Zanzibar: Rais Magufuli amshangaa Dk. Shein kusaini makaratasi ya mtu aliyekataa mkono wake

Zanzibar: Rais Magufuli amshangaa Dk. Shein kusaini makaratasi ya mtu aliyekataa mkono wake

Ivi Magu alienda kuwaunganisha Wazanzibari kweli ?

RAIS: hakuna mpinzani atatia mguu katika serikali yangu..
(sio kauli ya kibaguzi? lakini kwani Mrema vepe ?au kamsahau ?)

RAIS: huyo aliekataa kisima chake kutumiwa na watu wa chama fulani, mngemtumbukiza kisimani..

Na je aliekataa wapinzani kuingia kwenye serikali yake ?

RAIS: huwezi kukataa mkono wangu halafu nisaini stahiki zako..

Na je waliomzomea Mbeya, ndio atawatenga ?
Sehemu tofauti za hotuba yake zinakinzana sijui anatuma ujumbe gani kwa wanao tafakari hotuba zake.
 
Hakika tumepata Raisi mkweli na wala sio mnafiki kabisa. Raisi mpenda ukweli na mkemea uovu hadharani.
Hii imedhihirika katika Ziara yake uko Zanzibar.

Hakika umeacha somo kubwa sana Zanzibar la kuhusu amani na upendo kwamba baada ya uchaguzi kinachofuata ni kufanya kazi na kuachana uhasama wa kisiasa.

Wako wanaofurahia Zanzibar kuwa sehemu ya machafuko hao ndio wanaopita mitandaoni na kuchafua ile maana yako yakutokuwa mnafiki na kusema ukweli mtupu.

Maraisi wa hulka yako ni wachache sana duniani maana Maraisi wengi haswa wanakuwa madikteta huwa wanadili na wapinzani wao kimya kimya laki ww unamwambia ukweli tena hadharani kwamba wanachotengeneza ni bomo na wao hawastahili.

Hakika Zanzibar somo wamelipata na wamelielewa vizur na matunda yake yataonekana soon.
Hongera sana JPM.

Mwenyekiti CCM JF
 
Mkiona mnakereka sana mjue umasikin hautaki kuwaachia, lakn neema huja kwa maumivu, hivyo tumieni maumivu hayo kuwa fursa mtoke huu ndo wakt wenyew. Wa
Wapinzan nyie mpo wapi kati ya makundi haya? Mosi Protestants, Pili Opposition?? Tafakarin dhana hizo na agenda zake ndo mtajua mnaendesha siasa gan, na hatua za magufuli ni halali yenu.
 


Nimesikiliza hotuba ya Rais ya JPM akimshangaa Rais wa Zanzibar kuwa anasaini makaratasi ya mtu aliyekataa kumpa mkono siku ya mazishi ya Jumbe, na kusema kwake isingekuwa rahisi hivyo.

Nimejiuliza maswali mengi sana lakini mojawapo likawa ni Je stahiki za Maalim Seif ni za hisani ya rais aliyeko madarakani au ni matakwa ya kisheria/kikatiba?

Na je kama ni matakwa ya kikatiba; JPM anamanisha kwamba Shein avunje katiba kwa kutosaini stahiki hizo? Ama kweli safari ndo imeanza.

Stahiki zake zitaingizwa kwenye madeni, kama vile pesa za Wazee wastaafu wa jumuia ya Afrika mashariki. Wapo watu pia wanadai viinua mgongo vyao
 
Hata yeye hajui kuwa sio vyote vizuri anavyovifanya vinatumiwa na wanaompenda tu?
Hata mahasimu wake wanavitumia. Hata Mungu huwanyesha Mvua na wale wa shetani wavune japo watayatumia mavuno hayo kushukuru shetani kuwa kawabariki. !!
Hata kitendo cha kumnyima mtu 'salamu' ni cha kishetani, kina ashiria shari !
 
Kesho twaweza kukutana na;
Mshitakiwa; Maalim Seif
Kosa; Kukataa kutoa mkono
 
Rais anahubiri chuki kiasi hiki? Afrika isahau maendeleo. Mungu hawezi kujalia nchi yenye watu wenye chuki kiwango hiki.
Yeye kugoma kutoa salamu mbele ya hadhira tena msibani mahali watu wanapotegemea kufarijiana hiyo sio chuki !?? .......huwa mnajipa muda wa kufikiri ?
 
Wagawe uwatawale ndio anachofanya. Anataka mafuta ya Zanzibar haraka lazima awakunekune watu fulani ili wamruhusu kirahisi.
Kwani hao walio 'nuna' na hawatoi mikono walipanga hayo 'mafuta' kumpa nani !??
 
Wapinzani humu Jf ni wa ajabu sana
Sefu alipokiuka sheria ya mungu inayosema mpende adui yako kwa kukataa kutoa mkono wake,msibani mbele ya viongozi wa dini mlimsifia,sasa Rais wetu anavunja sheria ya dunia,tutapisha sheria mpya ya mafao,kiongozi akijitoa ufahamu mafao yafyekwe
 
unashangazwa na aliesema naneno tu wala sio matendo mimi nilitalajia ushangazwe na maalim sefu muumini wa dini ya kiislam kukataa mkono wa umuumini mwenzie kwa swala dogo tu cheo huku akijua wazi kwamba ktk kupeana mikono kuna kusemehewa mazambi yao na kupotea chuki baina yao hatimae yaweza kuwa sababu ya mafikio mema
Seif yupo sahihi maana alipokonywa ushindi wake halali wa Uraisi kwaiyo inakuwa inafiki kumpa mkon mtu ambaye ujamsamehe
 
Yeye kugoma kutoa salamu mbele ya hadhira tena msibani mahali watu wanapotegemea kufarijiana hiyo sio chuki !?? .......huwa mnajipa muda wa kufikiri ?
Juzi Mamvi kampa mkono JPM wamempongeza na kumpamba sana, ila Maalim anapongezwa kwa tendo lake lisilo la kiungwana. Looh, huu uungwana hata hauleweki. Natamani enzi za Komando Salmini zirudi, ndipo mziki ungekuwa mtamu.
 
KWAHIYO UNASEMA KUWA KWA KAULI HIYO YA RAIS BASI NCHI INAKWENDA KUANGAMIA...IS IT?

HILO NDILO AMBALO MMEONA LINAANGAMIZA NCHI NA SUALA LA SEIF KUTOMPA MKONO RAIS SHEIN MLIONA NI JAMBO LENYE KHERI KWA MUSTAKABALI WA NCHI.

RAIS WETU MPENDWA MARA NYINGI AKIWA ANAZUNGUMZA HUWA PIA ANAIFURAHISHA HADHIRA YAKE KWA KUCHOMEKEA MANENO YA UTANI...NYIE BAVICHA MNAKAA ATTENTION KUSIKIA KAULI GANI ANAITOA MJE KUPOTOSHA HAPA KWA KUSEMA ANAMAANISHA....

RAIS JPM TUNAMFAHAM VIZURI NA TUNAIFAHAMU DHAMIRA ALIYONAYO KWA TAIFA LETU YA KUONA KILA MTU ANAISHI MAISHA MAZURI YENYE MATUMAINI. KUWEPO WATU WA KUMPINGA NA KUPOTOSHA HAIEPUKIKI KWAKUWA WAPO WATU AMBAO DHAHIRI HAWATAFURAHISHWA NA NIA YA SERIKALI YAKE YA KUPAMBANA NA RUSHWA NA UZEMBE KAZINI. WATU HAO NI WACHACHE UKILINGANISHA NA WANYONGE AMBAO TUKO WENGI NA TUNAMUUNGA MKONO...
Kumbe alikuwa anatania.sikujuwa
 
Back
Top Bottom