Zijue sababu za wanaKigoma kumpokea kwa wingi Rais Samia

Zijue sababu za wanaKigoma kumpokea kwa wingi Rais Samia

Mama Kaja Kigoma na baraka kubwa sana.
Mvua ya baraka imenyesha sana leo.
hii ni ishara kuwa Rais wetu ana baraka tele.
Mungu aendelee kumlinda.
Kweli kabisa inaonyesha hata mbigu zinafunguka kwaajili yake Rais Samia Suluhu amefanya jambo kubwa sana Kigoma maana ilisahaulika kwa miaka mingi sana
 
Hakuna sababu yoyote ile ila ni "ushamba" tu ndio unawasumbua. Ushamba wa ving'ora na msafara wa Rais ndio vimewafanya wajazane hapo.
Mikoa ya pembezoni mwa nchi bado watu wengi ni "washamba washamba " sana.
Mikoa ya Rukwa, Katavi, Kagera, Lindi na nyanda za juu kusini bado kuna "ushamba" mwingi mno.
Punguza makasiliko mkuu Rais Samia Suluhu ni kipenzi cha watu kila anakopita watu wanaitika
 
Yaani kiti cha maana kigoma ni kuanzisha ujenzi wa soko ambayo limeshabomolewa kwa ajili ya kujengwa upya! Pia kuangazia ukarabati wa meli na bandari ya kigoma bila hayo ni blahblah tu!
Kwaiyo wewe umeme, maji, shule unaona havina maana punguza makasili Rais Samia Suluhu anaupiga mwingi
 
Kweli kabisa inaonyesha hata mbigu zinafunguka kwaajili yake Rais Samia Suluhu amefanya jambo kubwa sana Kigoma maana ilisahaulika kwa miaka mingi sana
uko sahihi kabisaa, hizi ndizo dalili za mtu wa Mungu mwenye baraka.
Mungu azidi kumlinda.
 
Je!
Yote hayo yameanza na kukamilika ndani ya miaka hii miwili ya Samia Madarakani?

Je!
Katika hizo Barabara unazozitaja,ebu tutajie hata moja tu ambayo Samia alihusika kuweka jiwe la msingi wa kuanzishwa kwa ujenzi wake!

Hii umati ni nguvu ya ziada inayotumika kutoka kwa wabunge na wateule wa Rais,ili kujipendekeza kwamba wako nae sambamba ila ukweli ni kwamba wanatetea kitumbua chao.

Unaita umati wote huo halafu hutski maswali ya moja kwa moja kujua kero zao?

Bullshit propaganda hizo!

Na ni bahati yenu humu JF hakuna identity,ila kwa ujumla mleta mada ni bonge la mpumbavu!

Hata Magufuli alijaza umati mara mbili ya huo.....lakini leo hii umepotelea wapi huko CCM?

Si ndio hao hao wanaomnanga kila uchao?
Hakuna aliesema jpm hajafanya mambo Rais Samia Suluhu aliahidi kumalizia kila kilichaochwa na mtangulizi wake na sasa amefanikiwa kumaliza miradi kwa wakati mama anaupiga mwingi sana kigoma ni sehemu iliyokua imesahaulika lakini mama amepeleka maendeleo mengi na anahakikisha na sasa kigoma itakua mji wa kibishara
 
Amewapelekea neema au ni wajibu wa serikali? Mnapoteza fedha za umma kulazimisha watu kuwasujudia kwa kodi zao!
Lakini kumbuka awamu ya sita ndio imewakumbuka maana walikaa miaka mingi bila maendeleo lakini Rais Samia Suluhu ameganikisha umeme wa uhakika, elimu maji miundombinu
 
Lakini kumbuka awamu ya sita ndio imewakumbuka maana walikaa miaka mingi bila maendeleo lakini Rais Samia Suluhu ameganikisha umeme wa uhakika, elimu maji miundombinu

Hayo yako kwenye mipango Muda wote, na kodi zetu kila tunaponunua Luku ndio zimetumika. Hata kama Samia asingekuwa madarakani. Usitake kufanya kuwa Samia kafanya kama hisani. Labda kwa wajinga ndio wataamini ni upendo wa rais kwao na sio kodi zao.
 
MARIO, NANDY, HARMONIZE, TOT BAND, KWA YA UTUMISHI WA UMMA, BENDI YA JKT MAKUTUPOLA

hapo kwanini watu wasijae?!
 
Wanakigoma au wanafunzi? Hiyo mbinu ya kuzoa wananchi kwa malori, na kutaka watumishi wa umma kuhudhuria kwa shuruti ni mbinu so outdated. Mnaishia kutumia kodi za wananchi vibaya kwa kusaka kiki za kisiasa.
Imewauma kweli kweli, pia unaangaliwa uwezekano treni ya SGR kufika kigoma maana ndipo itakapolipa zaidi, tusikosee kama kenya kutengeneza SGR ya Nairobi to mombasa ambayo inawapa hasara tucheze kiakili na mradi huu wa SGR, DAR PORT TO BY ANY MEANS KIGOMA, BURUNDI KIGALI DRC
 
Wanakigoma au wanafunzi? Hiyo mbinu ya kuzoa wananchi kwa malori, na kutaka watumishi wa umma kuhudhuria kwa shuruti ni mbinu so outdated. Mnaishia kutumia kodi za wananchi vibaya kwa kusaka kiki za kisiasa.
Umeongea ukweli mtupu , Hawa husomba watu kila wilaya lengo onesha eti anakubalika kumbe hamna kitu, dawati la Siasa la chama ichi lina mbinu nyepesi sana
 
Tatizo watu wengine mmeshazoea kupinga kila kitu sasa hapo nani anaonekana amelazimishwa wananchi ni wazalendo na wanaona Rais Samia Suluhu amewapekelea neema Kigoma, maana ilisahaulika kabisa.
Acheni mambo ya ajabu, hizo sifa zote ulizoandika mbona hazionekani katika nyuso zao?
Mnalundika watu kushangaa misafara yenu ya magari na mbwembwe kwa watu wengi wasio na shughuli za kufanya kisha mnawatumia kuwa wanawaunga mkono?
Kenyatta Sr. aliziita hizi akili za maiti

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Wanakigoma au wanafunzi? Hiyo mbinu ya kuzoa wananchi kwa malori, na kutaka watumishi wa umma kuhudhuria kwa shuruti ni mbinu so outdated. Mnaishia kutumia kodi za wananchi vibaya kwa kusaka kiki za kisiasa.
Zuchu was Nini?
Alipeleka ujumbegani?
Wakigoma sio mazuzu
Subirini uchaguzi mtajua
 
Acha kudanganya

WAMEKUJA kuona wasanii!

Hata Mimi akija tu lazima nikamuone ni Haki yangu kwenda!!

Halafu lini mnawaacha na wapinzani nao wafanye siasa!!

NCHI ya kidemokrasia HII!!
 
Ngoja nikusaidie kitu inawezekana kigoma huijiui vizuri
Kigoma haina umeme wa uhakika hata baada ya kuunga grid ya taifa kwa baadhi ya wilaya bado mambo yaliendelea kuwa Yale Yale ya kukatika umeme mara kwa mara, hadi jana anaingia kigoma mjini kulikua hamna umeme zaidi ya masaa ma 4 sasa sijui ni umeme upi wa uhakika unao zungumzia

Kwenye miundo mbinu ya barabara serikali imejitahidi kwa kiasi Fulani imefanya vizuri tangu kipindi cha "Mjomba", sasa hivi kuna maeneo ukifika unakuta barabara zina tengenezwa Kila siku kwa hilo naunga mkono hoja

Hapa kwenye Elimu bado kuna shida Sana, hadi Leo bado kuna shule tena za mjini watoto wanakaa chini kwenye madarasa mapya yaliyo jengwa kwa mkopo wa COVID 19, kwenye vyoo vya shule ndio usiseme kabisa ni vituko achilia mbali walimu na vifaa vya kufundishia

Kwenye maji na penyewe ni shida vile vile, japo kigoma ina ziwa Tanganyika lakini maji ni shida, kuna maeneo wana kaa hadi siku 7 bila maji yani ni mgao kwa kwenda mbele, ukienda wilaya za mbali na ziwa watu wengine huko wanategemea maji ya mito na mabwawa ambayo sio salama kwa afya zao,
kuna mradi mkubwa wa maji aliuacha magufuli, ika semekana utakua ni mwarobaini wa shida ya maji kigoma lakini shida Iko pale pale
sasa ni uhakika upi wa maji unao zungumzia wewe

Muambieni ukweli ili atatue shida za wenye nchi sio kumsifia hata kwa vitu ambavyo havipo,
 
Back
Top Bottom