hasa zile za msingi au zile za umuhimu zaidi Zanzibar ni bure kabisa.
Zanzibar mwanamke anapokwenda zahanati, kituo cha afya au hospitalini kujifungua hakuna kubeba vikorokoro, hata akijifungua kwa operation halazimiki kuchangia hiyo gharama.
Hapa Dar es salaam mke wako akijifungua kwa operation kazi unayo iwe public au private hospital.
Hii ni kwasababu Zanzibar ina watu wenye akili nyingi.
Tuombee vizazi vyeti viwe na akili nyingi ili wasiishi kwa kubahatisha.
 
Angalau umeona. Kuna wajinga humu husema Zanzibar wala urojo, mara ooh Zanzibar huwafanya watoto wasiwe na vichogo na ndio maana huwa na akili ndogo.
Nyinyi Watanganyika nani aliyewaroga??!!
Kaeni na vichogo vyenu kama nyanya mshumaa 🤣
 
Nyerere namlaumu sana kwenye haya mabutumbafu
 
Hata wabara wakienda Zanzibar wanajifungua bure?
 
Yaani unakuja hapa kustaajabu "kamkoa" kenye Watu laki 8 kutoa huduma za aina hiyo kweli?
Kwanza kama sugadaddy anaitwa Tanganyika na pili kana buzi linaitwa "Uarabuni" afu mwisho kana danga linaitwa watalii
 
Usidanganyike, Tanganyika ndio tunao gharami hiyo uduma ya afya Zanzbar
 
Angalau umeona. Kuna wajinga humu husema Zanzibar wala urojo, mara ooh Zanzibar huwafanya watoto wasiwe na vichogo na ndio maana huwa na akili ndogo.
Nyinyi Watanganyika nani aliyewaroga??!!
Kaeni na vichogo vyenu kama nyanya mshumaa 🤣
Tunashukuru kwa matusi yakhee, ila kwa hili la kujali huduma ya afya kwakweli hapo mliweka urojo pembeni mkapiga kazi

Huku bara twalia yakhee, watu wanalimbikizia mali tu wakiumwa waenda tibiwa ulaya sheikh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…