Ziara ya Rais Samia nchini Kenya, Mama anakosea

Ziara ya Rais Samia nchini Kenya, Mama anakosea

Labda diplomasia ya kuvaa ushungi.
Punguza chuki mkuu, usije ukapata presure au ugonjwa wa moyo bure!!!
haya maisha ni mapito tu.

Pia kumbuka kuwa binaadamu wote ni sawa tu mbele za Mungu hivyo hatuna sababu ya kuchukiana au kudharauliana.
 
ulitaka tuuze wapi gas mzee, manake hata tusipowauzia sisi wao wanaweza kuuziwa na wengine. unataka gasi tuifanyie nini mzee. yaani unapata mteja kununua gas afu unasema unaogopa kumuuzia asije kukupita kiuchumi? akili au matope.
Matope hasa.
 
Baadhi ya wanaJF wanamchukulia Mama kama Rais ambaye anaingia ofisi ya URAIS akitokea kwenye uchaguzi. Jueni kuwa mama ana UZOEFU wa miaka 5 kama Makamu wa Rais.

Amehuzuria mikutano mingi sana ya Kimataifa inayohusu mambo ya kibiashara na uchumi akimuwakilisha Rais, hivyo ana uzoefu wa kutosha. Nawaomba wanaJF tumwamini natum-support na tumpe muda. ANAWEZA NA ATATUVUSHA SALAMA
 
Napenda kuandika kidogo tu kulingana na uwelewa wangu juu ya Ziara ya Mama nchi Kenya na mikataba mlio tiana sign.

1. Ujenzi wa bomba la gas kutoka Tanzania kwenda Mombasa kwa ajili ya matumizi ya viwanda nchini Kenya,hapa mama unefail pakubwa sana maana yake nikwamba bidhaa za Kenya zitakuwa zinazalishwa kwa gharama nafuu zaidi na kuteka soko la Africa Mashariki kuliko Tanzania. Tutarudi miaka ya nyuma tena kila kitu Made in Kenya...

1) hakunaga kitu kinaitwa surplus, biashara ni game of opportunities + risks!

a) sera ya viwanda its impossible kwa tanzania wakati mnahubiri ajira, magufuli alitia watu moyo viwanda mkamkejeli sasahv mnalalamika nn? endeleeni na maombi ya ajira acha wakenya waje kuwekza arifu.

b) nyie ndo mlikua mstari wa mbele kulalamika hatuwawekei wawekezaji mazingira mazuri ya kuja kuwekeza, sasa acha mama ajenge mahusiano mazuri waje kuwekeza kama unavojua kenya wamewekeza bil 1.5 mpaka sasa tanzania na waendelee kuja mpaka muelewe magufuli alikua anazungumza nini.

2) Air tanzania mmesema ndege zote ziuzwe, kama haukuemo usiniquote vibaya!

3) soko la utalii watanzania wananufaika kwa ajira tu toka tumepata uhuru, mkiambiwa mjitahidi kuwekeza mnapoweza mnalalilia ajira
 
Hayo maneno ya mkosaji !!fikra za miaka ya 50!!, wanawake wameongoza wazungu na kuleta maendeleo makubwa itakuwa kwa mwafrika, tena mtanzania?!!huyo mwanaume aliyeongoza miaka mitano , maendeleo gani ameyaleta?hao kina mseveni, mugabe, derby, biya, sasongweso zaidi ya miaka 30, madarakani walifanya nini?!acheni hizo muhukumuni mtu kwa uwezo wake na sio JINSI, yake.MAMA KANYAJA TWENDE,
Mwambie huyo mjinga! Nani anaongoza Germany, Scotland, Newzealand ? Nani anaongoza WTO, IMF?
 
Ndiyo maana nimesema tuna viongozi wasiokuwa na maono.
Umetoa mfano wa Korosho, sasa hebu jiulize, ingekuwaje kama tungekuwa na kiongozi mwenye maono na akili akahakikisha nchi inakuwa na viwanda vya kuchakata Korosho, na kisha Korosho hiyo tukaiuza kutokea Tanzania kwenda kwa walaji moja kwa moja?

Tukija kwenye issue ya Gesi, kwanini viwanda vyetu visipewe kipaumbele kwanza kabla ya kuiuza kwa majirani zetu?
Viwanda vya kubangua korosho tulikuwa navyo wakati wa Nyerere lakini kwa sera zetu za kijamaa na kukosa menejimenti vilikufa by early 1990s.

Hatuwezi kurudia kuvifufua na ku iendesha kama Serikali, Ila ni fursa kwa Sekta binafsi kujishughulisha na unanguaji korosho. Kazi ya Serikali inabakia ni kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya biashara kustawi.
 
Magufuli na Kikwete nani aliua uchumi. Au ule uchumi wa madawa ya kulevya ndiyo mliona maendeleo. Mpende msipende hakuna raisi wa TZ ambaye aliupandiksha na kuukuza uchumi kama Magufuli. Mnaweza mkamchukia lakini alitutoa chini kabisa na kutufikisha uchumi wa kati. Hata Nyere hakuweza hilo. Leo hii ingekuwa bado awamu ya NNE hata mawaziri na viongozi wakuu wa serkali wangekuw wamekwisha kuwa MATEJA.
Uchumi wa kati[emoji1787][emoji2][emoji1787]
 
Hili suala la kuweka restriction za corona na kujipendekeza kwa watu sijajua mshauri ni nani, inatuletea picha ya udhaifu! Akimaliza hii ya Magufuli, itakuwa ngumu sana mimi kumpigia kura, niwe mkweli, nachukia udhaifu dhaifu kwenye uongozi! Tunarudi tena enzi za msoga sasa.

Mama anakwenda vizuri. Atasifiwa na kina bashiri, chakubanga au dotto mlipa mapesa kweri?

Mama mitano mingine inamhusu sana ila atushawishi kwenye haya:

1. Kupatikana kwa ripoti sasa ya CAG kuhusu BOT na TPA.
2. Kupatikana sasa kwa ripoti ya wataalamu kuhusu Corona.
3. Kuchukuliwa hatua stahiki kuhusiana na ripoti za CAG.
4. Kushughulikiwa bila kuangalia makunyanzi kwa yale magenge yaliyotaka kuuhujumu na kuuzima urais wa mama kihayawani.

Akiyaweza hayo - mitano mingine itamhusu mama kutoka kwa kila mtanzania na hasa kutoka kwa kila mzalendo.
 
Unatazama kwanza hicho unachokiuza ni kwa gharama ipi. Sio tu kwasababu hakina mahitaji kwa sasa basi ukamua kukitoa sadaka na ukasahau baadae.

Gesi kwa sasa ni nishato nyeti sana kwetu sisi watanzania. Hatutakiwi kuigawa kama tunagawa njugu. Hebu fanya utabiri wa matumizi ya miaka ijayo ya nishati ya gesi kama chanzo cha nishati mbadala...
Unaposema kugawa gesi una maanisha nini? Kwani hao wakenya wanapewa bure?
 
Kwanza unapelekaje gas kenya wakati watanzania wenyewe haujatusambazia ;hii kweli nchi ya ahadi
 
Tawiree!
Aliyekufundisha uchumi kwamba unauza kitu nje ya nchi tu iwapo una "surplus" mwambie amekudanganya. Comparative advantage na monopolistic competition ndio msingi wa biashara ya kimataifa unaotumika sasa. Na ingekuwa hivyo usemavyo, basi dunia asingeweza kuishi mtu.
 
kwani gas anapewa bure...?

Urusi anauza gas karibu ulaya yote..

sioni kibaya labda kama tunampa bure.
 
hapo kwa hilo la gas bila kupepesa macho tuambiane tu ukweli ameteleza: zaidi ya hapo atupe maelezo yeye amelenga wapi?
 
mbon nimeskia nkataba wa ges ulikua wa muda mrefu mazunguO yanaendelea walichofanya ni kumalizia kuweka dole.je unah hakika gan hii haikua plan toka en ya wamu ya tano.?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwani gas anapewa bure...?
Urusi anauza gas karibu ulaya yote..

sioni kibaya labda kama tunampa bure...
warusi wenyewe wanashida ya nishati kama sisi?
na hata kama unauza, sio bure sawa ila ndo unauza mpaka kitu unakihitaji tena sana
 
Sasa unajua aliyetaka kumpa Dangote gesi ni nani na aliyemnyima ni nani?

Bomba lilishafikishwa mpaka Mita chache karibu na kiwandani. Rais wenu aliyefariki ndiye alikataa asipewe gesi bali pale pajengwe Substation uzalishwe umeme, yeye auziwe umeme na umeme mwingine utatumika kwenye viwanda vitakavyojengwa pale kwamaana palishatengwa kama Industrial park kwa Mtwara. Kwahiyo makosa ya mwingine asipewe Mama Samia, labda yeye atarekebisha, who knows!!

Aya nitajie kiwanda kingine kilichohitaji gesi kikanyimwa!!
Si ndio nikasema hakuna alienyimwa, wote wamepewa 💯
 
Back
Top Bottom