Zanzibar: Padri auawa kwa kupigwa Risasi!

Zanzibar: Padri auawa kwa kupigwa Risasi!

Status
Not open for further replies.
Haya yote nayayotokea si kwa bahati mbaya bali wanaofanya hayo wanatekeleza yaliyomo katika mkataba wao na yule waliyemweka kwenye kiti cha enzi kwa kuhakikisha sauti ya waislamu inasikika na kuogopwa kila sehemu ya nchi.

Yote yamepangwa! na ni agenda yao ya siri. Ndiyo maana hata kiongozi "wetu" hawezi kusimama na kupanua mdomo katika kukemea hayo....!!!

Kwa akili na macho mepesi ujumbe huu unaweza kuonekana kama uchochezi, lakini ukweli ndiyo huo. modes nieleweni vizuri tu.

Pamoja tutafakari.
 
Wanasaikolojia wanasema kuwa "Mtu akisema kuwa atafanya jambo fulani, basi iko siku atalitenda"

Huyu mtu anaeitwa Hassan Ilunga wa Mwanza ni mtu muhimu sana katika upelelezi wa mauaji Padre Mushi, yeye ndiye aliehutubia waislam na kusambaza DVD kuwa waislam waue Mapadre, Maaskofu na Wachungaji iwe hadharani au kwa kujificha.

Kwa sababu yeye ndiye alitoa maagizo, kuna uwezekano wauaji walimpa taarifa kuhusu mipango ya uuaji. Kuna uwezekano Ilunga anafahamu mtandao wa kimafya, kuna taarifa kuwa kuna watu walipelekwa SOMALIA kwa ajili ya mafunzo ya uuaji (ushetani. Serikali ikikamata huyu jamaa atasema mtandao huo.


Mods najua mtafuta uzi huu but no p
 
Serikali inamuogopa!! Utashangaa watakao kamatwa ni waumini aliokuwa anaenda kuwahudumia!! Umesahau Buseresere kauawa Mchungaji, wakakamata wachungaji!!?
 
Mungu wetu wa Israel shughulika na tatizo hili.
Pumzika kwa amani Padri.
Mungu wa Isael anasema;nimefumba macho na mtakula jeuri yenu maana hamkuyajua yale yaletayo amani na
hakika kupigwa na utapigwa Tanzania maana adui zako wamepanga kukuzingira na watakupiga wewe na watoto wako wasikuachie jiwe juu ya jiwe maana hukuyajua yale yapasayo amani.
Ona maaskofu na wachungaji wako walivyojineenepesha kwa mali za wizi na rushwa,ona wanavyowatetea majambazi kisa wamehongwa ubunge, ona wanavyowakebehi watumishi wangu wa ukweli kwa sababu wamepewa magari ya rushwa na watawala waovu,ona wanavyojikomba kwa chama dhalimu cha mauaji ya watu wngu wasio na hatia,ona maaskofu wenu wanavyojipendekeza kwa serikali dhalimu,ona mapadri na wachungaji wenu wanavyowakomunisha majahiri na wezi huku wakijua kuwa wanashiriki kufuru kubwa kabisa,ona wachungaji na maaskofu wenu walivyo busy kutafuta mali ya dunia badala ya uso wangu!
Nasema kama niishivyo, mtakoma maana huo ni mwanzo tu kwani nyinyi na viongozi wenu mneniasi vya kutosha,nimechoka kuwavumilia na sasa mtapata kibano na kulia sana nami sitawasikia wala kuona mateso yenu mpaka hapo mtakapotubu vinginevyo ni kibano tu mpaka mjue kwamba mimi ndimi Bwana Mungu wenu,niliyeawaweka katika nchi hii ya maziwa na asali na mimi ndimi mtunza amani na sio viongozi dhaifu wenu na majeshi uchwara yenu hayo!
 
Kuna mtu anaitwa Ustadh Ilunga wa Mwanza alisambaza DVD na videos kwenye youtube zinazomwonesha akiwahimiza waislamu jinsi ya kupambana na mfumokristo. Moja ya njia aliyotaja ni kuua mapadre na maaskofu. Tafuteni hata kwenye youtube ile hotuba yake aliyoitoa akizungumzia mauaji ya sheikh Abood Rogo huko Mombasa, alihimiza waislamu nao watafute askofu wampige risasi afe. Vipeperushi vikaanza kusambazwa Zanzibar vya kuhimiza kuua mapadre, ndipo Padre Ambrose Mkenda akapigwa risasi, bahati nzuri hakufa. Wakasambaza vipeperushi vingine wakasema si mwisho. Leo yametokea tena, wamemuua padre Evarist Mushi.
Kinachonishangaza, huyu Ustadh Ilunga hajawahi kuhojiwa kuhusu kauli zake hizi.
 
Na zanzibar kuna tatizo kubwa la mapadre kutembea na wake za waumini...haya yapo na yanatokea..na pia huwa wanatembea na masista na halafu kuwarejesha Tanganyika...
hivo wanaou chunguza wachunguze ukweli..sio ugaidi...tu...tukiimba nyimbo za ugaidi ...sasa sijui watakamatwa nani kwani uamsho timu nzima iko jela....sasa labda akamatwe mufti na kadhi mkuu wa zanziabar.....
tabia zao mapadri hapa zanzibar zichunguzwe pia.....wamekua na tabia kinyume ya mafundisho yao



Mkuu adolay
Waislamu wa Zanzibar hawana tatizo na wakristu; wameishi begabega miaka mingi hata hay matatizo ya kuchoma makanisa chanzo ni siasa za maji taka; kama hawakuyachoma miaka hiyo iweje leo? Rejea kwenye suala la padri nimewauliza hivi hamjawahi kuona au kusikia mapadri wanazini na wake za watu mbona hamjibu? Kuuwawa kwa padri Zanzibar haimaniishi muaji ni muislamu anaweza akatoka George Kibaha kwenda kuua Zanzibar; sioni ni kwa misingi ipi mnataka kuwahusisha wazanzibar na mauji ya padri; acheni vyombo vya sheria vifanye kazi yake; JF wanafiki mpo wengi sana mnakumbuka siku alipouliwa polisi Zanzibar maneno mliyoyatoa? Hizo zote ni roho za binadamu.
Chama
Gongo la mboto DSM


Chama,

Naelewa unataka kupanua wigo wa 'potential' reasons kwanini Padre Evarist Mushi ameuliwa, na pia kwanini matukio ya kushambuliwa huko Zanzibar.

Kwa bahati nzuri, namfahamu (marehemu) Padre Evarist Mushi, nimefanya naye kazi. Na hata yule Padre mwingine aliyenusurika nimefanya naye kazi pia. Sababu ulizo-suggest -kutembea na wanawake- sio motive ya yeye kupigwa risasi. Padre Evarist ameuliwa kwa sababu ya imani yake! Na tukio la leo halikuja kwa kushtukiza, kumekuwepo na vipeperushi vinavyoelezea mipango ya kuuwa wakristo. Taarifa zimekuwa zinatolewa lakini hakuna chochote kinachofanyika!

Matukio mengine ya ku-target wakristo huko nyuma hayakuwa yanarepotiwa kama ilivyo sasa lakini nataka nikuambie mambo yalianza kwenda kombo miaka mingi iliyopita. Na ni wakristo wa madhehebyu yote. Makanisa yanachomwa, waumini wanavamiwa kila kukicha. Mwaka jana kanisa la Anglican (zamani ilikuwa ndio eneo la soko la watumwa) lilinusirika kuchomwa moto. Watu waliwahi kuuzima hata hivyo waliharibu vitu. Imefikia mahali hawa watu wanawashambulia sio tu wakristo walio hai, bali hata walio kufa! Makaburi ya wakristo yanavamiwa, misalaba inavunjwa/kuong'elewa na kuna kipindi walitaka kufukua maiti!

Wakristo Zanzibar wanaishi kwa kujificha. Mwaka jana hali ilikuwa mbaya kiasi baadhi wa viongozi wa makanisa (madhebu mbalimbali) kukimbilia Tanzania bara. Na waumini wengine hawakutoka makwao. Na hata waliobakia majumbani, inabidi mtu atoe taarifa mara kwa mara kwa waumini wenzio ili kujua kama mko salama! Hii ndio hali ilivyo.

Unaweza kuelewa ni jinsi gani mtu anakuwa very dissapointed anaposoma hoja zinazo-link mauji ya Padri Evarist na mambo ya wanawake. Hii ni kutomtendea haki marehemu na wahanga wengine wa maovu yanayoendelea.

Kwa kukufafanulia, wapo waislam Zanzibar - kiasi- ambao wanapinga kabisa hii tabia ya kuvamia makanisa na kushambulia wakristo. Wanakataa aina hii ya kutumia dini kufanya uovu. Lakini wanafanya hivyo kwa gharama kubwa. Mmoja wao ameshalipa hiyo gharama, naye ni yule sheikh waliyemwagia tindikali. Na hivi tunavyojadili hapa, hakuna mtu amekamatwa kwa tukio hilo la kumwagia Sheikh tindikali!

Zanzibar kuna tatizo, tuwe wakweli.
 
Kwa ufafanuzi wa swali lako gonga hapo; Ali Sina reveals Islam and Prophet Muhammad !
Acha ujuha Mdini mkubwa wewe....Uislamu unaongozwa kwa Kuran na hadith na wala sio vi-link vya mtandao vinavuonzishwa na wadini wakubwa kama nyinyi!! Yaani miongoni mwa watu wanaochefua kwa udini kwenye jukwaa hili wewe ni mmoja wapo na watu kama nyinyi hata huyo YESU atawakana kwa maana yeye pamoja na kukumbwa mikasa ya hapa na pale bado alikuwa mtu mwenye upendo na hakuwa na chuki wa yeyote!! Wewe humu jamvini posts zako ni za udini mtupu halafu unajiita mkristo...Mkristo gani wewe uliejawa na moyo wa jazba na chuki huku ukiwa huoneshi tofauti yoyote na watu kama akina Ponda?! Jichunguze kwa makini....pitia posts zako nyingi zinazohusiana na masuala ya dini, kisha soma Biblia kwa makini kisha tafakari kwa makini endapo mahubiri yako yanafanana na yale yaliyomo kwenye Biblia au vipi....!! Narudia, wakristo dizaini yako hawana tofauti yoyote na waislamu dizaini ya wafuasi wa Sheikh Ponda! Kinachokosekana kwako ni kukosa umoja toka kwa wadini wakubwa upande wa dini yako ili mkapata nguvu ya kufanya yale yanayofanywa na akina Ponda!
 
Tuwaacheni watu wa usalama wafanye kazi yao. Sheria ni msumeno lazima itapatikanq jibu..si mnajua damu ya mtu haipoteagi hivi hivi. Lazima litapatikana jibu tu.
 
hii nchi hii..!, kazi ya mahubiri ya sheikh ilunga imeanza kuonekana....
nyie ndio mnaosababisha machafuko inchi hii.... Sasa sheikh ilunga anahusikaje hapa. Wanajf..nyie ndio mnaoiharibu inchi hii kwa uchochezi wenye wa kishenzi.
 
Haya ni matokeo ya kampeni za udini zilizofanywa na viongozi wa ccm kwa ushauri wa tiss wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2010. Watu wenye akili finyu walidhani kuwa wakristu wangepigia kura wagombea wakristu kitu kilichowapa kiwewe na kuanza kuhubiri udini hovyo. Dhambi hii haitawaacha waasisi wa udini nchi hii.
 
NasDaz kinachosikitisha hakuna juhudi za wazi za makusudi kutoka kwa hao Waislamu safi kuelimisha wenzao ubaya wa haya!

Ndugu yangu MTAZAMO, unataka kuniambia hao unawaowaita Waislamu safi wanafurahishwa na hayo mambo?! Watafurahishwa vipi wakati wanawafanya wajiskie vibaya kwa kuonekana wao ni watu hatari?! Trust me, hao watu hawasukumwi na dini bali wana agenda binafsi na dini ni kama cover tu! Na kama wanafanya hivyo kwa ajili ya dini basi hawaifahamu dini....huo ndio ukweli wenyewe!!

Ngoja nikupe mfano wa yale yanayotokea Mashariki ya Kati!! Unakuta Mwislamu wa Suni anaenda kujilipua kwenye Msikiti wa Shiha...sasa huyo nae anapigania dini? Dini ipi wakati wote ni dini moja na walichotofautiana ni madhehebu?! Lakini ukifuatilia kwa makini, utakuta dhehebu moja lina-opress dhehebu lingine labda kwa vile dhehebu husika lina watu wazito serikalini au ndio wanaoshikilia na kumiliki keki ya taifa! jambo hili limetokea sana Iraq baada ya Saadam kuondolewa madarakani! sasa hiyo utaita dini? Tuje kwa Osama ambae ndo alifanya sura ya Uislamu iharibike kabisa duniani!! Je, huyu nae alikuwa anapigania dini?! Hivi ulishawahi kusikia Al-Qaeda ya Osama ikiripua Kanisa?! Hivi umeshapata kusikia Osama akiilenga Vatican au Cantebury?! Why target yake kubwa ilikuwa ni USA pamoja na UK? Why not at least Italy yaliko Makao Makuu ya RC au German iliko Lutheran?! USA na ukristo wapi na wapi? Hivi wewe unaweza kutamka kwa yakini kabisa kwamba Ukristo wa Marekani ni tishio kwa Uislamu? Kwa Ukristo upi walio nao? Hivi kuna uhusiano gani kati ya ukristo na overseas embassies ambazo Osama alikuwa anazilenga?!

Nimekupa mfano wa Osama kukuonesha ni namna gani watu wanatumia dini wakati ukiangalia kwa makini unakosa uhusiano wa matendo yao na kile wanachodai kukipigania! Osama alikuwa anapigana vita anayoifahamu mwenyewe...(Binafsi nahisi ni vita za kutetea Waarabu wenzake au ni vita dhidi ya watu wa magharibi)! Lakini kama ilivyo kawaida, njia moja wapo ya kushinda vita ni kuwa mzuri wa propaganda!! Osama alifahamu fika kwamba Waarabu hawapo kila mahala duniani, lakini Waislamu wapo kila mahala! Hivyo alifahamu kabisa akisema napigania Uislamu basi anaweza pata sapoti hata toka kwa wandengereko wa Tanzania kuliko kusema anapigania Waarabu! Na hilo akafanikiwa....!

Sasa basi, kwa haya yaliyotokea ZNZ, kwanza ni mapema mno ku-conclude ni nani amefanya mauaji hayo! Lakini vyovyote iwavyo, si sahihi kusema kwamba hao wauaji wamesukumwa na Uislamu...! Uisllamu kwa maana ipi? JIHAD au nini? JIHAD haipo hivyo....JIHAD kwa mujibu wa Uislamu ni pale inapotokea kuwapo kundi la watu kuwazuia Waislamu kwa namna yoyote ile kufanya ibada zao...mathalani, leo aje kiongozi mmoja na akatoa amri kwamba misikiti yote ifungwe na ni marufuku Waislamu kusali....hapo JIHAD ruksa! Na hapa ndipo Muislamu anapoambiwa kufa kwa ajili ya dini yake! Na hili hata Wakristo wanaweza kufanya....sizani kama nchi itakalika hii leo hii itangazwe kwamba marufuku Wakristo kwenda kanisani!

Sasa basi, kutokana na mfano mdogo wa JIHD ni nini hasa, je hao wa ZNZ wanapigana JIHAD ipi?
binafsi naona kinachotokea ZNZ ni ZNZ Politics! Ninavyozungumzia ZNZ politics hapa simaanishi siasa za CCM na CUF....bali siasa za "tuachieni ZNZ yetu"; hatutaki muungano!! Hawa wasiotaka muungano wana chuki ya wazi na watu wa Bara! Kwa bahati mbaya kabisa, makanisa yanaonekana ndio chimbuko la watu wa Bara!! Trust me, leo hii ikitokea Wakristo wote ZNZ wametoka na kurudi bara, wauaji hao sasa watawageukia Wabara wengine kwa visingizio vingine!
 
Mungu wa Isael anasema;nimefumba macho na mtakula jeuri yenu maana hamkuyajua yale yaletayo amani na
hakika kupigwa na utapigwa Tanzania maana adui zako wamepanga kukuzingira na watakupiga wewe na watoto wako wasikuachie jiwe juu ya jiwe maana hukuyajua yale yapasayo amani.
Ona maaskofu na wachungaji wako walivyojineenepesha kwa mali za wizi na rushwa,ona wanavyowatetea majambazi kisa wamehongwa ubunge, ona wanavyowakebehi watumishi wangu wa ukweli kwa sababu wamepewa magari ya rushwa na watawala waovu,ona wanavyojikomba kwa chama dhalimu cha mauaji ya watu wngu wasio na hatia,ona maaskofu wenu wanavyojipendekeza kwa serikali dhalimu,ona mapadri na wachungaji wenu wanavyowakomunisha majahiri na wezi huku wakijua kuwa wanashiriki kufuru kubwa kabisa,ona wachungaji na maaskofu wenu walivyo busy kutafuta mali ya dunia badala ya uso wangu!
Nasema kama niishivyo, mtakoma maana huo ni mwanzo tu kwani nyinyi na viongozi wenu mneniasi vya kutosha,nimechoka kuwavumilia na sasa mtapata kibano na kulia sana nami sitawasikia wala kuona mateso yenu mpaka hapo mtakapotubu vinginevyo ni kibano tu mpaka mjue kwamba mimi ndimi Bwana Mungu wenu,niliyeawaweka katika nchi hii ya maziwa na asali na mimi ndimi mtunza amani na sio viongozi dhaifu wenu na majeshi uchwara yenu hayo!

Sijui Mungu wa Tanzania nae atasema nini!!!
 
...Tuwape nafasi vyombo vya usalama vifanye kazi yake...Binafsi Naamini Watanzania tunachonganishwa! hiki ni kitendo cha ugaidi kilichoratibiwa vilivyo...soon mambo yote yataelea hadharani...
 
Nasdaq: ni kweli wasuni wanawafanyia washia maafa na washia Nao! Lakini ni udini! Ni ile dhambi ya ubaguzi, Nyerere aliielezea vizuri sana. Kule Uchaggani wakati aw uchaguzi kulijitokeza ukabila baina yao. Moshi Vijijini inaundwa na Old Moshi, Mbokomu, Uru na Kibosho pamoja na Kahe/Mabogini na TPC. Ukiangalia sana Hawa ni watu wako Enzo Dogo sana kijiographia lakini walikwenda kujiona zaidi waURU au waKIBOSHO! Hakuna sasa ila ukabila katika Hali hii.

Kilichofanyika Zanzibar ni udini tu. Pd Evaristi amefia dini! Ndio maana viongozi wengi aw kiislamu wamekutana na kuanza kujisafisha. Inasikitisha na kukasirisha sana!
 
Mungu nisaidie nashindwa hata kupata usingizi kwa kulifikiria hili.Wakatoliki huu ni wakati wa kuamka toka usingizini.Kumbuka safari ya Waisrael toka misri walipigana na kumwomba Mungu na walishinda.Tunakuomba Mungu utuoneshe njia ya kumaliza mkasa huu.
 
Haya ni matokeo ya kampeni za udini zilizofanywa na viongozi wa ccm kwa ushauri wa tiss wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2010. Watu wenye akili finyu walidhani kuwa wakristu wangepigia kura wagombea wakristu kitu kilichowapa kiwewe na kuanza kuhubiri udini hovyo. Dhambi hii haitawaacha waasisi wa udini nchi hii.

acha kujipofusha. Udini umeletwa na cdm kuanzia kule sumbawanga katika uchaguzi mkuu 2010 ambapo waumini wa kanisa walitengwa na kuvuliwa uumini kwa sababu waliichagua ccm badala ya chadema.
 
Very sad news indeed....May the Almighty GOD rest his Soul in eternal peace. Amen.
 
mungu amlipe kutokana na alichokitenda duniani,si kitu cha kutoa tuhuma tuu na kuanza kuropoka ropoka,hivi kuna taarifa yoyote ilio sema kwamba alie husika ni nani?kama bado unapata ujasiri gani kusema waislam hawwwapendi wakristo?kama hivyo ndivyo jee zanzibar wakristo ni mapadri tuu?mbona hatujasikia kuuwawa au kupigwa risasi mkristo wa kawaida?
jamani huyu ni binaadam ijapokua alikua padri,huwezi jua nini alichokua anafanya nje ya upadri,usikute ana mabifu na watu,lamda jambo limetekelezwa kwa kua watu wanataka uongozi,au limefanywa kwa kisiasa,au kamdhulum mtu,au kuna watu makusudi wanataka kuigombanisha zanzibar na kuitia kwenye mapigano ya wenyewe kwa wenyewe,hebu tuwe watulivu na baadae ndio tusemae wakati tushajua ukweli uko wapi,
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom