Zanzibar: Rais Magufuli amshangaa Dk. Shein kusaini makaratasi ya mtu aliyekataa mkono wake

Zanzibar: Rais Magufuli amshangaa Dk. Shein kusaini makaratasi ya mtu aliyekataa mkono wake

Yule Aliyekuwa Mpaka Leo Hajaamini Kama CCM wana Akili Ndogo (Narrow Minded) Kuliko Hata Kuku Basi Mkutano Wa Leo Unguja na Uzi Huu Unatosha Kumjuilisha Hilo!!!

Kuhusu Rais Shein Kusaini Kwa Ajili Ya Kumpatia Hela Za Kusafiri Nje Ya Nchi, Pamoja Na Matibabu
Muheshimiwa Magufuli Kalizungumza Hili Pale Alipowasoma Wale Hadhira (CCM) kuwa Akili Zao Ni Finyu Kiasi Ya Kwamba Ni Brainwashed na Ni Remote Controlled Kiasi Ya Kwamba Watashindwa Kujiuliza Anasaini Kwa Sheria/Katiba ipi??

Ni Kweli Maalim Seif Alikuwa Ni Waziri Kiongozi, Na Baadae Akawa Makamo Wa Rais!
Kipindi Hicho Cha UwaziriKiongozi/UmakamoRaisi ni Kweli Alikuwa Akisafiri Kwa Kutumia Fedha Ya Serikali Kwa Ziara Zote Za Kiserikali Kwasababu Katiba inamruhusu Kufanya Hivyo.

Lakini Baada Ya Kuachana Na Nyadhifa Zote Hizo Basi Hasafiri Kwa Ziara Za Kiserikali, Bali Anasafiri Kwa Safari Zake Binafsi au Ziara Za Kichama!
Na Safari Hizo Zote Anatumia Pesa/Nauli Yake na Wala Si Kutoka Kwa Shein!

Mheshimiwa Magufuli Usiwachezee Watu Akili Kiasi Hicho Ya Kuwa Shein Atowe Pesa Za Serikali Ampe Seif Akazitembelee Ughaibuni.

Yeye Akiwa Ni Kama Makamo Wa Rais Mstaafu Atakuwa Anazohuduma Zilizoainishwa Kwenye Sheria Ni Lazima Azipate Kutoka Serikalini! Lakini Swala La Kusafiri na Kutibiwa Nje Ya Nchi Hilo Maalim Seif Haitegemei Serikali Kifedha Bali Ni yeye Mwenyewe Anaouwezo Wa Kujifadhili.

Labda ingefanana ungelisima Wewe Muheshimiwa Magufuli na Mheshimiwa Shein Mushirikiane Na Balozi Za Nchi Mbali mbali ili Anyimwe Viza Za Kusafiria Kama itawezekana! Na hilo Ndiyo lililo kwenye uwezo wenu.
wacha uwongo huo.. mara ya mwisho alipoenda matibabu india Serikali ndiyo iliyolipa gharama zote.. Naona una goldfish memory.. kwani hiyo habari ilienea kila sehemu.. tafuta chengine cha kudanganya
 
Rais kasema "Kama mtu anakataa mkono wako nawe kataa mkono wake kwa mambo yake, nikuombe nawe uwe unamkatalia mkono wako kufanye mambo yake' Anamuomba Mungu kumpa walau robo ya moyo wa Shein lakini naye ambae walau robo ya mawazo yake."

Wacha kupotosha watu
Sasa wewe hapa umeleta kitu gani tena mbona hatukuelewi!
 
Kauli kama hizi ndio kauli za kichochezi,mambo ya zanzibar ni heri angetuachia wenyewe wazanzibari kama alivonukiliwa akisema huko nyuma kuwa mambo ya zanzibar hayamuhusu,
kauli hizi zina maana ya kuendelea kupigilia misumari mgawanyiko wa wazanzibari ili kuendelea kuitawala zanzibar "devide and rule"
raisi anasimamisha siasa za upinzani ili kujenga nchi na kauli mbiu ya "hapa kazi tu",sasa hizi siasa za vijembe na kufurahisha wanaosikiliza kwenye mikutano ya hadhara zitajenga nchi kweli
 
Tatizo ni kwamba akifanya mambo haya, ipo siku wataingia madarakani watu wasisaini naye stahiki zake wakati yeye keshastaafu.

What goes around comes around!
 
Nimesikiliza hotuba ya Rais ya JPM akimshangaa Rais wa Zanzibar kuwa anasaini makaratasi ya mtu aliyekataa kumpa mkono siku ya mazishi ya Jumbe, na kusema kwake isingekuwa rahisi hivyo.

Nimejiuliza maswali mengi sana lakini mojawapo likawa ni Je stahiki za Maalim Seif ni za hisani ya rais aliyeko madarakani au ni matakwa ya kisheria/kikatiba?

Na je kama ni matakwa ya kikatiba; JPM anamanisha kwamba Shein avunje katiba kwa kutosaini stahiki hizo? Ama kweli safari ndo imeanza.

Huku tunakoenda sasa siko aisee,
Yaani mtu akikataa kukupa mkono wewe unambania stahiki zake ambazo ziko kikatiba kisa una madaraka??
Kwani huo mkono nao uko kikatiba mpaka ulipize kwa kumnyima mafao yaliyoko kiikatiba??
Anawafundisha nini walioko chini yake??

Mpaka 2020 tutakua tumeona na kusikia mengi sana aisee
 
Alikuwa anatania tu. Nakumbuka alivyotania tufyatue
 
Huku tunakoena sasa siko aisee,
Yaani mtu akikataa kukupa mkono wewe unambania stahiki zake ambazo ziko kikatiba kisa una madaraka??
Kwani huo mkono nao uko kikatiba mpaka ulipize kwa kumnyima mafao yaliyoko kiikatiba??
Anawafundisha nini walioko chini yake??

Mpaka 2020 tutakua tumeona na kusikia mengi sana aisee
Huyu mtu kuna wakati itafika ataamrisha mishahara na vyeo viwe vinapanishwa kwa kuzingatia itikadi za kisiasa
 
Uongozi wa visasi kamwe hauwezi kutibu majeraha ya umaskini tuliyonayo Tanzania.
 
kuongoza ni kazi ngumu sana ndiyo maana mzee jakaya alipoingia madarakani alianza kuota Mvi Mapema.
 
Huyu ana nia mbaya na kuwachonganisha Wazanzibar tu, kauli zake zote ni za ovyo kwa wazanzibar sio za kuunganisha ni za kuwagawa ili aendelee kuwatawala.
Kwako seif anania nzuri ya kuunganisha wazambari
 
Huku tunakoenda sasa siko aisee,
Yaani mtu akikataa kukupa mkono wewe unambania stahiki zake ambazo ziko kikatiba kisa una madaraka??
Kwani huo mkono nao uko kikatiba mpaka ulipize kwa kumnyima mafao yaliyoko kiikatiba??
Anawafundisha nini walioko chini yake??

Mpaka 2020 tutakua tumeona na kusikia mengi sana aisee
ndio maana hajaenda mbeya hawakumpa mkono.
 
Back
Top Bottom