Zifahamu athari za kunywa maji kupita kiasi

Zifahamu athari za kunywa maji kupita kiasi

Habari wana JF,
Wakati mwingine tunapojadili au kutafsiri maandiko ya watu ni vyema kuweka chanzo cha makala husika na au kuweka wasifu wa mhusika.

Mimi si mtaalamu wa sayansi ya unywaji maji ila ni mtaalamu wa afya/daktari LAKINI naona kuna maelezo yanayotolewa kwa jumlajumla bila tahadhali yoyote. Hii inaweza kuwabadili watu kutoka kwenye jambo jema kiafya na kuwapeleka kwenye hali tata kwa kuogopeshwa na maelezo waliyoyasoma.

Suala la unywaji maji hutegemea vichocheo vywa mwili ambavyo humpa taarifa binadamu/mnyama juu ya uhitaji wa maji/kiu. Upataji wa kiu hutegemea zaidi na size ya mwili wa mtu, hali ya hewa, aina ya kazi au mazoezi na utimamu wa vichocheo husika vya mwili juu ya utoaji taarifa ya kiu.

Ni kweli kwamba unywaji wa maji mengi unaweza kuwa na madhara kwa mhusika kutokana na moja kudilute kiasi cha madini yaliyoko mwilini lakini pia kutokana na mfumo wa mzunguko wa damu kuwa hauna nafasi ya ziada ya kubeba kiasi cha maji yaliyonywewa basi unaweza kusababisha kujaa kwa mfumo/overload.

Madhara tajwa hapo juu huweza kujitokeza zaidi pale binadamu au mnyama anapotundikiwa maji/drip. Lakini kutokana na mfumo wa mrejesho hasi/feefback kwa upande wa anaekunywa maji si rahisi kusababisha hilo labda tu kama mfumo wake wa kuondoa kiu na kuridhika/satisfaction utakuwa una shida.

Kitaalamu kwa siku, inakisiwa kisayansi kuwa kwa ujumla (jasho, kupumua, choo kikubwa, kuongea pamoja na mkojo) vinasababisha kiwango cha maji lita moja na nusu kutoka mwilini. Njia ipi hutoa zaidi, hutegemeana na hali ya mazingira husika
Hivyo ni vizuri kurudisha kiasi hiki cha maji mwilini japo si kwa wakati mmoja.

Ni kweli kwamba kadri unavyokunywa maji ndivyo mwili utakubali kutoa maji kama jasho au mkojo. Na kadri usivyokunywa maji ya kutosha ndivyo mwili hautayatoa hayo maji, hii haimaanishi kuwa uko salama zaidi au na afya njema bali mwili unang'ang'ania maji hayo kutokana na kutokuwa na maji toshelevu. Hivyo, kama ukipata choo kitakuwa kigumu, mkojo utakuwa ni wanjano/concentrated, jasho kidogo na lenye chumvi nyingi. Hii ni hatari kwa afya kwani mwili utabakiza uchafu mwingi mwilini kwa kukosa maji ya kuandamana na huo uchafu.

Nini kifanyike?
Tii kiu yako, kunywa maji kwani mahesabu mengi hayazingatii hali ya mazingiira uliyopo ambapo kila mmoja huitaji ku-adjust kulingana na hali yake na mazingira. Isipokuwa kwa wale wenye shida maalumu kama matatizo ya digo nk.

Pale unapoona wewe unakunywa maji mengi kupindukia kuzidi watu wanaokuzunguka, fika kwa wataalamu wa afya wakufanyie uchunguzi kwani matatizo ya vichocheo tajwa hapo juu yapo.

Kunywa maji kwa afya.
Good comment, ila hujashauri kwa wastani kiasi gani cha maji kitumike kwa mtu mzima tuliyopo ktk Tropical Countries
 
Good comment, ila hujashauri kwa wastani kiasi gani cha maji kitumike kwa mtu mzima tuliyopo ktk Tropical Countries

Sayansi inaeleza kuwa jumla ya upoteaji wa maji kwa siku ni lita kwa wastani ni lita 1.5, lakini hii inaweza kuongezeka zaidi au kupungua kulingana na:
-ukubwa wa mwili
-aina ya kazi
-mazoezi
-hali ya hewa/mazingira
-joto la mwili wako/mgonjwa
-uwepo wa magonjwa mengine yanayoweza kuathiri matumizi ya maji mwilini

Ukizingatia tu baadhi ya vitu tajwa hapo juu, huwezi kutoa jibu la jumla kwa kila mmoja anywe maji kiasi gani kwa kuwa yuko kwenye eneo la ki-Tropic. Ingawa, cha kwanza ni kurudisha hiyo lita 1.5 kwa siku kama wastani wa kwanza.
Kwani kila mmoja kwenye eneo tajwa bado anaweza kuwa na mazingira tofauti ya mwili wake na shughuli.

Mfano:
  • mfanyakazi anaeshinda kwenye chumba chenye air condition.
  • machinga anaeuza kanga juani
  • mkulima anaeshinda shamba
-mfanyakazi kwenye mazingira ya boiler
nk.

Kila mmoja atahitaji adjustment/ongezeko kulingana na sababu mbalimbali zinazofanya kuongeza au kupunguza utoaji vs uchukuaji wa maji yaliyopungua.

NB: Kama hauna shida yoyote kiafya, wewe tii kiu yako na kujenga mazoea ya kunywa maji, feedback mechanism ya mwili ipo kukulinda kama kitoshelezi cha mwili kimefikiwa.

Pia ukitaka kuwa na uhakika/precisely unaweza kumwona mtaalamu aliyekaribu nawe umweleze aina ya kazi na vyote unavyochukua kwa siku kama vinywaji na chakula ili kuwa na uhakika ni kiasi gani uchukue.
 
Back
Top Bottom