Kwahiyo mzizi wa tatizo hapo maana yake ni wanaume waache kurubuni mabinti wakiwa bado wadogo siyo?
Nafikiri wewe umenielewa
Jadda Yupo poorly trained eneo la mahusiano plus anaonekana kuwa over spoiled yenye mchanganyiko wa Daddy issues. Mitazamo yake mingi ni copy and paste ya eurocentric feminist agenda propaganda,hanaga tija ya kijinsia eneo la uafrika.
Hivi mnajua ninyi mna matatizo sana, kwahiyo mwanamke akikosoa wanaume ndio ana shida kwenye mahusiano na malezi yake, ila mwanaume akikosoa wanawake ndio yuko sahihi na anataka jamii ibadilike hivi huwa mnatumia nini kufikiri
Shida yako unamtazamo kama wa kifaru kila jicho lina upande wake ila anafosi kutazama kwa macho yote kwapamoja kuelekea direction moja. Nani aliyekwambia tunabadili maneno?
Ni kweli wanawake wanaochezewa wengi wao hawaolewi wanaishia kuwa masingle mother au wasimbe for life at yhe the same time wapo wanaochezewa na kisha kuolewa na ndoa zao hazina maisha marefu sababu hakunaga mwanaume atadumu na Mwanamke ambaye amechezewa sana na hata wakiwa ndoani basi huputia magumu kama matokeo ya historia zao
Ndio mmebadili maneno kwa sababu wimbo wenu wa kila siku ni kwamba generally mwanamke aliyechezea usichana wake haolewi kabisa, baada ya kuambiwa kwamba wapo wengi tu wanaoolewa mkahamisha magoli na kusema ndio wanaolewa ila ndoa zao hazidumu, baada ya kuambiwa wapo ambao ndoa zao zinadumu mkahamisha tena magoli na kusema ndio mnawaamsha wanaume wenzenu ili waache kuoa wanawake wasiojitunza unaona sasa namna mnavyo hamahama kwenye hoja zenu
Hili swali limeshajibiwa na mleta uzi kama umesoma vema stages alizoongelea. Binti akiwa mdogo anataka uhuru ili kupata vitu vinavyokuja kama hongo kutoka kwa wanaume plus anakuwa anataka kuexplore maisha ya usichana kama matokeo ya kukosa muongozo wa namna ya kujipanga na maisha ya baaae
Mimi sidhani kama kutaka uhuru ni kosa kwa sababu tunaambiwa kila binadamu ana haki ya kudai uhuru wake mradi hamdhuru mtu wala havunji sheria za nchi, kwani ninyi wanaume ni nani anayewabana kuwa huru mbona ninyi mnafanya mambo yenu na starehe zenu huko na hakuna anayewasimanga kwanini akifanya mwanamke iwe nongwa, najua utasema nahamasisha wanawake kushindana na wanaume ila hayo ni mawazo yenu tu kwanini kila jambo analofanya mwanamke inaonekana kama anataka kushindana na wanaume na siyo kwamba anataka tu kuifurahisha nafsi yake
Tunaposema wanawake hawataki kuwa accountable tuna maanisha kukwepa sehemu yao ya lawama ya matokeo ya matendo yao. Mwanamke asipolaumiwa na kusemwa matokeo yake anahisi yupo sawa ila matendo yake yanakuja kuigharimu jamii nzima. Kumuacha mwanamke afanye anachojiskia ndio chanzo cha haya majanga ya sasa ya magonjwa ya zinaa, watoto haramu,usingle mother na kadharika.
Ndio maana nikakuambia ambao hamtaki kuwa accountable ni wanaume ninyi ndio ambao mnakwepa lawama ya matokeo ya matendo yenu wanawake sidhani kwamba wanakwepa hizo lawama bali wanataka muwajibike wote, wanawake wameshasemwa sana na kuona kwamba wao kufanya ngono ni kosa lakini bado hayo maovu yanaendelea unadhani sababu ni nini hapo, ni kwa sababu jamii imemuaminisha mwanaume kwamba yeye kufanya ngono ni sawa hivyo hata akitembea na wanawake na kuwaacha hatapata madhara lakini mwisho wa siku madhara ndio hayo tunayaona ya wanaume kukutana na limited supply ya wanawake waliojitunza pale wanapotaka kuoa
Unaposema tunawalaumu wanawake its like unaongelea general population ya wanawake wakati sisi tumetarget a certain group of individuals ndani ya population ya wanawake,why sasa upo concerned kuwatetea badala ya kuobserve shida ipo wapi?
Wewe unaweza kudhani kwamba unatarget a certain group kumbe hiyo certain group ni zaidi ya asilimia 90 ya wanawake wote sasa hapo si ni sawa tu na kuwalaumu wanawake wote, au wewe kwa dunia ya leo ni mabinti wangapi wanaofikisha miaka 25 wakiwa bado na bikira zao yani mara nyingi ukikuta binti bado ana bikira basi ujue hayuko tayari kuolewa, narudia tena mimi siwatetei wanawake bali hoja yangu ni kwamba wote wanawake na wanaume wana makosa na wanapata madhara tofauti na ninyi ambao mnalazimisha kwamba wenye makosa na wanaopata madhara ni wanawake tu
Again, usichokijua ni sawa na usiku wa giza nene. Usichojua ni kuwa mabinti siku hizi wanajitongozesha ili kuweza kupata kitu kwa mwanaume,imekuwa ni biashara huria. Sasa unaongelea as if tupo miaka ya 1920 nyakati ambazo wanawake walikuwa hawawezi hata kumtazama mwanaume usoni kwa haya. Ila sasa mtoto wa kike wa miaka 16 yeye ndie anakutongoza na kutaka ukamle ili uwe sponsor wake. Sasa ukinikatalia hapa nitakuuliza wewe unawajua vipi wanawake eneo la ngono?
Aise kumbe hadi mabikira nao wana uwezo wa kuwatongoza wanaume ili wakaliwe sasa kama ni hivyo hiyo decency ya mabinti wenye bikira iko wapi, ikiwa hata wao wana uwezo wa kuingia kwenye mahusiano na wanaume kwa ajili ya tamaa tu, maana mimi nilidhani mabinti bikira wanasifiwa kuwa wanafaa kuolewa kwa sababu ni naive na wako decent
Lakini kumbe nao wanaweza kuwa micharuko hata kabla hawajakutana na wanaume sasa huoni kama kwa kauli hiyo umefuta sifa zote nzuri za mabikira na kuonekana kitabia hawana tofauti na wanawake waliotumika, anyway kama kweli kuna mabikira wanatongoza wanaume kwanini na ninyi wanaume msifanye kile ambacho mnataka wanawake wafanye, ninyi si mnasema mwanamke akitongozwa ni maamuzi yake kukubali au kukataa halafu hapa unasema kuwa kuna wanawake nao wanatongoza wanaume ili wakaliwe
Sasa kama kweli ninyi wanaume mngekuwa mnataka jamii isiharibike kwanini msivikatalie hivyo vibinti vinavyowatongoza ili vitunze hizo bikira zao, kama ninyi mnaona ni ngumu kwenu kukataa vishawishi vya wanawake kwanini mnalazimisha kwamba ni rahisi kwa wanawake kukataa vishawishi vya wanaume, wewe lini ulishawahi kuwa mwanamke ukajua kwamba ni rahisi mwanamke kukwepa vishawishi vyote vya wanaume kwa miaka yote hadi atakapoolewa
Nimekuuliza kule juu kuwa unafahamu kuwa wanawake hao bikra unaowaongelea unajua kuwa hizo bikra huwa wanawapa a very small percentage ya wanaume katika general population ya wanaume?
So how can you be serious kusema wanaume wanalaumu wanawake wanaowatoa bikra kwa kutokuwa bikra? Hivi mfano darasani,kazini au hata mtaani,wanaume wenye mvuto huwa ni wengi kuliko wasio na mvuto? Unadhani mabinti huwa wanakimbilia kundi gani kati ya wenye mvuto na wasio nao?
Mimi nimekuambia fafanua ni kwa namna gani idadi ya wanaume wanaotoa bikira za wanawake ni ndogo kuliko idadi ya wanaume wasiozitoa, kwa mantiki hiyo unaniambia kwamba kuna wanaume wao asilimia kubwa ya wanawake wanaotembea nao ni mabikira huku wanaume wengine wakizikosa kabisa, hapo uliposema kwamba wanaume wasio na mvuto hawatoi bikira za wanawake ni uongo wa mchana kweupe nenda karudie hiyo research yako
Inaweza kuwa swala la Bikra kwao hawajalipa kipaumbele sababu ya nature ya wanawake wao ni wawazi na wakitia boko wanakuwa wawazi tofauti na nyie wa huku utapeli mwingi na uongo. But,wanawake wa magharibi vipaumbele vyao ukilinganisha na wa huku dunia ya tatu wanatofautiana.
Sasa hapa unajaribu kusema nini mbona kama unajizungusha tena kwani hoja ni wanawake kuwa wawazi au kutumika, kwani mwanamke akiwa muwazi ndio inabadili ukweli kama katumika au akisema afiche ndio inabadili nini, hoja ni kwamba bikira siyo kipaumbele kwa wanaume wa kizungu sababu wanajua wao ndio walioshiriki kuzitoa hizo bikira
Hayo ni maoni yako binafsi but wapo wanaoishi hivyo na wapo wanaoishi kwa mfumo wa mke kukaa nyumbani kufanya majukumu yake kama kawaida (traditional wives).
Wewe hujanielewa hoja yangu mimi sijasema kwamba wazungu wote wanaishi mfumo wa 50 50, ila nimesema ukikuta wanaoishi huo mfumo basi huwa wanagawana majukumu yote pasu kwa pasu hakuna cha kusema haya ni majukumu ya mwanamke wala haya ni ya mwanaume, lakini wale ambao wanaishi huo mfumo wa mke kukaa nyumbani maana yake mke atafanya majukumu ya nyumbani na mume atafanya majukumu ya kiuchumi
Nilikugusia hiyo point ili kukukata wenge kwenye issue yako ya kuhoji wanaume huwa tunalalamika wanawake kuwa magoli kipa lakini mkitoka kutafuta tunalalamika tena ndio nikasema wenzenu wanatoka ila hawana 50/50 na wanaume zao wanakwenda 100% kwenye majukumu ndani ya ndoa na mahusiano bila kutegea wala kuvizia. Wakati ninyi huku mnataka 50/50 ya mdomoni ila mkiachiwa mlipie watoto bili mnaona kuonewa na mnaleta dharau plus kutaka kujitenga na mwanaume ili muishi wenyewe. You can't have you whole cake 🎂 and eat it at the same time.
Ndio maana nikakuambia wenzetu huko 50 50 yao imenyooka na inaeleweka wanagawana majukumu yote ya nyumbani na ya kiuchumi pasu kwa pasu hawategeani, sasa ninyi huku mnataka majukumu ya mwanaume tu ndio yagawanywe pasu kwa pasu ila ya mwanamke aahh yafanywe na wanawake wenyewe hapo ndipo wanawake wanapowaona wababaishaji, shida ni kwamba wanaume wa kiafrika hamtaki haki sawa ila mnataka majukumu sawa tena ikibidi mwanamke afanye zaidi kwani ni wanawake wangapi leo hii wanafanya majukumu ya wanaume halafu linganisha na idadi ya wanaume wanaofanya majukumu ya wanawake
Sasa wewe aliyekwambia ukijitegemea kiuchumi kama mwanamke ndio tiketi ya kumkosea adabu mwanaume au kutomheshimu ni nani? Hii ikupe tu taswira ya namna ulivyo inferior.
Hivi wewe ambae unahisi ukiwa na financial power then kumtii mwanaume wako na kumheshimu inakuwa ni option una tofauti na mwanaume ambaye ana amini akiwa anafinance kila kitu kwenye ndoa then anatakiwa kumtreate mwanamke wake kwa dharau na kumuona kama punda na kutompa upendo wa mke? Unaona jinsi gani ulivyo mweupe eneo la uelewa wa how relationship ina fanya kazi?🤔
Tofautisha kati ya kumkosea adabu mwanaume na kutofuata matakwa yake usichanganye hivi vitu kumkosea adabu ni kama kumfokea au kumtukana lakini mimi hoja yangu ni kwamba utii wa mwanamke kwa mwanaume unajengwa kwa misingi ya mwanaume kumhudumia mwanamke na si vinginevyo, kwahiyo kama mwanamke anajitegemea kiuchumi kunakuwa hakuna sababu tena ya mwanaume kumtawala huyo mwanamke kwa sababu mamlaka aliyonayo mwanaume juu ya mwanamke yanatokana na wajibu alionao juu ya mwanamke huwezi kukitawala usichokiwajibikia, hilo lina tofauti kubwa sana na mwanaume kumnyanyasa mkewe eti kisa anamhudumia hilo ni kosa kwa sababu mke siyo kwamba anahudumiwa bure bure tu naye ana majukumu yake ya nyumbani ambayo mwanaume hawezi kuyafanya kwahiyo hata kama mke hatafuti pesa basi anahudumiwa kwa sababu ya majukumu ya nyumbani anayoyafanya hivyo anastahili kuheshimiwa walau kwa hayo
Hakuna uhalisia unaoongea ninachoona unaunda unda vipande vya scenario tofauti ili ujenge picha ya uhalisia wako binafsi kama director wa bongo movie.
Hiyo ni picha uliyo nayo kuhusu imaginary man katika maisha yako na mitazamo yako. On average wanaume wa sasa hadi anafika miaka 35 ukitoa wanawake wa kununua kama makahaba na wale wa kupiga kimasihara,unakuta hajawahi hata kubahatika kuchezea mwanamke sababu ili apate hiyo chance inabidi awe na leverage ya kuwashika kiakili, anapata wapi hiyo nguvu na hana pesa kama akina diamond platinum (who is the perfect example and a fit for this narrative umeleta hapa). So hii hoja yako again haijazingatia uhalisia ambao kwasasa mabinti wapo more interested na tamaa zao na sio mapenzi wala kupendwa on the other hand by average wanaume wapo more interested na mapenzi na mahusiano seiro ndio maana wapo busy kulalamikia tabia za hovyo za mabinti na wanawake wa kisasa.
Kwamba unataka kusema wanawake wakiingia kwenye mahusiano ni kwa ajili ya pesa tu lakini wanaume wakiingia kwenye mahusiano ndio wana mapenzi ya dhati, hivi huoni aibu kuandika huu uongo wako na kuupaka rangi ili uvutie na uonekane kuwa ndio ukweli yani wanawake wana matatizo gani hadi wote waingie kwenye mahusiano kwa ajili ya pesa tu na wanaume wana utakatifu gani hadi wote waingie kwenye mahusiano kwa ajili ya mapenzi, kwani ni wanaume wangapi wanaingia kwenye mahusiano kwa lengo la kupiga na kusepa tena wengine wakiwadanganya hao wanawake kuwa watawaoa mradi tu wapate wanachokitaka waondoke hivi kwanini wanaume mnapenda kujiona mko innocent sana
So by your own words una maanisha kuwa wanawake wana lack intelligence ya maamuzi sahihi juu ya miili yao kwamba mwanaume ndie mwenye last say juu ya bikra ya mwanamke na si yeye mwenyewe kutojua uzito na umuhimu wake?
Ndio maana nikakuambia nitajie umuhimu wa mwanamke kutunza bikira yake mpaka sasa hii hoja hujaijibu unarukaruka tu kama kitenesi, kwa sababu hata wanawake nao wanalipenda hilo tendo kwahiyo wakitunza bikira zao, maana yake wanakosa utamu wa lile tendo hivyo kusema wasubiri hadi ndoa ikiwa hawajui wataolewa lini na nani ni uongo usiowezekana
Kwahivyo wenye shida na hizo bikira ni wanaume na siyo wanawake na ndio maana ninyi ndio mnazipigia sana chapuo, ninyi wenyewe mnadai kuoa wanawake bikira kunawafanya mjisikie fahari na kujiona vidume pekee kwa hao wanawake mliowatoa bikira, kwahiyo tunaona bikira ya mwanamke haina faida kwa mwanamke mwenyewe bali kwa mwanaume atakayetoa
Sasa kitu kinachokufaidisha wewe mwenyewe kwanini hutaki kufanya jitahidi zozote kuhakikisha kinatunzwa unataka huyo mwenye nacho ndiye akitunze hadi ndoa, sawa wakati huo huo katika jitihada zake za kukitunza unamsumbua tena akupe kabla ya ndoa kisha akikubali unaanza kumtukana tena kuwa ni ujinga wake, halafu ukifika wakati unataka kuoa unaanza kukitafuta tena hicho kitu ulichokitoa kwa tamaa zako za kijinga na kushindwa kuvumilia hadi utakapomuoa mtoto wa watu
Again, unarudia hoja zile zile kwa maneno tofauti. Nimekujibu kule juu kuwa wewe unaassume kuwa mwanaume kwa wastani anapata idadi kubwa ya Wanawake wa kulala nao na kuwatoa bikra and its like unaongelea kuwa hii privilege wanaipata wanaume wote kwa wastani. Nikakufahamisha kule juu kwamba unafahamu kuwa kwa wastani mwanaume wa sasa anaweza fika hadi 35 na hajapata hata kukutana na mwanamke bikra? Na unajua wanaowala na kuwafungua mabikra kwa wastani ni kundi dogo sana la wanaume yaani 10% ya population ya wanaume wote. Na hao ni badboys,wanaume za watu na watu wenye pesa nyingi.
Hilo la kusema kwamba wanaume wanaowatoa bikira wanawake ni asilimia ndogo haliwezi kuwa kweli kwa sababu huna takwimu rasmi za idadi hiyo zaidi ya kutunga uongo wako ili mradi tu utetee hoja yako, na kama ni hivyo basi anzeni kwanza kuwakemea hao wanaume wenzenu mnaodai wanawamalizia hizo bikira kabla ya kuwakemea wanawake yani ambianeni ninyi kama ninyi wanaume kwamba wasiwatoe bikira wasichana ambao hawana malengo nao, na narudia kukuambia hoja siyo kutoa bikira tu bali ni kutembea na wanawake kabla ya ndoa hata ninyi ambao hamtoi bikira lakini bado mnatembea na wanawake na kuwaacha mnashiriki kuongeza mileage kwa hao wanawake sasa kwanini mwisho wa siku muende kutafuta ambao hawajatumika hawa waliotumika mnamuachia nani
Rejea juu kule it seems unasoma haraka haraka ujibu badala ya kuelewa kwanza una kichwa kigumu sana cha kuelewa unaonekana ni kabishi mno.
Yani bado nashangaa inakuwaje mimi ndio naonekana mbishi halafu wewe ambaye nabishana naye unajiona siyo mbishi kana kwamba hapa nabishana peke yangu wewe ungekuwa siyo mbishi si ungeacha kubishana, na hivi ndivyo namna mnavyofikiri kwenye kila angle wala sijakosea kuhusu ninyi hata kwenye mahusiano ndio ninachokisema hiki kwamba wewe na mwanamke mmetoka kufanya ngono halafu mkitoka hapo unamuita mwanamke mzinzi huku wewe ukijiona siyo mzinzi kana kwamba hilo tendo huyo mwanamke kafanya peke yake, halafu mbaya zaidi mnashindwa kuelezea the logic behind mnabaki kuleta visingizio visivyo na kichwa wala miguu na kudai eti ni nature ilihali hiyo nature yenyewe inawakataa
Prove me wrong badala ya kusema takwimu cha mchongo.
Hivi uliona wapi mtu anaanza kuwa proven wrong kabla yeye mwenyewe hajajiprove right kama siyo dalili ya kukwepa kuwajibika ni nini, yani wewe hujamaliza kuprove hizo takwimu zako za kubumba umejiandikia tu kutoka kichwani mwako halafu ghafla umenitwika mimi jukumu la kukuprove wrong umechanganyikiwa au, katika hali ya kawaida ukiraise issue yoyote inayohitaji ushahidi halafu hujaweka huo ushahidi maana yake lazima mtu akupinge hivyo ni jukumu lako wewe sasa kuweka huo ushahidi kisha ndio umuambie yeye akuprove wrong kwa ushahidi na siyo huu uhuni uliofanya wewe
So unaassume kila mwanaume anaishi maisha ya kingono?
Siyo mimi ninayeassume bali wanaume wenyewe ndio husema kwamba hakuna mwanaume asiyefanya ngono haijalishi kaoa au hajaoa
Majukumu kivipi,mfano diamond, Chris brown hawa unawafananisha na Wanaume wa kawaida kimafanikio?
Kinachokugharimu ni kuamini Mwanaume na mwanamke ni sawa na hivyo ni sahihi kuwa judge the same.
Mwanaume na mwanamke wanaweza kuwa tofauti kwenye masuala mengine ila siyo kwenye suala la ngono kwa sababu kwenye hilo suala ni kama pande mbili za shilingi, ninyi ndio mnaolazimisha huo utofauti hadi kwenye mambo mengine ambayo logic inakataa ili mradi tu mtetee maovu yenu, tendo linalohusisha jinsia zote mbili haliwezi kuwa kosa kwa jinsia moja halafu liwe sahihi kwa jinsia nyingine vinginevyo kama kwa wanawake ni kosa ilitakiwa wanaume wafanye na kina nani sasa
Kuchezea kwa namna gani? Ukisema kuchezea wanawake una maanisha kuwa wanawake wanakuwa serious na true intentions while wanaume wanakuwa hawapo serious na wanalenga kuwapotezea muda hao mabinti wakiwatumia kingono.
Hapana kuchezea ninakomaanisha mimi ni kwamba kwenye jamii yetu inachukuliwa kuwa mwanaume ana uwezo wa kupata mwanamke wa kuoa katika umri wowote ule hata miaka 50 lakini mwanamke akishafikisha miaka 30 tu tayari anaanza kuonekana mzee na ameshatumika, hivyo inakuwa ngumu kupata mwanaume wa maana wa kumuoa kwahiyo kutokana na mtazamo huu mwanaume na mwanamke wakiwa kwenye mahusiano kisha wakaachana lazima mwanamke ndio aonekane kapotezewa muda, sababu umri wake unazidi kuenda na uwezekano wa kuolewa unazidi kupungua so hii inawapa wanaume jeuri ya kuendelea kuchezea wanawake huku wakijua wao wako kwenye safe side na wana uwezo wa kuoa muda wowote suala la umri kuenda kwao siyo tatizo
Hivi wewe huwa unawasikiliza wanawake wenzako namna wakiwa wanapanga kumchuna,kudangia wanaume? Sio nyie akiitwa m'moja mnakuja crew nzima? Sio ninyi ambao mwanaume akikutongoza siku hiyo hiyo simu kioo kinavunjika, gesi inaisha,nywele zinafumuka, unataka huyu mwanaume akuchukulie serious wakati intentions zako ni kumtumia kumaliza shida zako?🤔
Lazima mjue hawa wanawake hawafanyi haya out of blue ni sababu wanajua siku hizi mapenzi hakuna wenyewe huwa mnasema hakuna mwanaume mwenye mwanamke mmoja, sasa assume mwanaume unatongoza wanawake saba kwa mpigo wote unawaambia unawapenda na wote unawaahidi utawaoa, ilihali unajua fika mwisho wa siku hapo utakuja kuoa mmoja tu kati yao wengine utawaacha au unaweza usiwaoe wote kabisa
Sasa kwa hali hiyo ndio mnataka mkipata wanawake wajicommit kwenu ilihali ninyi wenyewe hamjajicommit kwao mnakuwa mko kwenye majaribio tu, sasa kwanini na wanawake nao wasiangalie interests zao kwanza kisha wakiona mwanaume yuko serious ndio nao wanaamua kuwa serious, ninyi msichukulie poa suala la kujicommit kwa mtu halafu mwisho wa siku anakutenda
Ukumbuke mwanaume ndiye anayeamua anamuoa nani na anaoa lini mwanamke hawezi mlazimisha mwanaume amuoe, kwahiyo akiachwa anabaki kuugulia tu maumivu yake moyoni sasa ninyi sijui mnadhani wanawake wana mioyo ya vyuma, kwamba wakitendwa hawaumii hadi mnataka wawe wanajicommit kwenye mahusiano kirahisi rahisi tu
Mwanamke kuwa na hadhi au kushushwa ni yeye binafsi sio swala la mwanaume. Faida au hasara ni matokeo ya yeye amejiweka vipi. Madhara ya mwenendo wako mwanaume anaingaje sasa mbona unauliza swali la kitoto?
Mfano wewe umelala na wanaume mtaa mzima,unahisi utakuwa unachukuliwaje hapo mtaani kama mwanamke wa hadhi au takataka ya mtaa ambayo kila mtu anaweza pita nayo na kuikojolea akitaka?
Yani sijui kama unanielewa msingi wa huyo mwanamke kushushwa hadhi na kuchukuliwa kama takataka ni upi, kwa sababu mimi ninachojua mwanamke akifanya ngono naye anafaidi hilo tendo hivyo naye anajiburudisha nafsi yake sasa inakuwaje mtu aumie kwa kuifurahisha nafsi yake, wewe nipe hasara ya moja kwa moja anayopata mwanamke yeye kama yeye kwa kutojitunza usiniambie eti sijui wanaume watamdharau na kumshusha hadhi kwani yeye inampunguzia nini
Unahisi mwanaume anaoa ili iweje?🤔
Sasa ungewauliza wanaume wenzio ambao pamoja na mabaya yote ya wanawake wa sasa pamoja na sheria kali za mgawanyo wa mali baada ya talaka lakini bado wanaoa
Ushawahi kukutana na msemo "My body my choice" unajua maana yake?🤔 Kuna vingi haujui ila unaongea kwa kujiamini as if una uelewa mkubwa sana na jamii za majuu.
Huwa siongelei jambo ambalo sina uelewa nalo ukiona naliongelea jambo kwa kina basi ujue nina uelewa nalo au unataka mpaka niseme kwamba nimeshafanya kazi na hao watu na kutembelea baadhi ya nchi zao, ili mseme nina show off maana jf ndio pigo zenu hizo hata kama jambo ni la kawaida tu mnasema mtu ana show off kumbe ni inferiority complex ndio inawasumbua, kwahiyo mimi sina shaka na uelewa wangu kuhusu jamii za majuu na wala sihitaji validation kwenye hilo
Binti wa miaka 20 anakuwa kwenye dating app kutafuta nani exactly?😂 Au unasema yale mabonge nyanya yasiyo na mvuto at 20?
Si unaona sasa umehamisha tena magoli kutoka kusema ni mishangazi ya 30+ mpaka kusema ni mabinti wa 20s ila mabonge nyanya yasiyo na mvuto, maana hapa hoja ilikuwa ni wanawake kujazana kwenye dating sites wakishakosa wanaume baada ya kutumika, baada ya kuambiwa kwamba kuna mabinti unasema tena hawana mvuto ni nani aliyekuambia kwamba mabinti walioko huko ni wasio na mvuto na kingine aliyekuambia suala la mvuto ni objective ni nani
Nimekuuliza wewe kama wewe as a personal question usikwepe swali na majibu ya chenga. Jibu hilo swali,wewe kama ni mama wa mtoto wako wa kumzaa utasemaje acha kukwepa?🤔
Wewe katika hiyo scenario ungetumia approach gani? Hii ikupe taswira kamili ya unafiki wako
Jadda unapenda sana kukwepesha magoli.
Sijakuuliza maswala ya kazi,swali langu lipo very open na specific. Kama umeshindwa kujibu ni bora useme.
We sema tu ulitaka nikupe jibu linalokufurahisha wewe ila usiseme kwamba nimeshindwa kujibu maana huo mfano niliokupa ni relevant kabisa sema kwa vile umeona utakosa namna ya kuchomoka hapo, umejifanya kupotezea jibu langu na kusema sijajibu mimi nimeshakujibu kwamba kinachomatter siyo hisia zangu juu ya mwanamke ambaye kijana wangu angemchagua, bali ni sifa za mwanamke husika mimi siwezi kuchukua approach yoyote labda kama unataka niseme approach ambayo ungechukua wewe sasa
We kuelewa ni tatizo sana. Unaongea kitu unakibadilisha then mbeleni unakirudia tena kile kile ulichojibiwa unahoji tena. Wewe kule juu mimi nimeseme vipi kuhusu wanaume wanaooa hao wanawake ambao sisi tunasema hawana vigezo? Yaani mfano huyu Hamisa mobeto,hana vigezo vya kuwa mke wa mtu kaliwa na Diamond,alikiba,abdu kiba, Majizo,Rick Ross,yule jamaa mnaijeria,haya hao ni baadhi tu ya watu maarufu kuna ambao hatuwajui huko faraghani.
Bado ana watoto wawili with two different men. Halafu huyo Aziz K anakuja pigia goti,analipia ng'ombe 30, then wewe unakuja kuuliza why tunasema huyo Hamisa anaolewa na hana vigezo? Upo serious wewe?
Kaka yako au mdogo wako aliyefanikiwa kiuchumi akiwaletea mwanamke mwenye profile ya Hamisa mobeto wewe kama dada au mdogo mtu wa kike uta approve kaka yao au mdogo wako alete aina hiyo ya wifi awe mwanafamilia kwenu?🤔
Utakuwa kichaa ukisema ndio.
Yani hapa hoja ni kwamba wanawake type ya hamisa wanaolewa sana tu tofauti na ninyi mnaosema kwamba hawaolewi kabisa, mnaposema hao wanaume hawana akili mmetumia vigezo gani kuhitimisha hivyo siyo kwamba wasio na akili ni wale ambao wamerukaruka na wanawake huko halafu wakitaka kuoa wanadai bikira as if waliziweka, nasisitiza mwanaume yeyote ambaye ameshatembea na wanawake kadhaa enzi za ujana wake hana haki wala hastahili kudai bikira mnastahili hao hao wanawake mliowatumia ndio maana wanawake wengi hawakubali kuolewa na ninyi wakiwa bikira nature inawahukumu ninyi kwa staili hiyo
Wewe unavyosema wanawake wasiojitunza wanaolewa vizuri tu, hivi upo serious? Huku mtaani hawa masingle mother ni akina nani hawa? Wewe pia hapo mfano hai hapo umeolewa?🤔 Tabia zako za ubishi na ujuaji unajiona ukienda kuwa mke wa mtu na ukawa mtii na mwenye heshima kwa mumeo?
Haya ni maoni yako na ni kufahamishe kuwa upo wrong. Nipe jibu moja wewe umeolewa hapo ulipo na una miaka mingapi kufika 30?
Sasa mimi kuolewa au kutokuolewa inahusiana nini na mada kwani marital status yangu mimi ndio itatoa picha halisi ya mamilioni ya wanawake walioko kwenye jamii, wewe ukishaijua marital status yangu ndio itabadili ukweli kwamba hata wanawake wasiojitunza nao wanaolewa tena kwa wingi kuliko hao mabikira, hao ambao bado hawajaolewa ni suala la muda tu lakini wote tunajionea hali halisi wanawake wengi wanaoolewa ni hao hao waliotumika kuliko mabikira sababu mabinti wengi bikira zinatolewa mapema kabla hawajakubali kuingia kwenye ndoa
🤔
Injiri itaendelea kusonga mbele. Tutawala na kuwahonga but heshima ya ndoa ni ya bikra sio mwanamke asiyetunza mwili wake. Ukiona hauna bikra na umevalishwa pete then umeonewa huruma but hauna hiyo hadhi.
Hapa umeendelea kubadili maneno tena kwamba kama hujajitunza na umeolewa basi umeonewa huruma tu wakati mwanzo wimbo ulikuwa unasema kama hujajitunza basi huolewi kabisa, hapo pa kuendelea kuwala na kuwahonga ndipo hasa ninaposisitiza kwamba hamuwakomoi wanawake bali mnajikomoa wenyewe, sana sana mnawafaidisha hao wanawake kiuchumi halafu mwisho wa siku mkitaka kuoa hizo bikira mnazisaka kwa manati na wengi wenu kuzikosa na kurudi kuoa hao hao mliowatumia na kujifariji kuwa mmechagua angalau wenye 'afadhali'
Swali lako sijalielewa maana umeuliza kama as if wew sio mwanamke na hauna ufahamu mwanamke ana stahiki kuwa namna gani ili kuitwa mke bora.
SIfa za mke bora zinatofautiana baina ya jamii, kuna jamii mke bora ni yule anayemsaidia mumewe majukumu kutafuta pesa na kuchangia uchumi wa familia, sasa jambo likishatofautiana baina ya jamii hakuna namna utalazimisha kwamba jamii fulani ndio iko sahihi na nyingine haiko sahihi
Sio tu mwanamke hata dumu la maji atalitomba akikosa demu ila sasa ataoa dumu la maji? 🤔
Mwanaume hawezi kosa mwanamke wa kufanya nae na hao wapo wengi tu wengine ni wake za watu. But issue tunaongelea wanawake ambao wanataka kuingia ndoani ila maandalizi yao ni hafifu.
Na hapo ndipo tatizo hasa lilipo mnanichanganya mnaposema mwanaume hawezi kukosa mwanamke wa kufanya naye sasa hao wanawake atawatoa wapi ikiwa mnataka wote wajitunze, tuseme labda jamii ikaamua kuanzia sasa mabinti wote wenye bikira hakuna kufanya ngono hadi pale watakapoolewa maana yake hiki kizazi cha wasiojitunza kitaenda kitaisha kitabaki cha wanaojitunza sasa ndio nauliza katika kizazi hicho wanaume watafanya na kina nani kabla ya ndoa, unaposema watafanya na wake za watu maana yake unaona ni sawa vijana kutembea na wake za watu mind you katika hoja yetu hii tunaassume kwamba wake za watu wa kizazi hicho wote wataolewa mabikira hivyo hawatacheat maana mnasema mwanamke akiolewa bikira hawezi cheat sasa hao wanaume watafanya na kina nani
Huwa haupingi na haupo specific na hoja zako una hama hama. Kama kweli una hoja tengeneza uzi. Wewe huwa tunakutana kwenye comment sections tu ila sio kwenye uzi wako maalumu.
Ni sheria gani inayonitaka kila ninapowakosoa wanaume basi nianzishe uzi wangu kwani nikiandika kwenye comments ujumbe haufiki au tofauti yake ni nini na nikiandika uzi, by the way kuna nyuzi kibao tu nimeanzisha kuhusu both wanaume na wanawake kama una muda fuatilia labda wewe ni mgeni jf ila wanaonifahamu wanajua namna nilivyokuwaga naanzisha mada za aina hii, kinachonifanya nisianzishe nyuzi za aina hii ni sababu wanaume wengi huwa hamna hoja badala ya kujikita kwenye mada mnaanza kunishambulia mimi mtoa mada sasa unataka nani apoteze muda wake kujishana na watu kama hao mimi ukija na hoja tutaenda sambamba ila ukija na matusi nakuacha ukatafute mahali pengine pa kumalizia stress zako
Soma tena vizuri. Nimesema utajiri sio kipimo pekee au cha msingi cha mwanaume.
Basi kama ni hivyo acheni kusema kwamba thamani na ubora wa mwanaume katika kuoa unapimwa kwa pesa, maana kwa kusema hivyo tayari mnakuwa mnajicontradict kwa sababu kwa mujibu wenu ni kwamba kumbe hata mwanaume masikini anaweza kuoa, by the way kama ubora na thamani ya mwanaume havipimwi kwa pesa tu niambie katika hali ya kawaida kati ya masikini aliyeoa bikira na tajiri aliyeoa single mother ni nani anayeheshimika hapo
Na mimi nakwambia tena ni wajinga kwasababu hakuna sifa hata moja inayoreflect uanaume katika maamuzi yao. Unaita sio wajinga kwasababu ujinga wao ndio unaowafanya ninyi wanawake wa sampuli yako msio na vigezo vya kuwa mke wa mtu mpate mabwege wa kuwapumzisha.
Yani unavyoandika ni kana kwamba wanaume ni watoto wadogo wana akili za kushikiwa na hawajui wanachofanya, hivi toka wanaume wameanza kuimbiwa hizi ngonjera zenu za kuacha kuoa wanawake wasiojitunza tena na shuhuda juu toka kwa ndugu na jamaa unaona kuna hatua zozote zimechukuliwa au dalili zozote za wanaume kuacha kuoa wanawake wa aina hiyo, unadhani wao hawaujui umuhimu wa bikira au unadhani hawajui ni wapi pa kuwapata wanawake mabikira ukishajiuliza hayo jiulize kwanini bado wanaoa hao hao wanawake wasiojitunza kisha uniambie kosa la hao wanawake liko wapi hapo ikiwa wanaume ndio wenye maamuzi ya kuoa
Hiyo sio kazi yetu sababu tunaamini wanawake wanauwezo wa kujua baya na zuri na wanaweza kufanya maamuzi sahihi. Mbona hamkubali kukaa nyumbani na kuwa wavumilivu kwa wanaume wakitoka kutafuta chochote kitu huko uraiani.
Oohh kwahiyo wanawake tu ndio wenye uwezo wa kujua baya na zuri ila wanaume ndio hamna uwezo huo, wanawake nao wanaangalia mambo yanayowafaidisha sasa kama kutoka kutafuta chochote kitu kunawafaidisha kwanini wakomae kukaa nyumbani, sidhani kama kuna mtu anakubali kufanya jambo ambalo halimfaidishi hata kidogo kama wanawake wanaamua kukubali kufanya ngono kabla ya ndoa maana yake nao wanafaidi hiyo ngono wangekuwa hawafaidi basi wasingefanya
Hivi unadhani kijana anaefanya ngono anakuwa interested na bikra ya mwanamke?
Kwamba wanaume wote wenye interest na bikira za wanawake hawafanyi ngono ama unataka kusemaje hapo
🤔
Mwanaume akitomba nje anapata ujuzi na namna ya kuishi na mwanamke anamuelewa vema. Mwanamke akiliwa nje anaharibu maumbile yake,anarisk kubeba na kutoa mimba hovyo,anakuwa na mfadhaiko wa kihisia hatoweza tulia na mwanaume m'moja.
Again, acha kulinganisha mwanaume na mwanamke.
Sasa mimi ndio nataka nijue huo ujuzi wanaume wataupata wapi ikiwa wanawake wote wanatakiwa kujitunza, mbona kama hamjui mnachokitaka wala mnachokipigania kama wanawake wote wakijitunza wanaume watafanya na kina nani, hapo ndipo ninapotaka sasa niuone huo utofauti kati ya mwanamke na mwanaume linapokuja kwenye suala la ngono hebu fafanua vizuri
Ingekuwa mi mimi tu nakusema hivyo ningesema sawa but haustaajabu watu tofauti kukuona na shida ya aina moja?
Unajua unachokifanya,yaani kubishana. Ikifika watu wanakudescribe kwa assumption then jua umefika point wanastaajabu kuwa unafananiaje in real life.
Tatizo siyo watu kunidescribe tatizo ni aina ya watu wanaonidescribe wote ni wale wale misogynists aina ya wanaume ambao mada zao kutwa ni za kutukana wanawake tu na mbaya zaidi ninyi hamjioni kama mna matatizo ila wanawake wakikosoa wanaume ndio wana matatizo, mimi mbona kuna wanaume wengi tu humu huwa wananisifia na kunipongeza kwa mitazamo yangu hii hii sasa kipi kinachofanya ninyi misogynists muwe sahihi juu yangu na wao ndio wawe wanakosea, by the way usichokijua mimi kinachonipa nguvu ya kuendelea kuwakosoa wanaume ni ile jeuri ya kwamba sijachezewa na wanaume niko kwenye safe side, tofauti na wanawake wengi wa humu jf waliochezewa ndio huwa wanaogopa kuwakosoa sababu zile personal attacks zenu zinawaumiza maana kwao ni ukweli mchungu, ila sisi wengine huwa hatuumii wala hatujali sababu tunajijua hatuko hivyo mnavyotusema yani kwa kifupi mngejua jinsi mwenzenu ninavyowachora na kuona kama mnajifariji tu na stress zenu sababu yote mnayojisemesha kuhusu mimi hayana ukweli so hainiathiri chochote
Kwasababu huwa unaanzisha counter arguments na haukubali kuelewa upande wa pili. Mfano naweza kusema ,Juice ya embe ni kiboko" wewe unarespond " Kwann embe tu, mbona kuna maparachichi na ni kiboko pia".
Kwa waliosoma cuba wanajua tu hapa huyu mtu anataka tu kuanzisha mijadala nje ya mada kwani nikipenda embe bila kupenda parachichi ninakuwa sipo sahihi? Kwann kwanza ulete hoja ya parachichi kwenye mjadala wa maembe ?
This is how you come off as an argumentative and illogical being to others .
Tatizo siyo wewe kupenda juisi ya embe tatizo ni kusifia juisi ya embe na kuponda juisi ya parachichi kama umeamua kusifia basi sifia ya embe bila kuponda ya parachichi, tena mbaya zaidi katika kusifia na kuponda huko unageneralize na kulazimisha kwamba juisi ya embe ni nzuri kwa kila mtu na ya parachichi ni mbaya kwa kila mtu, kwahiyo wewe ndiye unayetakiwa kuwa makini na namna unavyowasilisha hoja zako vinginevyo ukikosolewa usianze kulialia kwamba watu wanapenda kubishana na kuhamisha mada