Zanzibar: Kanisa la T.A.G pamoja na makazi ya Mchungaji wake Daudi Suna, yamebomolewa na wanaodaiwa ni wakazi wa eneo hilo

Zanzibar: Kanisa la T.A.G pamoja na makazi ya Mchungaji wake Daudi Suna, yamebomolewa na wanaodaiwa ni wakazi wa eneo hilo

Kwanza tusiwe na jazba,swali la msingi,anayetoa kibali Cha ujenzi wa Kanisa au kitu chochote ni serikali,mamlaka husika ya eneo,je huyo pastor alipata vibari vya ujenzi wa Kanisa?

Pili sio sahihi kujenga nyumba ya Ibada karibu na makazi ya watu na kufanya mahubili kwa sauti kubwa wakati wa usiku,hata zile adhana za ndugu zetu za alfajiri Mimi huwa zinanikela kwa maeneo ambayo misikiti ipo kwenye makazi ya watu.

Tatizo la makanisa ya ndugu zetu walokole,Ibada zao ni ndefu Tena mziki mkubwa kwa sauti ya juu,sasa Kanisa likiwa kwenye makazi ya watu hii inakuwa ni shida sana.

Fikeni Dodoma,kisasa muone makazi yalivyopangiliwa,makanisa,misikiti,bar,lodge nk,hakuna KERO maana sayansi imetumika kwenye plan ya mji,sio kujijengea tu.

Kwenye hii story,kichwa kinasema wananchi wamebomoa Kanisa,je wao ndio wameleta Hilo gari la kubomoa?mi nilitegemea nione shoka,nyundo,wananchi wakivunja Kuta!
Hiyo misikiti na makanisa yanayojengwa katikati ya makazi hapa dsm umeiona..au kwakuwa ni zenji ndio unaona sio sawa kanisa kujengwa kwenye makazi yawatu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kanisa la T.A.G pamoja na makazi ya Mchungaji wake Daudi Suna yamebomolewa na wanaodaiwa ni wakazi wa eneo hilo wakishinikiza kuwa hawataki Kanisa katika eneo lao.

Hii ni kunyume kabisa na sheria za nchi zinazoruhusu Uhuru wa Kuabudu. Kama jambo halitafanyika basi ni wazi kuna kiongozi mbaguzi wa dini anaewalinda wabomoaji na pia hii itachochea sehemu nyingine makanisa na makazi ya wachungaji kubomolewa.

Pia miezi michache ijayo kipindi cha mfungo kikianza huwa ni marufuku kwa wakristo kula sehemu za wazi, ukikutwa unafungwa mpaka mfungo uishe, wengine huwa wanapigwa sana, sasa hapa ni kwamba mtu kama umeamua kufunga kwa imani yako iwaje hutaki kuona wenzako hawali, ni kwamba imani yako no nyepesi sana kuisimamia, kama ni hivyo kuna haja gani ya kufunga.

View attachment 2146530

View attachment 2146523

============================================

Taarifa uhakika juu ya tukio hilo ni kuwa Mchungaji David Victor Suna ni mzaliwa wa Sumbawanga, lakini kwa miaka mingi amekuwa akiishi Zanzibar baada ya familia yake kuhamia huko. Kaka yake naye ni mtu wa kanisani lakini anafanya shughuli zake Dar es Salaam.

Alipoanza harakati za kutafuta eneo kwa ajili ya kanisa alipata wakati mgumu kwa kuwa walikuwa wanamkatalia, baadaye akabadili gia na kutafuta eneo la kununua la kwake binafsi na siyo kwa ajili ya kanisa.

Baada ya kutafuta eneo lake binafsi ndipo akapata eneo hilo lililopo Sebleni, Unguja. Akanunua kwa Sh 16,000,000 (milioni 16) akalipa fedha taslimu, akasaini mkataba rasmi wa mauziano (tazama picha), japokuwa katika eneo hilo alikuta mmiliki tayari amejenga banda ambalo nalo lilikuwa sehemu ya mkataba wa manunuzi.

Baada ya kununua akajenga ukuta kuzungushia eneo husika kisha akaanza shughuli zake za ibada, baada ya majirani kubaini kuwa mnunuzi ameanzisha kanisa eneo hilo ndipo mgogoro ulipoanzia.

Wakamwabia hatakiwi kuwa na kanisa eneo husika lakini David Victor Suna akashikilia msimamo wake kuwa ataendelea na shughuli zake za kanisa.

Mhusika ambaye aliuza eneo hilo naye akamvaa David Victor Suna na kumtaka arejeshe eneo hilo kwa kuwa hakuuza kwa ajili ya kanisa bali kwa ajili ya kujenga makazi, bado David Victor Suna akagoma kubadilisha matumizi wala kurudisha eneo.

David Victor Suna akawa asisistiza kuwa yeyote mwenye malalamiko aende Mahakamani ambapo haki itatendeka, hata waliposhirikisha Serikali za mtaa nao wakawa wanamshawishi ama kubadili matumizi au kurejesha eneo, msimamo ukawa ni uleule.

Ndipo siku ya tukio, lilikuka bulldoza likaanza kuvunja eneo husika wakati wahusika wakiwepo wachache wakiendelea na ibada kama kawaida, kanisa likavunjwa na baadhi ya vitu vikiwemo viti vikaharibiwa na gari hilo.

Mamlaka za Serikali za mtaa hazijawa tayari kuzungumzia tukio hilo, naye David Victor Suna amekuwa mgumu kuzungumzia kinachoendelea kwa kile kinachodaiwa hajatulia hadi sasa.

SERIKALI YAINGILIA
Taarifa zinaelezwa kuwa Mkuu wa Wilaya wa eneo husika anatarajiwa kutolea ufafanuzi suala hilo mchana wa leo Machi 11, 2022.

Nitarudi kuwapa kilichoendelea kuhusu tamko la Serikali.

ITAENDELEA...
View attachment 2146667
View attachment 2146668
View attachment 2146670
View attachment 2146671 View attachment 2146672

Naona kuna tatizo hapa, masharti vigezo, desturi, imani na tamaduni haikuzingatiwa.

Unaweza kumiliki eneo lakini kuna masuala mtambuka ambayo mnunuzi hakuyazingatia akayaona ni mepesi, kumbe kuna mengine hayaandikwi lakini yanafuatwa na jamii husika wakaazi wenyeji wa mwanzo kabisa .
 
Injili itahubiliwa mataifa Kwa mataifa na hapo kila MTU akishahubiliwa na kuskia neno la mungu ndipo mwisho wa dunia hii utakapofika.

Hapo kuna Vita ya kiroho inaendelea na watumishi wa mungu Kwa msaada wa roho mtakatifu watashinda hio Vita.
 
Hayo majamaa mapumbavu sana, yanashindwa kuelewa tafsiri za maneno ya kiswahili kwa zama hizo yalikuwa yanatungwa na Waarabu ndiyomaana Kanisa liliitwa Sinagogi sababu bado kiswahili kilikuwa hakijakua ktk ubora wake sawa na zama hizi?

Mawatu mengine bhana ni tabu tupu kujitambua yakishakaririshwa ujinga wa hadithi za vijiweni.
Mkuu sinagogi ni msikiti wa wayahudi.

Sio kanisa.
 
Naona kuna tatizo hapa, masharti vigezo, desturi, imani na tamaduni haikuzingatiwa.

Unaweza kumiliki eneo lakini kuna masuala mtambuka ambayo mnunuzi hakuyazingatia akayaona ni mepesi, kumbe kuna mengine hayaandikwi lakini yanafuatwa na jamii husika wakaazi wenyeji wa mwanzo kabisa .
Kama ardhi ni Mali ya serikali.

Mwanainchi wa kawaida hana mamlaka ya kumpangia mwenzie cha kufanya.

Waache ubaguzi wa dini na utaifa pia.

Huyo angekuwa mkristo lakini asili yake sio bara wala wasingethubutu kumsogelea.

Wazanzibar ni wabaguzi.
 
Kama ardhi ni Mali ya serikali.

Serikali inaongozwa na watu, ila watu hao wana imani, desturi, tamaduni pia taratibu zao hivyo mtu makini hawezi kupuuza yale ambayo hayajaandikwa katika katiba.

Afrika itaangamia ...

31 Dec 2020 — Utamaduni usio dhibitiwa na unao sambaa kiholela ni hatari sana kwa kesho ya Afrika.
Utamaduni ni muhimu kwa wanasosholojia kwa sababu una jukumu muhimu na muhimu katika uzalishaji wa utaratibu wa jamii, ambayo inahusu utulivu wa jamii kulingana na makubaliano ya pamoja ya sheria na kanuni ambazo zinaruhusu sisi kushirikiana, kufanya kazi kama jamii, na kuishi pamoja (kwa hakika) kwa amani na maelewano.
 
Yaani mtu akuzidi miaka 590 halafu mtu anajimwambafy sie tulitangulia daa wakati unajiuliza naongea na mtu au picha ya mtu! Na hapo baada ya kafariki ikapita miaka 557 useme tulitangulia kama si ku copy na ku paste!
Hivi Yesu aliposema ''

Sikuja kutengua torati,
Bali kuitimiliza ""

Alimaanisha nini?

Ndy ujuwe kama dini ilikuwapo na mitume ilikuwapo/vitabu vya dini pia vilikuwapo kabla ya Yesu kuja duniani...

Au na Yesu alicopy?

Je hao waliokuwapo kabla ya Yesu kusulubiwa hawakuwa wakristo?
Au walikuwa dini gn?
 
Mkristo wa wapi wewe? Kwa hiyo kama wewe umezaliwa mkristo, ukaenda kwenye uislam inabidi uhamie msikitini?
Hon siwez kuami ila nitafanya utaratibu mwingine wa kuabudu

Mim nimewai kufungua biashar ya kitimot Hapo singida nyum ya msikit mkuu sijui ila yaliyonitokea siyo poa
 
Mbona waislamu wana misikiti ipo Ulaya na Marekani na maeneo yenye wakristo wengi na hakuna mtu anawabugudhi

Hata hapa Tanzania bara maeneo ya wakristo wengi misikiti ipo na hakuna mtu wa wakubugudhi
Siyo watu wote Ni waelewa hasa waisalamu hawaelewi lolote wanajiona wao ndio din sahih ulaya na huku tofauti Sana Tena Zanzibar huku bara hatuna shida nao kbsa
 
Hii iko kwa pande zote hata wakristo huwa tunapiga vita uislam baadhi ya maeneo.

Mimi ni mwenyeji wa kibosho Moshi, walitokea waislam katika kijiji kimoja kinaitwa Mweka ambapo kuna taasisi kama Chuo cha wanyamapori, geti la kushukia watalii kutoka Mt kilimanjaro, mashule nk, hivyo wakataka kujenga misikiti ili waweze kuswali karibu maana misikiti upo moshi mjini.

Waliponunua eneo na kumwaga tofali na mchanga, fitna zikaanza na padre akasema kanisani mnakubalije misikiti hapa, kilichotokea ni vita mpaka mradi ukafa.

Nafikiri Watu wa dini zote wanahitaji kustaarabika na kuelewa kwamba tunatakiwa tuishi wote kwa kuchukuliana.
Hata kule kwetu meru Happ kwa mrefu Arusha kulitokea mwarabu mmoja kanunua sehemu wakapewa kbsa akaanza kujenga tank la maji badae akamaliza na msikiti mdg fln HV wananchi wa pale wengi ni wakristo basi asbh namapema Sana iliisikika adhana saa kumi na moja watu wote tulimkaah kutazam hyo kelel inatokeaa wapi .watu wakapandisha kumfata na kuelezwa kwamb ikifika saa sita kamili za mchana huo mskiti usionekane hapo au wasisikie kelel zozote za adhna ..msikit ulikufa palepale
 
Back
Top Bottom