Ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan - Zanzibar, leo Septemba 2, 2022

Ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan - Zanzibar, leo Septemba 2, 2022

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan - Zanzibar, leo Septemba 2, 2022



Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Hamad Masauni amesema kuwa kupitia mfuko wa tozo, Wizara ya hiyo inajipanga kujenga vituo vya polisi na makazi ya askari 51780 nchi nzima.

Mpango wa awali wa wizara hiyo ilikuwa ni kukamilisha mchakato huu kwenye kipindi cha miaka 10 lakini kutokana na uwepo wa vyanzo vipya vya mapato (tozo ikiwemo), sasa wataukamilisha ndani ya miaka 3 ya mwanzo ya uongozi wa awamu wa sita.

Aidha, Mhe. Masauni amesema mapendekezo ya Rais aliyoyatoa moshi kuhusu kutatua changamoto ya matumizi mabaya ya fedha kwenye idara ya jeshi la polisi, wao kama wizara wameanza kuchukua hatua ikoiwemo kuhamisha fedha za mfuko wa "kufa na kuzikana" kwa kuzipeleka kwenye Shirika la bima ya Taifa ili walipwe kutoka huko.

Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa kituo cha Polisi Mzimkazi, Jimbo la Makunduchi, Kusini Unguja ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alikuwa mgeni Rasmi.
 
Aisee..hapo anaamini huku nyuma amewaacha "wanae" wanarekebisha mambo kuhusu malalamiko ya tozo.

Madaraka ni mazuri sana ukiwa na akili nyepesi huku ukitawala wajinga.
COUNTER ATTACK ambayo mzee wa tozo atampiga huyu mama 2025 maji ataita mmaaa!
 
Rais mchapa kazi anayewaza kuwatumikia watanzania muda wote,Anawaza kuwainua kiuchumi watanzania, Anawaza kugusa maisha ya watu na kuwapa unafuu wa kimaisha wananchi, Mama Samia Suluhu Hassan Ni zawadi kwetu watanzania
 

Attachments

  • IMG-20220831-WA0012.jpg
    IMG-20220831-WA0012.jpg
    47.6 KB · Views: 2
Uzuri huku kwetu hatulipi TOZO. Wakazi wa Mchamba-wima na Mwembe-mchomeke wamefurahia Sana ziara hii
 
Tunajenga ikulu ya JMT pamoja na ofisi ya Waziri Mkuu.

Zenji kuna nukia bweche tu.

Ngoja nitafute kiwanja huko Bujuu.
 
Back
Top Bottom