Zielewe kazi za Usalama wa Taifa (TISS) na mipaka yake

Huu uzi ukitoboa mpaka saa kumi na mbili na nusu jioni, mniite mbwa... Nimekaa paleeeee 😂
Ujuwe kwamba yanayoandikwa hapa yapo hata kwenye mitandao, ukiwamo mtandao wa serikali. Ukitukana viongozi badala ya kujadili hoja utaharakisha kusudio lako la kuitwa jina tofauti.....
 
NATAKA nijunge usalama nafanyaje kaka
Vijana bana! 😂 hapo usikute anajidanganya wale wanaokuwaga kwenye misafara wanafaidi sanaaaa! Au wana mapesa sanaaaa! Au kuna watu anataka awavimbie, awalipe visasi au wamuogope... Wacha upumbavu! Hao watu ni Choosen from god!

Haipatikani hiyo status kizembezembe! Concentrate na mambo mengine
 
Hahaha sio kweli, mbona hatusikii walioacha? Usichanganye askari kanzu na usalama. Askari kanzu anailinda jamii dhidi ya jinai usalama anailinda dola dhidi ya watu wenye akili za juu sana.
Mbona wengi siku hizi hawana akili hizo za juu. Wako idarani sababu ya undungu na kujuana? Wanawezaje kuilinda dola sasa?
 
Ngalikihinja njoo usome, usiogope manyoka...
Kwa kuongezea Wakurugenzi wa Mashirika ya umma kama si wote ni Usalama. Shida ya sasa, baba akiwa usalama anapachika na watoto wake au ndugu.
Ndiyo maana mambo ya Idara hii iko tofauti na zamani. Ile ya kuwatafuta watu makini toka Sekondari na vyuo, watakuwa wachache nowadays ni ndugu ili mradi umefika form six.
 
Kazi ya usalama haina umuhimu sana Kwa Nchi kama Tanzania.Maana yeye ni kushauri tu basi na ukizingatia rais Kwa Tanzania anaweza kupokea ushauri wako au akaukataa kutegemea yeye anachopenda Kwa mujibu wa Sheria.kwa Tz Kila kitu kinategemea rais anajisikiaje kuamua jambo na siyo mifumo.
 
pesa zinatoka sana nchi inaliwaliwa we mpaka tunakuja kusikia watu wameweka pesa kwenye magunia hiyo idara inafanya nini..?
mara EPA mara escrow, mzee magu aliwatumia vilivyo wakati wake maana hii dhana ya wawekezaji ni nzuri lakini deep down ni tunanyonywa sana!.. hiyo idara kazi yake nini na makampuni yakigeni yaliyowekeza yanaleta janjajanja..??

kama kuna vitu wanashindwa kuitaka serikali ifanye basi wajue hawana nguvu! mfano wakitaka sheria fulani ipitishwe bungeni ili kuondoa changamoto ya wao kufanya kazi nakulinda masirahi ya taifa!,wakishindwa kufanya hivyo basi wao si lolote!!.
Nitaendelea kuwalaumu kwasababu si kwamba sikubalianinao ila nahitaji waichape kazi yao vyema natuone matokeo,maana ukisema wanaleta amani ndio amani ni muhimu lakini baada ya amani maisha mengine yanatakiwa yaendelee,amani ambayo haitakuletea tija ni sawa na uchawi tu!.

kama pia wanashindwa kuingilia uchumi wajitafakari uchumi ni jambo nyeti sana kwenye nchi yoyote,aibu kwa Tanzania kunyanyasika kwaajili ya sukari aibu sana!,halafu vipi hamuioni hiyo dollar inavyorarua pesa yetu..??
najua hakuna nchi isiyokosa changamoto lkn kuna changamoto ni changamtoto! miaka 60 nakenda ya uhuru uchumi wetu hautakiwi kuwa hapa!.
sasa someni halafu mkalale tena usingizi wa pono!
 
Angalia sana....jambo zuri info nzuri....usiende mbali zaidi watakusumbua hao jamaa....zako najua ni jambo.la familia...@ chahali ....
 
Zaman za kale
 
Mkuu mleta mada, bandiko informative kama hili halafu unashindwa ku-cite legal authority yoyote ili kusupport na kuverify narration yako?!

Anyway, ngoja nimuite mkuu Eagle girl aje hapa kusabahi wananzengo. 😎

-Kaveli-
Mkuu, Kama kila bandiko natakiwa ku cite legal authority sasa elimu, na ujuzi wangu una maana gani kichwani mwangu? Sijaandika kupata academic credits au journal article ninayotakiwa kuichapisha kwenye scientific journal.

Unachotakiwa kufanya ni kuingia library au kwenye mitandao ya serikali mbalimbali ili uje ukanushe nilichoandika kupitia maandiko ya wengine. Vinginevyo nilichoandika hakijapata mpinzani hadi sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…